Uchaguzi 2020 Ushawishi wa Salum Mwalimu (CHADEMA) kisiasa huenda ni mara 5 zaidi ya Samia Suluhu (CCM)

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,129
35,148
Nimekuwa nikifuatilia kampeni za wagombea wenza wa urais baina ya Salum Mwalimu (CHADEMA) dhidi ya Samia Suluhu (CCM) na kwa hakika kuna tofauti kubwa sana.

Nilijikita kuchambua kwenye mambo muhimu matano tu (Handira, Hamasa, Hoja, Ushawishi na Upeo). Bila shaka utagundua wazi kabisa kuwa, uwezo wa Salum Mwalimu kisiasa uko juu mnoo ikiwa utamlinganisha na Samia Suluhu katika hayo mambo matano. Yaani kampeni zimeshika kasi lakini Samia Suluhu ameshindwa kuwa gumzo katika majukwaa ya kisiasa wakati Magufuli yupo kwenye mapumziko ya kampeni.

Binafsi sioni faida ya Samia Suluhu katika kumsakia kura Magufuli. Amepwaya sana. Samia amekuwa kama kivuli kisichoonekana. Yaani Samia Suluhu kampeni zake zina Hadhira ndogo, Hamasa kidogo, Hoja zisizovutia wahudhuriaji, Ushawishi duni na Upeo mwenye kutia mashaka sana.

Mama Samia anakwama wapi?
 
Ingawa mimi ni CCM, ila yupo mgombea mmoja wa CHADEMA amefanya kampeni nzuri sana, bahati mbaya anakaa Geita ila ningempa kura yangu! huyu apa


Laiti kampeni za CHADEMA zingekua ivi, tungekua na imani na uongozi
 
Nimekuwa nikifuatilia kampeni za wagombea wenza wa urais baina ya Salum Mwalimu (CHADEMA) dhidi ya Samia Suluhu (CCM) na kwa hakika kuna tofauti kubwa sana....
Kumbuka mama Samia ni makamu wa Rais, anafanya mambo kwa heshima na utaratibu kulingana na hadhi yake, anaongea kwa hoja, anachagua cha kuongea, anajua aongee nini kutokana na watu anaokutana nao, hawezi kubwabwaja hovyo tu kama Salum Mwalimu.
 
Kumbuka mama Samia ni makamu wa rais, anafanya mambo kwa heshima na utaratibu kulingana na hadhi yake, anaongea kwa hoja, anachagua cha kuongea, anajua aongee nini kutokana na watu anaokutana nao, hawezi kubwabwaja hovyo tu kama salum mwalimu.
Haijalishi hizo ulizotaja ndio zingempa uwezo wa ushawishi
 
Kumbuka mama Samia ni makamu wa rais, anafanya mambo kwa heshima na utaratibu kulingana na hadhi yake, anaongea kwa hoja, anachagua cha kuongea, anajua aongee nini kutokana na watu anaokutana nao, hawezi kubwabwaja hovyo tu kama salum mwalimu.
Na Magufuli anayeongea kama katoka msalani je?
 
Haaaaahaaa huyu ni Upendo Peneza,anashuka mistari huyo

Kwakweli anafanya kampeni nzuri sana. hio video comment wote wamemnyooshea mikono amna aliempinga wote CCM na CHADEMA!

Ila yule kichaa mwingine naona wamefunga comments kwenye youtube channel yao, na wanasema uhuru wa kutoa maoni wanaupigania, kwa kwel baada ya uchaguzi, zile kesi ziendelee mapema sana
 
Kumbuka mama Samia ni makamu wa rais, anafanya mambo kwa heshima na utaratibu kulingana na hadhi yake, anaongea kwa hoja, anachagua cha kuongea, anajua aongee nini kutokana na watu anaokutana nao, hawezi kubwabwaja hovyo tu kama salum mwalimu.
Mbona anayemuombea kura anabwabwaja tuu? Hujawahi kumsikiliza? Anatamani hadi wasichana apewe wa kulala nao?
 
Back
Top Bottom