Ushauri Wangu kwa Wakongo (DRC)

Ushauri Wangu kwa Wakongo (DRC)

Binafsi naona Congo DRC itakuwa na amani ya kudumu pale tu Mseveni na Kagame wakiacha kujingiza katika masuala ya kisiasa ndani ya Jamuhuri ya Kongo - hizi kampeini za chini chini za kuchochea vurugu katika jimbo la kaskazini mashariki mwa DRC specifically KIVU yote kuna ajenda ya siri ya muda mrefu yenye lengo la ku-annex jimbo hilo ili lichukuliwe na nchi jirani, hao ndio wana-fund na kuwapa silaha waasi ili waendeleze vurugu katika jimbo hilo - akili zao finyu wanafikiri wanaweza kujenga hoja ya kushinikiza umoja wa Mataifa kwamba Congo DRC ni kubwa mno hivyo ni bora KIVU ijiunge na Rwanda - hiyo ndio plan ya muda mrefu, tutasema mengi lakini ukweli wa mambo mzizi wa fitina unanzia hapo, na hata siju moja Congo DRC haitakuwa na amani ya kudumu kama AU au Umoja wa Mataifa utashindwa kuwa confront M7 na PK head on na kuwambia kwamba wakome kujiingiza kwenye masuala ya kisiasa ndani ya Kongo DRC, wakiwa vig'ang'anizi basi itafutwe njia mbadala ya ku-deal nao once and for all.
tutaongea mengi,ukweli ni kwamba vita ya Congo,niyakufitinishwa na majirani,kibaya zaidi wanaofaulisha hizo fitina ni wacongo wenyewe,namaanisha ndani ya Congo kuna wa Congo wasaliti,wa Congo wanao wauza wa Congo wenzao kwa tamaa zao binafsi na maslahi yao binafsi,lakini swali lakujiuliza ni hili je kwa nn usaliti huu umekuwa sugu ndani ya ardhi ya Congo,jibu ni hili uzalendo wa wacongo ulishazikwa kitambo tangu enzi za mobutu seseseko,hivyo Congo ina generation ambayo neno uzalendo halimo ,yaani kisayansi ile Gene ya uzalendo haimo.ni kweli Congo ina viongozi lakini ni viongozi wa sio na uzalendo na ardhi yao,ni kweli Congo ina Wana nchi wazee kwa vijana lakini ni wananchi wasio na uzalendo na ardhi yao,ni kweli congo ina jeshi lakini ni jeshi lisilo na uzalendo na ardhi yao,ni kweli congo ina polisi lakini ni polisi wasio na uzalendo na nchi yao.hakuna nchi ambayo huwa haifitiniwi lakini tunaona linapokuja kwenye suala la nchi wananchi,viongozi na jeshi huweka tofauti zao pembeni na kuwa na sauti moja,kiongozi akisema adui na apigweee,wananchi na jeshi lote huitikia apigweee tena kwa kumaanisha kutoka moyoni wakiwa na Nia moja na ari moja ,na sio apigweeee ya mdomoni hapana.hata wapalestine tunawaona wanavyopambana kwa pamoja hata Kama bado hawaja fanikiwa lakini dunia nzima inaona wapalestine wanavyo waumiza vichwa waisrael,na hata Kama ukisimama useme wapalestine hawana uzalendo watu watakushangaa Sana,hii ni tofauti kwa ndg zangu wacongo.tatizo la congo limekuwa la muda mrefu Sana,lakini ni wao wacongo wenyewe wamekubali na kuridhika na yote. Ukweli ni kwamba wakongo kwa pamoja wakisema sasa basi inatosha,wanauwezo wa kumpiga adui yao nakumtoa nje ya mipaka,wanauwezo wa kumpiga hata wakaingia ndani ya mipaka ya adui na kumpiga,inawezekana kwa wacongo lakini ikiwa hawata geuka nyuma na kuviwazia vilivyo nyuma yao.kurudisha heshima ya kongo inahitaji sadaka ,sadaka ya kujitoa ,wacongo wa sasa wanahitaji kujitoa sadaka ili kutengeneza congo mpya yenye heshma kwa kizazi na kizazi kijacho.
 
Rais Felix Antoine Tshisekedi Tshilombo wa DRC amepata uenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), wakati nchini kwake bado kunawaka moto na ebola imerudi. Je, atayamudu matatizo ya Afrika nzima ikiwa kwake bado kugumu? Wakongo msaidieni Rais Tshisekedi.

