Ushauri wenu, kapata zero nataka nimrudishe form two

Ushauri wenu, kapata zero nataka nimrudishe form two

kumbuka na age ni tatizo, hakimaliza form 4 akiwa na umri mkubwa hata kama amepass haendi form5 ya government
Kwani umri wa kujiunga na 4M5 government ni miaka mingapi mwisho?
 
namba hawez kupata kwa utaratibu wa sasa maana zinatumika TSM9 za shule za shule ya msing lbda atumie jina la mtu aliyeacha shule.
Inamaana hamna wanaorudia 4M2 sasa hivi??
 
Jaman si kila MTU kaumbiwa kusoma jaribu kucheki anapenda kufanya nini mwenyewe pia cheki na vitu ambavyo atafanya apate kazi...
 
Muulize anapenda nini
Mpeleke hata kwingine ataweza kutoka na akuache mataa ukijiona ulikosea kumfikiria arudie kusoma.. mwaka mmoja sawa ila yote hiyo aiseee

Tulia nae nenda mahala mkipata soda akueleze na ninj haswa kinampa ugumu.. labda kama unajua tayarina amekubali.. basi muifanyie kazi.
 
Kwanza kabisa inabidi utumie saikolojia kwanini alipata division zero? Na kwanini asipate four au three au two ama one? Kikubwa nenda shule aliyokuwa anasoma ukaongee na walimu waliokuwa wanamfundisha hapo ndipo utakapopata jibu sahihi ni kwann alipata sifuri mitihan yote? Pia uogee na muhusika akwambie ni kwann alipata zero...hapo inabidi uwe mkali mpaka akupe jibu sahihi!!! Kupata zero ni fedheha sana tena sana.... Haiwezekani miaka minne anakosa hata "D" tu!!! Kama hajitambui ama kichwa kigumu basi ataweza soma hata miaka 10 akawa anishia kupata zero... Ila kama anajitambua basi ni rahisi kuibadilisha zero kuwa four ama three!!!
 
kumbuka na age ni tatizo, hakimaliza form 4 akiwa na umri mkubwa hata kama amepass haendi form5 ya government
Kuanzia umri gani mtu haruhusiwi kwenda F5 ya serikali?
 
Nianzie kujua jinsia ka me au ke maana kama ni me mwambie apambane Sana asiposoma kuna kazi ngumu na akishindwa kazi ngumu basi tena umombasa sasa ambao si mzuri kabisa na kama ke basi kama kitabu akipandi atulie ajipende aje kuwa married bdae tunatafuta wake bado tupo
 
Mwaka Jana nimempeleka mdogo wangu angalau arudie Na apate namba afanye necta kama school candidate walisema haiwekani Kwa utaratibu wa sasa
Anaweza kufanya kama reseter akaanza form two au form three
 
niwe tofaut na wenzangu, mfundishe biashara ndogo ndogo yaan ujasiliamal kwa ujumla, au fan nyingne yoyote ile, kama vile ufund umeme, udereva, mpeleke geregi nahakika baada ya miaka 3 ataleta matokeo mazur na utafrai. akikataa ndo mpeleke form two. gharam za kumtoa form two had form 4, zngetosha kufanya moja kat ya hayo nlyokushaur.
Naunga mkono maoni yako.
 
mpeleke VETA akasome fani yoyote ile aipendayo maana hata waliosoma wengi siku hizi hawana ajira wala vipato vya uhakika
 
Mwaka Jana nimempeleka mdogo wangu angalau arudie Na apate namba afanye necta kama school candidate walisema haiwekani Kwa utaratibu wa sasa
Anaweza kufanya kama reseter akaanza form two au form three
Ulimpeleka private au Government?
 
Back
Top Bottom