Ushauri wenu jinsi ya kutoka nyumbani na kuanza maisha, Mimi mwenyewe nimeshindwa

musa abel jr

Member
Oct 12, 2016
39
57
Habari nianze kwa kuwapa pole ya majukumu ya kila siku,

Naombeni ushauri ndugu zangu mimi ni kijana nimemaliza chuo 2019 katika kada fulani ya afya na nikabahatika kufaulu na nimesomeshwa na kaka yangu, sasa baada ya kumaliza chuo nikarudi nyumbani na kuanza kutafuta ajira angalau nipate hela ya kununua boxer.

Sasa bwana changamoto ikaja nimeoata ajira ya kwanza kwa mtu binafsi nikaenda mpaka kuonana naye na nikafanya vitu kadhaa sasa kaka yangu aliyenisomesha akasema rudi nyumbani huo mshahara haufai, nikarudi tu nyumbani nikaanza kutafuta nyingne nikapata huko Tarime. Nikatakiwa kwenda lakini sababu zikawa nyingi kutoka kwa huyo kaka angu na mama angu, ikapita hiyo

Sasa wiki hii nimepata ajira nyingne huko Lindi nikatakiwa kwenda lkn kaka yangu akanambia niongee na mama angu, nikaongea naye mama akarudi kuongea na kaka na kuja kunipa jibu kuwa kaka yako kasema huko kuna ugaidi mwingi ni Kusini na pia yeye anataka nifanye kazi katika hospital ili nijenge CV nzuri hata kama kwa kujitolea na mama angu pia anaafiki kwa hilo.

Kumbuka hapa nyumbani mimi ndio kama mfanyakazi wao yaani kuna kuku mimi ndo mlishaji, kuna gari hapa mimi ndio muendeshaji na kutumwa sehemu mbali mbali.

Sasa naomba ushauri juu ya haya...

1. Nifanyeje ili nitoke nyumbani?
2. Je, hawa ambao ni kama wazazi wangu wana nia njema na maisha yangu?
3. Je, nitakaa nyumbani mpaka lini?
4. Na nitapata vipi CV kwa kukaa nyumbani muda mrefu
5. Kwann wananifanyia hivi?

USHAURI WENU NI MUHIMU NDUGU
 
Umemaliza chuo 2019 I assume Umemaliza una miaka 23. Leo 2022 nadhani una miaka 25/26.
Kwa umri huo sidhani kama kuna mtu bado inatakiwa akuambie nini ufanye na kipi usifanye, hata kama bado upo kwake/chini yake.

Ni maisha yako, yako pekee yako one will feel sorry for you mambo yakikuaharibikia. Shetani mjanja sana anaweza kumtumia yoyote tu ilimradi usitimize jambo lako ilimradi tu awe ameona huko unakoelekea kuna potential fulani upande wako.

Ushauri wangu kwako, jitahidi ufanye maamuzi kwa ajili ya maisha yako. Just do it.
Thanks sana mkuu nimekupata vyema
 
Baada ya miaka 10 maisha yatakuwa mikononi mwako na hao ndugu hawatakutambua Cha kufanya fanya unaloona linafaa kwako usiogope kuwa sijui utawavunjia heshima ,maana hayo ni maisha yako na familia yako

Ila usifanye kazi ya 10000 kwa siku tafuta mishe /kazi ya maana
 
Familia mzima mna matatizo...

Ingawaje unadhani ni kaka yako ndie mwenye matatizo, hata wewe una matatizo...

Asiye na utaalamu wa kuisikia sauti ya maandishi anaweza asinielewe lakini mwenye utaalamu wa kusikia sauti za maandishi, atanielewa!

Angalia unavyotaja hayo maeneo...

Nikapata ajira HUKO Tarime,

Nikapata ajira HUKO Lindi...

I'm very certain ingekuwa kwa mfano unaishi Morogoro halafu ajira ukapata Dar, wala usingesema "Huko Dar" bali ungesema tu nikapata ajira Dar!