Kila siku Wakongo wanatumia midomo yao kuimba nyimbo za "nakupenda Cherie; na lingi mwasi kitoko na ngai." Huku wakikata mauno wakati nchi imegubikwa na migogoro isiyoisha tangu uhuru 1960!

Wakongo waache kabisa nyimbo hizo, badala yake waanze kutumia "midomo yao" kuimba nyimbo za mapinduzi ya kujenga nchi yao, kufanya maridhiano, kusameheana na kuaminiana kama walivyofanya Wazanzibari (serikali ya mseto) na Wakenya (handshake), japo wao walijadiliana - hawakuimba nyimbo.

Wao watumie "midomo yao" kuimba nyimbo za kumaliza tofauti zao na kuweka misingi ya umoja thabiti.

Wakongo ni ndugu zetu wa karibu, Waafrika wenzetu, majirani zetu na binadamu wenzetu; tuwasaidie kupatana na si kuchapana!
Kinacho waumiza wakongo ni mali yao iliyo ardhini dunia hii yote teknoligia haiwez kwenda bila kongo!!!

Nawasilisha
 
Maoni mazuri
tutaongea mengi,ukweli ni kwamba vita ya Congo,niyakufitinishwa na majirani,kibaya zaidi wanaofaulisha hizo fitina ni wacongo wenyewe,namaanisha ndani ya Congo kuna wa Congo wasaliti,wa Congo wanao wauza wa Congo wenzao kwa tamaa zao binafsi na maslahi yao binafsi,lakini swali lakujiuliza ni hili je kwa nn usaliti huu umekuwa sugu ndani ya ardhi ya Congo,jibu ni hili uzalendo wa wacongo ulishazikwa kitambo tangu enzi za mobutu seseseko,hivyo Congo ina generation ambayo neno uzalendo halimo ,yaani kisayansi ile Gene ya uzalendo haimo.ni kweli Congo ina viongozi lakini ni viongozi wa sio na uzalendo na ardhi yao,ni kweli Congo ina Wana nchi wazee kwa vijana lakini ni wananchi wasio na uzalendo na ardhi yao,ni kweli congo ina jeshi lakini ni jeshi lisilo na uzalendo na ardhi yao,ni kweli congo ina polisi lakini ni polisi wasio na uzalendo na nchi yao.hakuna nchi ambayo huwa haifitiniwi lakini tunaona linapokuja kwenye suala la nchi wananchi,viongozi na jeshi huweka tofauti zao pembeni na kuwa na sauti moja,kiongozi akisema adui na apigweee,wananchi na jeshi lote huitikia apigweee tena kwa kumaanisha kutoka moyoni wakiwa na Nia moja na ari moja ,na sio apigweeee ya mdomoni hapana.hata wapalestine tunawaona wanavyopambana kwa pamoja hata Kama bado hawaja fanikiwa lakini dunia nzima inaona wapalestine wanavyo waumiza vichwa waisrael,na hata Kama ukisimama useme wapalestine hawana uzalendo watu watakushangaa Sana,hii ni tofauti kwa ndg zangu wacongo.tatizo la congo limekuwa la muda mrefu Sana,lakini ni wao wacongo wenyewe wamekubali na kuridhika na yote. Ukweli ni kwamba wakongo kwa pamoja wakisema sasa basi inatosha,wanauwezo wa kumpiga adui yao nakumtoa nje ya mipaka,wanauwezo wa kumpiga hata wakaingia ndani ya mipaka ya adui na kumpiga,inawezekana kwa wacongo lakini ikiwa hawata geuka nyuma na kuviwazia vilivyo nyuma yao.kurudisha heshima ya kongo inahitaji sadaka ,sadaka ya kujitoa ,wacongo wa sasa wanahitaji kujitoa sadaka ili kutengeneza congo mpya yenye heshma kwa kizazi na kizazi kijacho.
 
