(Sina uandishi wala usimulizi mzuri)
Binafsi tangu mwanzo nilitumikishw katika ngono,
Nimeishi muda mrefu nikiwa na mgogoro mkubwa sana wa nafsi bila kujua chanzo ni nini!, mitafaruku isiyoisha, mahusiano mabaya na watu wote hadi ndugu,
Shuleni sikufanya vizuri,
Kazini nimeteseka sana,
Mahusiano mabovu, mikosi kila leo,
Mambo yalivyozidi kuniharibikia sana kutokana na tabia ya uzinzi huku sielewi chanzo ni nini,
Nikajikuta naingia kwenye pombe,
Yaani nikajikuta nna mambo mawili yanayonitumikisha, uzinzi na pombe,
Kiukweli nimeteseka sana bila kujua,
Pesa hazikai, biashara nilizoanzisha zilikufa zote ndani ya muda mfupi,
Uharibifu ulionipata ni mwingi sana,
Nilifedheheka sana ndugu zangu maana hata sikuweza kufanikisha jambo lolote la maana.
Nilianza kutembea kwa waganga kwamba nimerogwa ndio maana mikosi hainiishi,
Nikauliza hadi magwiji wa waganga humu,
Kote nikaenda, niliishia Kuliwa na kupoteza pesa, bila msaada hata tone,
Wazo likaniijia niende kwa wataalam wa nyumbani nilipozaliwa,
Nikajipanga nikaenda nyumbani, ingawa wazazi wote walishalala, ila niliamini Kuna msaada,
Ile nimefika nyumbani, nikasikia sauti ikiniambia!
"mateso yangu yote chanzo ni uzinzi"
Ingawa nilienda kwa mtaalam wa huko nyumbani lakini hakuwa na jipya lolote.
Kurudi nikaanza kufanyia kazi kuachana kabisa na wanawake nibaki na mke tu,
Ingawa mwanzoni ilikuw ngumu, hadi nikajikuta narudi kwa mchepuko wangu niliokuw nauamin kuwa huenda una kismati,
lakini cha kushangaza niliishia kupoteza laki 5 bila kufahamu, plus fedheha nyingi kwenye pombe.
Tangia hapo nikaacha uzinzi na tatizo la pombe nalo limekata,
Namshukuru Mungu, mdogomdogo naanza kuona mkono wake.