Na ingawaje unaweza usijue tafsiri ya neno "huko" ambalo umekuwa ukilitumia, tafsiri yako moyoni ni kama ulivyoielezea Lindi kwamba:-
...huko kuna ugaidi mwingi ni kusini
And you've something about Tarime too!!

Kwahiyo, pigika kwanza vya kutosha ndipo utajua which is which kati ya Dar es saalam vs huko Namanyele!!!

Na zikishakutoka hizo akili za "huko" "huko", utakuwa kituo cha basi asubuhi ya siku inayofuata mara baada ya kupata offer "huko" somewhere!!
 
Familia mzima mna matatizo...

Ingawaje unadhani ni kaka yako ndie mwenye matatizo, hata wewe una matatizo...

Asiye na utaalamu wa kuisikia sauti ya maandishi anaweza asinielewe lakini mwenye utaalamu wa kusikia sauti za maandishi, atanielewa!

Angalia unavyotaja hayo maeneo...

Nikapata ajira HUKO Tarime,

Nikapata ajira HUKO

I'm very certain ingekuwa kwa mfano unaishi Morogoro halafu ajira ukapata Dar, wala usingesema "Huko Dar" bali ungesema tu nikapata ajira Dar!

Na ingawaje unaweza usijue tafsiri ya neno "huko" ambalo umekuwa ukilitumia, tafsiri yako moyoni ni kama ulivyoielezea Lindi kwamba:-

And you've something about Tarime too!!

Kwahiyo, pigika kwanza vya kutosha ndipo utajua which is which kati ya Dar es saalam vs huko Namanyele!!! Na zikishakutoka hizo akili za "huko" "huko", utakuwa kituo cha basi asubui ya siku inayofuata mara baada ya kupata offer "huko" somewhere!!
Kuna kitu nimepata mzee "kutumia neno huko ina maana kuwa hio sehemu huipendi maana mwenyewe sijawahi sikia mtu anasema naenda huko dar au nafanya kazi huko dar Ila utasikia nimepata kazi huko songea
 
Kuna kitu nimepata mzee "kutumia neno huko ina maana kuwa hio sehemu huipendi maana mwenyewe sijawahi sikia mtu anasema naenda huko dar au nafanya kazi huko dar Ila utasikia nimepata kazi huko songea
Ahsante sana... umenielewa vema! Mtu akishatanguliza neno "huko" tu, ni kwamba hiyo sehemu amei-downgrade!
 
Chakufanya wewe endelea kuwasikiliza mama na brother.. wallah unatoboa
 
Wewe ni msomi kweli?

Mbona unashindwa kupangilia mwandiko wako vizuri!!!

Je, huyo kaka na mama yko wao wamefanya juhudi gani kukutafutia hata hiyo nafasi ya kujitolea kwenye hospitali?
 
Habari nianze kwa kuwapa pole ya majukumu ya kila siku,

Naombeni ushauri ndugu zangu mimi ni kijana nimemaliza chuo 2019 katika kada fulani ya afya na nikabahatika kufaulu na nimesomeshwa na kaka yangu, sasa baada ya kumaliza chuo nikarudi nyumbani na kuanza kutafuta ajira angalau nipate hela ya kununua boxer.

Sasa bwana changamoto ikaja nimeoata ajira ya kwanza kwa mtu binafsi nikaenda mpaka kuonana naye na nikafanya vitu kadhaa sasa kaka yangu aliyenisomesha akasema rudi nyumbani huo mshahara haufai, nikarudi tu nyumbani nikaanza kutafuta nyingne nikapata huko Tarime. Nikatakiwa kwenda lakini sababu zikawa nyingi kutoka kwa huyo kaka angu na mama angu, ikapita hiyo

Sasa wiki hii nimepata ajira nyingne huko Lindi nikatakiwa kwenda lkn kaka yangu akanambia niongee na mama angu, nikaongea naye mama akarudi kuongea na kaka na kuja kunipa jibu kuwa kaka yako kasema huko kuna ugaidi mwingi ni Kusini na pia yeye anataka nifanye kazi katika hospital ili nijenge CV nzuri hata kama kwa kujitolea na mama angu pia anaafiki kwa hilo.