Mkuu kwanza ungeenda sikiza LOSAMBO ya EXTRA MUSICA kisha ungerekebisha kauri yako
si sahihi kusema wanaimba mapenzi hawaiimbii nchi yao
zipo nyimbo nyingi sana tangu miaka ya kina LUAMBO MIKIADI hadi enzi za kina KABASELE YAMPANYA
Nimekutajia LOSAMBO sababu ni maarufu
Ila wewe uliipenda sebene na midundo ya musica yake ukasahau ujumbe mzito uliopo humo ndani ya mashahiri ya hiyo nyimbo
ambapo humo utazisikia sauti zenye huzuni Mwingi na zenye UCHUNGU mkubwa na nchi yao za kina IBAMBI OKOMBI ROGATIEN na kundi nzima la EXTRA MUSICA wakiimbia nchi yao jinsi maswaibu inayoyapata kiasi wanamuomba MUNGU mpk wanamtaja kwa jina la ALLAH
awaunganishe wacongo
awape NGUVU wapambane kuikomboa nchi yao
Hiyo ni moja kati ya nyimbo nyingi tu mkuu hvyo swala la kuimba washaimba sanaaa

Hvyo nyimbo pekee hazitoshi
CONGO inahitajika apatikane KIONGOZI mzarendo asiyesimikwa na mabeberu mwenye uchungu na nchi yake wanacongo wenzake
Akawaunganisha wakawa wamoja wakaijenga nchi yao

Asikwambie mtu
WACONGO wanapata TABU
Wanateseka mno ndani ya nchi yao
Tangu enzi za KING LEOPORD mpk kesho wacongo wanaishi kwa mateso mno katika ARDHI yao ambayo imebarikiwa kila aina ya neema si madini mito misitu na ARDHI yenye rutuba na eneo pana

TATA NZAMBE YOKA LOSAMBO YA BANA YA LE CONGO
PESA NGUYA PAPA
PO TULUKA LA VIE

Extra wapo Congo nyingine
 
Mkuu Sio Kongo tu niseme Afrika kwa ujumla tulishakubali kuwa meza ya kuchezewa chess na first world hakuna namna ya kushauri kitu ilishakuwa more than too late yani mtu anakuwa mkubwa AU wakati nchini kwake ni afadhali ya shida.Inachekesha
 
Mkuu kwanza ungeenda sikiza LOSAMBO ya EXTRA MUSICA kisha ungerekebisha kauri yako
si sahihi kusema wanaimba mapenzi hawaiimbii nchi yao
zipo nyimbo nyingi sana tangu miaka ya kina LUAMBO MIKIADI hadi enzi za kina KABASELE YAMPANYA
Nimekutajia LOSAMBO sababu ni maarufu
Ila wewe uliipenda sebene na midundo ya musica yake ukasahau ujumbe mzito uliopo humo ndani ya mashahiri ya hiyo nyimbo
ambapo humo utazisikia sauti zenye huzuni Mwingi na zenye UCHUNGU mkubwa na nchi yao za kina IBAMBI OKOMBI ROGATIEN na kundi nzima la EXTRA MUSICA wakiimbia nchi yao jinsi maswaibu inayoyapata kiasi wanamuomba MUNGU mpk wanamtaja kwa jina la ALLAH
awaunganishe wacongo
awape NGUVU wapambane kuikomboa nchi yao
Hiyo ni moja kati ya nyimbo nyingi tu mkuu hvyo swala la kuimba washaimba sanaaa

Hvyo nyimbo pekee hazitoshi
CONGO inahitajika apatikane KIONGOZI mzarendo asiyesimikwa na mabeberu mwenye uchungu na nchi yake wanacongo wenzake
Akawaunganisha wakawa wamoja wakaijenga nchi yao

Asikwambie mtu
WACONGO wanapata TABU
Wanateseka mno ndani ya nchi yao
Tangu enzi za KING LEOPORD mpk kesho wacongo wanaishi kwa mateso mno katika ARDHI yao ambayo imebarikiwa kila aina ya neema si madini mito misitu na ARDHI yenye rutuba na eneo pana

TATA NZAMBE YOKA LOSAMBO YA BANA YA LE CONGO
PESA NGUYA PAPA
PO TULUKA LA VIE
Exta nusica hawatoki DRC bali congo brazaville
 
Tusikimbilie kulaumu mataifa ya nje,hata mataifa yaliyoizunguka baadhi yameifanya Congo kuwa hapa ilipo,wamejawa uroho tamaa iliyopitiliza,hata sisi ni wabaya sana Tena Sana,Kuna baadhi ya nchi zinaendesha hata nchi zao kwa uwepo wa Congo,tunabaki kulaumu mataifa ya nje yanafaidika yanagombanisha na maneno chungu nzima.
 
Back
Top Bottom