Ushauri wenu kabla sijafanya maamuzi magumu

Ushauri wenu kabla sijafanya maamuzi magumu

GalileiGalileo

Senior Member
Joined
Nov 19, 2011
Posts
165
Reaction score
225
Iko hivi:
Nina mpenzi wangu wa siku nyingi kama miaka 7 hivi. Hivi karibuni mapenzi yalianza kupoa na nikiri wazi kuwa mimi ndiye haswa niliyekinai na kumueleza mwenzangu kwa maneno hata kwa kumuonesha kwa vitendo. Hapa na pale nikaopoa Jimama na niseme wazi kuwa kilichonivutia kwake haswa ni huduma anazonipa kwa maana ya huduma zaidi ya mapenzi. Mpenzi wangu wa zamani akagundua hilo lakini hakukata tamaa hivyo tukawa tunaendelea kidogo kidogo na mahusiano yetu ambayo hata huyo Jimama alikuwa anajua kwani alinikuta nikiwa naye na kuahidi kuwa atamuheshimu.

Baada ya kama mwaka mzima kupita tukiendelea na mfumo huu wa maisha, nagundua kuwa huyu Jimama naye ana mzee wake tena wa siku nyingi tu ila anakomaa kuwa huyo anampa kampani ya kiuchumi tu ila Mimi ndio roho yake. Kwa kweli hali hii ilinifanya nipunguze mapenzi kwake kwa kiasi fulani. Yeye ameshindwa kukubaliana nayo na moja ya kitu anachodhani kimesababisha kuyumba kwa penzi letu ni yule mpenzi wangu wa tangu zamani akidhani kuwa mapenzi yetu yameimarika.

Balaa!
Ameamua kumfanyia jambo la ajabu sana mpenzi wangu huyu wa toka enzi kwa kununua wahuni na mmoja wapo kujifanya kuwa anampenda na anataka kumuoa. Huyu muhuni amewezeshwa gari, pesa na kujifanya ni afisa fulani wa Serikali. Huyu mpenzi wangu wa toka enzi kwa kutojua na kwa kuamini kuwa sasa amepata mwanaume atakayempenda kwa dhati akaingia mkenge na siku ya siku walipokuwa wanafanya tendo amejikuta amerekodiwa na video/ picha kusambazwa hadi kunifikia Mimi. Lengo kuu hapa nione kuwa nang'ang'ania mwanamke ambaye ni Malaya kama walivyo Malaya wengine. Hili limenisikitisha sana ukizingatia kuwa kwa sasa huyo binti amepatwa na shock mbaya hadi kulazwa hospitali.

Hapa nilipo nimejawa na huzuni, huruma, hasira na hali ya kuchanganyikiwa kiasi kwamba nafikiria kumfanyia huyu mama jambo baya!

Ushauri wenu tafadhali!
 
Pole sana kiongozi kwanza tuliza akili itulie maaba ni mtihani na ukizingatia kuwa video na picha zipo kwa watu. Kwanza huyo binti ndio kaumia zaidi maana hawa wanawake wakishajua watu wao wanawachit huwa wanakuwa na maamuzi magumu mno katika kulipiza kisasi amini usiamini huy binti anakupenda saba
Ila wewe baharia ni fara sana yaani unadate na jimama mpka mpenzi wako anafahamu unadhani yeye hana moyo? Nyambafu.
Ushauri wangu pliz kuwa karibu sana na huyo binti yaani wewe ndo uwe mfariji wake tafafhali but uache usenge wako sasa na huyo jimama
Ndio maana tunaambiwa vijana tufanye kazi.




Mwenye bajaj used anipm pliz
 
Muoe tu huyo jimama maana uliyataka mwenyewe. Ukimkataa atatuma manjemba yaje yakuambaruty bure! Nenda tu ukatulie na jimama maana hakukuita umtongoze.