Kumbuka hapa nyumbani mimi ndio kama mfanyakazi wao yaani kuna kuku mimi ndo mlishaji, kuna gari hapa mimi ndio muendeshaji na kutumwa sehemu mbali mbali.

Sasa naomba ushauri juu ya haya...

1. Nifanyeje ili nitoke nyumbani?
2. Je, hawa ambao ni kama wazazi wangu wana nia njema na maisha yangu?
3. Je, nitakaa nyumbani mpaka lini?
4. Na nitapata vipi CV kwa kukaa nyumbani muda mrefu
5. Kwann wananifanyia hivi?

USHAURI WENU NI MUHIMU NDUGU
Ongea nao,waambie unataka kujaribu bahati yako na kuwa utajitahidi kuwa makini huko kusini.
 
Familia mzima mna matatizo...

Ingawaje unadhani ni kaka yako ndie mwenye matatizo, hata wewe una matatizo...

Asiye na utaalamu wa kuisikia sauti ya maandishi anaweza asinielewe lakini mwenye utaalamu wa kusikia sauti za maandishi, atanielewa!

Angalia unavyotaja hayo maeneo...

Nikapata ajira HUKO Tarime,

Nikapata ajira HUKO Lindi...

I'm very certain ingekuwa kwa mfano unaishi Morogoro halafu ajira ukapata Dar, wala usingesema "Huko Dar" bali ungesema tu nikapata ajira Dar!

Na ingawaje unaweza usijue tafsiri ya neno "huko" ambalo umekuwa ukilitumia, tafsiri yako moyoni ni kama ulivyoielezea Lindi kwamba:-

And you've something about Tarime too!!

Kwahiyo, pigika kwanza vya kutosha ndipo utajua which is which kati ya Dar es saalam vs huko Namanyele!!!

Na zikishakutoka hizo akili za "huko" "huko", utakuwa kituo cha basi asubuhi ya siku inayofuata mara baada ya kupata offer "huko" somewhere!!
Upo sahihi Mkuu,

Jamaa anaonekana hayupo serious kutoka Apo kwao kwenda kureport mikoani.

Kwa lugha aliyotumia it seems ni yeye Binafsi ndo mwenye maamuzi hayo sema anatumia tu gear ya kumlaumu kaka na mama yake.

Mtoa mada take it from me.
Kaka ako alijitolea kukusomesha na huo ndo msaada mkubwa zaidi aliokupatia. Maisha ni yako na maamuzi ni yako pia, unapoamua kutafuta mafanikio kamwe usichukue maamuzi ya kusitasita na Wala usipende vya kusikia.

Ni vyema ukaisikiliza ile sauti ya ndani inayotoa hatima ya mafanikio ya maisha ya mtu.

Hakuna sehemu mbaya, na Wala hakuna sehemu nzuri Tanzania hii isipokuwa ni vile unavyoweza kuishi vizuri na watu wanaokuzunguka.

Popote ueandapo ishi kulingana na wenyeji wanavyoishi hutosikia,Kuna ugaidi,sijui kuchinjana,Wala kulogana.

Nasikitika kusema una bahati na kazi, Ila hauna maamuzi sahihi. Pilau la bure hapo kwenu linakulemaza akili.

Hujachelewa mwaka ndo kwanza umeanza changamka fursa hizo, nenda Lindi kareport.
 
Wana mashaka na umri wako....bado huna akili za kujiongoza na kujisimamia..

Kuwa mvumilivu waonyeshe kuwa umekuwa Sasa..unaweza kujitegemea
 
Wakishua wewe endeleza biashara za nyumbani ungekua upo familia ya kimaskini had sahivi ungekua umeshatolewa nduki ukafanye kaz yeyote
 
Back
Top Bottom