Ushauri wenu ndugu zangu pombe inanitesa

Ushauri wenu ndugu zangu pombe inanitesa

Ngumu sana kutoka mwenyewe... Lazima apate support kutoka nje
Hiyo support Toka nje, ndio inahitaji utayari wake ili aweze kutoka. All in all, anaonekana yupo tayari, so akipata right guidance anafanikiwa
 
Wadau habari za muda huu,

Nianze kwa kusema mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 30, nafanya kazi katika kampuni fulani mshahara laki 3, bado naishi kwa wazazi napanga kutoka lakini nashindwa.

Kikubwa ni unywaji wa pombe, yaani kila nikipokea kamshahara akili inanituma kunywa tuu na nikinywa napoteza mali zangu, Pesa, simu, viatu n.k.

Ushauri tafadhali hali ni mbaya. Nini nikifanye kuepukana na hali hii, maana binafsi siipendi ila najikuta tayari nipo huko na majuto ni baada ya pombe kuisha kichwani?

NB: Nimeandika kwa stress mno maana hapa nilipo nimeshapoteza laki 2 jana usiku.

Ahsanteni.
Pole sana pitia hapa kitambaa cheupe tabata tuzungumze zaidi swala lako..inasikitisha sana.
 
Amua kuacha
Mshirikishe na Mungu pia.
 
Write your reply...huyo alokupa namba ya mtaalam angalia sn usikubal kupewa dawa unywe et itakusaidia kuacha pombe ooh my friend we will loose you
 
Wadau habari za muda huu,

Nianze kwa kusema mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 30, nafanya kazi katika kampuni fulani mshahara laki 3, bado naishi kwa wazazi napanga kutoka lakini nashindwa.

Kikubwa ni unywaji wa pombe, yaani kila nikipokea kamshahara akili inanituma kunywa tuu na nikinywa napoteza mali zangu, Pesa, simu, viatu n.k.

Ushauri tafadhali hali ni mbaya. Nini nikifanye kuepukana na hali hii, maana binafsi siipendi ila najikuta tayari nipo huko na majuto ni baada ya pombe kuisha kichwani?

NB: Nimeandika kwa stress mno maana hapa nilipo nimeshapoteza laki 2 jana usiku.

Ahsanteni.
Pole sana kijana.

Wewe haujafikia hatua ya kulewa pombe kama nilizokuwa nikinywa mimi na kuna simulizi niliwahi kuitoa kushuhudia humu Jf.

Mimi niliacha kwa dhamira kama nilivyoona members wengi wamekushauri, hicho ndiyo cha muhimu sana, dhamira itoke moyoni mwako kwanza.

Kingine kilichonisaidia baada ya kuacha ni kufuta kabisa ratiba za kupita kwenye ma bar ama maduka ya vileo ulikozoea kupata vilevi.

Jambo la tatu hakikisha unaazisha miradi utakayoifanya baada ya kutoka kazini itakayokunyima wewe muda wa kukosa cha kufanya!

Ukishinda hatua hizo, kuna ndoto zitaanza kukuandama kuota upo kwenye madaramu ya pombe ukiogelea, umechafua meza ukinywa nk nk, kwa kweli zitakusumbua sana na hiyo ni ishara ya ushindi.

Ukishinda vita hii, hakikisha unaviepuka vishawishi vyovyote vya kukufanya uonje pombe hata kama ni kwenye sherehe ya kuzaliwa kwako ama siku yako ya ndoa usithubutu kuja kuonja pombe kabisa.

Ukija kuonja kwa kisingizio chochote, shetani wa pombe atarudi kwa kasi ya mwanga na hautakuja kushinda majaribu hayo tena mpaka kufa kwako.
 
Pole sana kijana.

Wewe haujafikia hatua ya kulewa pombe kama nilizokuwa nikinywa mimi na kuna simulizi niliwahi kuitoa kushuhudia humu Jf.

Mimi niliacha kwa dhamira kama nilivyoona members wengi wamekushauri, hicho ndoyo cha muhimu sana, dhamira itoke moyoni mwako.

Kingine kilichonisaidia baada ya kuacha ni kufuta kabisa ratiba za kupita kwenye ma bar ama maduka ya vileo ulikozoea kupata vilevi.

Jambo la tatu hakikisha unaazisha miradi utakayoifanya baada ya kutoka kazini itakayokunyima wewe muda wa kukosa cha kufanya!

Ukishinda hatua hizo, kuna ndoto zitaanza kukuandama kuota upo kwenye madaramu ya pombe ukiogelea, umechafua meza ukinywa nk nk, kwa kweli zitakusumbua sana na hiyo ni ishara ya ushindi.

Ukishinda vita hii, hakikisha unaviepuka vishawishi vyovyote vya kukufanya uonje pombe hata kama ni kwenye sherehe ya kuzaliwa kwako ama siku yako ya ndoa usithubutu kuja kuonja pombe kabisa.

Ukija kuonja kwa kisingizio chochote, shetani wa pombe atarudi kwa kasi ya mwanga na hautakuja kushinda majaribu hayo tena mpaka kufa kwako.
Ahsante kwa ushauri mzuri mkuu
 
Pole sana kijana.