Wengine wajifunze kutulia na wenzi wao. Harafu haya masuala ya kukaa uchumba miaka saba ni nini? Baadae mtaanza kuitana kaka na dada kisa uchumba usio na kikomo.
 
nimekuelewa jamaa yaaangu, naona wachangiaji wengine wamekimbili hoja dhaifu ya udangaji.
lakini jamaaa hapa kaeleza wazi, kuwa jimama anahudumia zaidi penzi/sexiana kuliko huyo wake wa zamani

hata mimi niliwahi kunasa sehemu sababu nilikuwa nikipiga simu kuomba nimekumiss naletewa mzigo tofauti na niliyekuwa naye kitambo yeye utetezi mwingi hadi najiuliza anaishije na ukeke bila kuchachua?

wanaume hata mdada awe mzuri vipi sisi shida yetu kubwa tunda, akili haifanyi kazi bila kula tunda.
imagine umempata sasa anakupa utakavyo[emoji8][emoji8][emoji8]
 
Iko hivi:
Nina mpenzi wangu wa siku nyingi kama miaka 7 hivi. Hivi karibuni mapenzi yalianza kupoa na nikiri wazi kuwa mimi ndiye haswa niliyekinai na kumueleza mwenzangu kwa maneno hata kwa kumuonesha kwa vitendo. Hapa na pale nikaopoa Jimama na niseme wazi kuwa kilichonivutia kwake haswa ni huduma anazonipa kwa maana ya huduma zaidi ya mapenzi. Mpenzi wangu wa zamani akagundua hilo lakini hakukata tamaa hivyo tukawa tunaendelea kidogo kidogo na mahusiano yetu ambayo hata huyo Jimama alikuwa anajua kwani alinikuta nikiwa naye na kuahidi kuwa atamuheshimu.

Baada ya kama mwaka mzima kupita tukiendelea na mfumo huu wa maisha, nagundua kuwa huyu Jimama naye ana mzee wake tena wa siku nyingi tu ila anakomaa kuwa huyo anampa kampani ya kiuchumi tu ila Mimi ndio roho yake. Kwa kweli hali hii ilinifanya nipunguze mapenzi kwake kwa kiasi fulani. Yeye ameshindwa kukubaliana nayo na moja ya kitu anachodhani kimesababisha kuyumba kwa penzi letu ni yule mpenzi wangu wa tangu zamani akidhani kuwa mapenzi yetu yameimarika.

Balaa!
Ameamua kumfanyia jambo la ajabu sana mpenzi wangu huyu wa toka enzi kwa kununua wahuni na mmoja wapo kujifanya kuwa anampenda na anataka kumuoa. Huyu muhuni amewezeshwa gari, pesa na kujifanya ni afisa fulani wa Serikali. Huyu mpenzi wangu wa toka enzi kwa kutojua na kwa kuamini kuwa sasa amepata mwanaume atakayempenda kwa dhati akaingia mkenge na siku ya siku walipokuwa wanafanya tendo amejikuta amerekodiwa na video/ picha kusambazwa hadi kunifikia Mimi. Lengo kuu hapa nione kuwa nang'ang'ania mwanamke ambaye ni Malaya kama walivyo Malaya wengine. Hili limenisikitisha sana ukizingatia kuwa kwa sasa huyo binti amepatwa na shock mbaya hadi kulazwa hospitali.

Hapa nilipo nimejawa na huzuni, huruma, hasira na hali ya kuchanganyikiwa kiasi kwamba nafikiria kumfanyia huyu mama jambo baya!

Ushauri wenu tafadhali!

Tafuta hela Kijana, usituandikie imagination ya maisha ambayo hayapo! Tatua matatizo yako kwa kutafuta pesa!
 
Kama li mama limetuma mtu mwenye gari na demu wako kakubari kuliwa hadi video juu nsomba Sky Eclat uniombee kwa huyu mtoa mada na mimi nikamlipizie kisasi kwa hill jimama na ahidi kurudi na video kama ya amber ruty.
Ninamlaumu mpenzi wako hakujua thamani yake mapema. Alivyojua uko na jimama alipaswa akumwage mapema.

Hizi love hexagons ndiyo zinaeneza HIV sasa kama mmoja wenu ni + hapo watu wanne mmeunga chain.
 
Back
Top Bottom