Ushauri Wangu kwa Wakongo (DRC)

Ushauri Wangu kwa Wakongo (DRC)

Gwappo Mwakatobe

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2019
Posts
1,796
Reaction score
2,335
Rais Felix Antoine Tshisekedi Tshilombo wa DRC amepata uenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), wakati nchini kwake bado kunawaka moto na ebola imerudi. Je, atayamudu matatizo ya Afrika nzima ikiwa kwake bado kugumu? Wakongo msaidieni Rais Tshisekedi.

Kila siku Wakongo wanatumia midomo yao kuimba nyimbo za "nakupenda Cherie; na lingi mwasi kitoko na ngai." Huku wakikata mauno wakati nchi imegubikwa na migogoro isiyoisha tangu uhuru 1960!

Wakongo waache kabisa nyimbo hizo, badala yake waanze kutumia "midomo yao" kuimba nyimbo za mapinduzi ya kujenga nchi yao, kufanya maridhiano, kusameheana na kuaminiana kama walivyofanya Wazanzibari (serikali ya mseto) na Wakenya (handshake), japo wao walijadiliana - hawakuimba nyimbo.

Wao watumie "midomo yao" kuimba nyimbo za kumaliza tofauti zao na kuweka misingi ya umoja thabiti.

Wakongo ni ndugu zetu wa karibu, Waafrika wenzetu, majirani zetu na binadamu wenzetu; tuwasaidie kupatana na si kuchapana!
 
Shukrani sana! Jumamosi kesho kutwa, saa 7 mchana baada ya habari za kimataifa, utanisikia na wenzangu wa Kampala na Kinshasa tukichambua uenyekiti wa Tshisekedi kupitia DW.

DW wanajiunga na FM Radios nyingi hapa nchini. Afrika tuna safari ndefu na ngumu endapo sisi Waafrika wote na AU hatutajipanga upya.
Nimekuelewa Sana ndugu. Huwa nakusikia ktk kipindi cha maoni cha radio DW.
 
Nadhani tungetumia vizuri fursa ya ujirani na uwepo wa maliasili zao kwa maendeleo ya nchi yetu. Hao Wakongo waendelee tu kutuburudisha na Ma soukouss yao.

Haiwezekani Mabeberu wa Kichina, Kimarekani, Kibeligiji, Kifaransa, Rwanda na Uganda wanafaidi, halafu eti sisi tunashangaa tu.
 
Ile nchi, fujo zote zilizopo hapo, ni makundi mbalimbali ya wakongo wenyewe ambapo hupenyezewa lupia kutoka nchi za ng'ambo ili tu nchi hizo ziendelee Kuiba utajiri wa wacongomani!

Ili kudhibiti, kunahitajika kuwepo jeshi la kizalendo la Wa Congo wenyewe, na linalojua kunusa ili kuwanyang'anya siraha hao waasi ambao wamejikita hata ndani ya jeshi
 
Ni kweli kabisa, Wakongo wakomboe na kudhibiti rasilimali zao ili wazifaidi ndipo waendelee kutuburudisha
Nadhani tungetumia vizuri fursa ya ujirani na uwepo wa maliasili zao kwa maendeleo ya nchi yetu. Hao Wakongo waendelee tu kutuburudisha na Ma soukouss yao.

Haiwezekani Mabeberu wa Kichina, Kimarekani, Kibeligiji, Kifaransa, Rwanda na Uganda wanafaidi, halafu eti sisi tunashangaa tu.
 
Umenena kwa usahihi kabisa. Inauma na kusikitisha sana!
Ile nchi, fujo zote zilizopo hapo, ni makundi mbalimbali ya wakongo wenyewe ambapo hupenyezewa lupia kutoka nchi za ng'ambo ili tu nchi hizo ziendelee Kuiba utajiri wa wacongomani!

Ili kudhibiti, kunahitajika kuwepo jeshi la kizalendo la Wa Congo wenyewe, na linalojua kunusa ili kuwanyang'anya siraha hao waasi ambao wamejikita hata ndani ya jeshi
 
Shukrani sana! Jumamosi kesho kutwa, saa 7 mchana baada ya habari za kimataifa, utanisikia na wenzangu wa Kampala na Kinshasa tukichambua uenyekiti wa Tshisekedi kupitia DW.

DW wanajiunga na FM Radios nyingi hapa nchini. Afrika tuna safari ndefu na ngumu endapo sisi Waafrika wote na AU hatutajipanga upya.
Nitakifuatilia.
 