Wewe haujafikia hatua ya kulewa pombe kama nilizokuwa nikinywa mimi na kuna simulizi niliwahi kuitoa kushuhudia humu Jf.

Mimi niliacha kwa dhamira kama nilivyoona members wengi wamekushauri, hicho ndoyo cha muhimu sana, dhamira itoke moyoni mwako.

Kingine kilichonisaidia baada ya kuacha ni kufuta kabisa ratiba za kupita kwenye ma bar ama maduka ya vileo ulikozoea kupata vilevi.

Jambo la tatu hakikisha unaazisha miradi utakayoifanya baada ya kutoka kazini itakayokunyima wewe muda wa kukosa cha kufanya!

Ukishinda hatua hizo, kuna ndoto zitaanza kukuandama kuota upo kwenye madaramu ya pombe ukiogelea, umechafua meza ukinywa nk nk, kwa kweli zitakusumbua sana na hiyo ni ishara ya ushindi.

Ukishinda vita hii, hakikisha unaviepuka vishawishi vyovyote vya kukufanya uonje pombe hata kama ni kwenye sherehe ya kuzaliwa kwako ama siku yako ya ndoa usithubutu kuja kuonja pombe kabisa.

Ukija kuonja kwa kisingizio chochote, shetani wa pombe atarudi kwa kasi ya mwanga na hautakuja kushinda majaribu hayo tena mpaka kufa kwako.
Kumbe pombe ni shetani... Kama ni shetani lazima uwe karibu na Mungu ili akuachiee...
 
NB: Nimeandika kwa stress mno maana hapa nilipo nimeshapoteza laki 2 jana usiku.

Ahsanteni.
Pitia Uzi wa wenzako hapa👇👇

 
Wadau habari za muda huu,

Nianze kwa kusema mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 30, nafanya kazi katika kampuni fulani mshahara laki 3, bado naishi kwa wazazi napanga kutoka lakini nashindwa.

Kikubwa ni unywaji wa pombe, yaani kila nikipokea kamshahara akili inanituma kunywa tuu na nikinywa napoteza mali zangu, Pesa, simu, viatu n.k.

Ushauri tafadhali hali ni mbaya. Nini nikifanye kuepukana na hali hii, maana binafsi siipendi ila najikuta tayari nipo huko na majuto ni baada ya pombe kuisha kichwani?

NB: Nimeandika kwa stress mno maana hapa nilipo nimeshapoteza laki 2 jana usiku.

Ahsanteni.
Hata tukikueleza huku tunalia,kama hautofanya uamuzi kuanzia na nafsi yako ili uache pombe kwanza,tutakuwa tunapaka rangi upepo.Acha pombe.Jiahidi kwa dhati kutulia.Fanya maombi na ujirudi kiroho.Anza polepole kujifunza bajeti na uchoyo hadi kwa nafsi yako kwa kujiwekea malengo ya maendeleo.
NB:Mimi mwenyewe naigonga ile ngumu.Naomba uache kunywa ili utuachie my wetu.Hapo mwisho ni utani usichukie.
 
Kinachokufanya unywe pombe, ni mazingira ya uuzwaji wa pombe a.k.a totoz; tafuta mwanamke mmoja awe anakuweka bize na asiwe mnywaji.
 
Tafuta haka kakitabu, mimi kalinisaidia sana.

Ifahamu pombe.png
 
Wadau habari za muda huu,

Nianze kwa kusema mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 30, nafanya kazi katika kampuni fulani mshahara laki 3, bado naishi kwa wazazi napanga kutoka lakini nashindwa.

Kikubwa ni unywaji wa pombe, yaani kila nikipokea kamshahara akili inanituma kunywa tuu na nikinywa napoteza mali zangu, Pesa, simu, viatu n.k.

Ushauri tafadhali hali ni mbaya. Nini nikifanye kuepukana na hali hii, maana binafsi siipendi ila najikuta tayari nipo huko na majuto ni baada ya pombe kuisha kichwani?

NB: Nimeandika kwa stress mno maana hapa nilipo nimeshapoteza laki 2 jana usiku.

Ahsanteni.
Pole sana ndugu! Hapo ni kwamba umeshapata addiction. Mimi nikutie moyo kwamba umshirikishe Mungu katika vita hiyo iliyo ndani yako

Na nikuambie kabisa ukweli kwamba kutoka katika hilo ulipitialo sio jambo jepesi hata kidogo

Kubali moyoni mwako kwamba ipo vita ngumu sana ambayo unakabiliana nayo, kisha amua kwamba unautaka ushindi

Na pia nikuambie haupo peke yako unayepitia kama hayo la hasha! Mfano mzuri ni kwenye maandiko haya matakatifu kwenye biblia


"Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo."
Rum 7:19 SUV
Huyo ni mtumishi wa Mungu Paulo!!

Pole sana mkuu na ninakutakia vita njema! Hatimaye utashinda 🫡
 
Mimi sina cha kukushauri.. kaongee na mama yako km yupo hai ukimaliza ongea na baba yako km yupo hai watakachokushauri kifanyie kazi...

Maana yakikukuta watakaohangaika kukukomboa wa kwanza ni hao na sio wengine, wengine wote watakuacha utaabike mwenyewe
 
Back
Top Bottom