Rais Felix Antoine Tshisekedi Tshilombo wa DRC amepata uenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), wakati nchini kwake bado kunawaka moto na ebola imerudi. Je, atayamudu matatizo ya Afrika nzima ikiwa kwake bado kugumu!? Wakongo msaidieni Rais Tshisekedi...
Inaonekana wewe kwenye mambo ya siasa hasa za DRC, ni mweupe kabisa!!mzozo wa congo asilimia kubwa si wao kwa wao ndani ya nchi, mfano, congo mashariki ndiko kwenye shida hasa kivu ya kasikazini, Goma, beni ambako ni mpakani mwa uganda, Rwanda, na maeneo kidogo ya huku kivu ya kusini, maeneo ya FIZI, ITOMBWE, na BARAKA, lakini ukiwa ktk jiji la UVIRA hayo mapigano unayasikia kama unavyoyasikia ukiwa TZ, shida kubwa ni RWANDA, kupitia wanyamulenge, hasa huku kivu kusini, pamoja na kasikazini.

wakongo wenyewe wala wao kwa wao hawana shida kabisa, na hili linatokana kwanza na kuwa na jeshi dhaifu, halafu ndani ya hilo jeshi kuna mapandikizi toka nje.ila kwa hatua aliyoanza nayo tshekedi kama ataifaulu ya kuwa mbali na kabila(japo inaonekana)ataweza basi DRC, Itaanza kupata mwanga.

yaani waasi wanazungukwa na jeshi la congo mala mnasikia amri toka kwa wakuu wenu mnaamuliwa kuondoka eneo hilo haraka!!!na kuna mpango wa jeshi la USA kwenda DRC, utaona kama KAGAME, au mseveni ataendelea kuleta choko choko pale, hao wasanii wala hawana uwezo huo unaousema.
 
Mkuu kwanza ungeenda sikiza LOSAMBO ya EXTRA MUSICA kisha ungerekebisha kauri yako
si sahihi kusema wanaimba mapenzi hawaiimbii nchi yao
zipo nyimbo nyingi sana tangu miaka ya kina LUAMBO MIKIADI hadi enzi za kina KABASELE YAMPANYA
Nimekutajia LOSAMBO sababu ni maarufu
Ila wewe uliipenda sebene na midundo ya musica yake ukasahau ujumbe mzito uliopo humo ndani ya mashahiri ya hiyo nyimbo
ambapo humo utazisikia sauti zenye huzuni Mwingi na zenye UCHUNGU mkubwa na nchi yao za kina IBAMBI OKOMBI ROGATIEN na kundi nzima la EXTRA MUSICA wakiimbia nchi yao jinsi maswaibu inayoyapata kiasi wanamuomba MUNGU mpk wanamtaja kwa jina la ALLAH
awaunganishe wacongo
awape NGUVU wapambane kuikomboa nchi yao
Hiyo ni moja kati ya nyimbo nyingi tu mkuu hvyo swala la kuimba washaimba sanaaa

Hvyo nyimbo pekee hazitoshi
CONGO inahitajika apatikane KIONGOZI mzarendo asiyesimikwa na mabeberu mwenye uchungu na nchi yake wanacongo wenzake
Akawaunganisha wakawa wamoja wakaijenga nchi yao

Asikwambie mtu
WACONGO wanapata TABU
Wanateseka mno ndani ya nchi yao
Tangu enzi za KING LEOPORD mpk kesho wacongo wanaishi kwa mateso mno katika ARDHI yao ambayo imebarikiwa kila aina ya neema si madini mito misitu na ARDHI yenye rutuba na eneo pana

TATA NZAMBE YOKA LOSAMBO YA BANA YA LE CONGO
PESA NGUYA PAPA
PO TULUKA LA VIE
 
Ningekuwa mweupe nisingeshiriki na kuaminiwa katika mijadala mingi ya kimataifa, hasa vyombo vya habari vya kimataifa. Wewe ndiye mweupe unayedhani sehemu moja ya nchi ikiwa na mgogoro basi huo si wa nchi nzima. Unakosea sana!

Mimi naamini Congo ikiwa na tatizo au nchi nyingine ya Afrika, basi hilo ni tatizo la Afrika nzima. Walioko Mtwara wakipata matatizo, yanakuwa matatizo ya Tanzania nzima. Huo ndio utu na Uafrika wetu halisi.

Shida ya watu wa Mashariki ya DRC ni shida ya Congo nzima na Afrika yote. Nkrumah na Nyerere waliamini uhuru wa sehemu moja tu ya Afrika, si uhuru hadi Afrika nzima iwe huru. Hawakuwa weupe!

Pole kwa ufahamu wako mdogo, lakini naamini utaelewa na kupanua ufahamu wako!
Inaonekana wewe kwenye mambo ya siasa hasa za DRC, ni mweupe kabisa!!mzozo wa congo asilimia kubwa si wao kwa wao ndani ya nchi, mfano, congo mashariki ndiko kwenye shida hasa kivu ya kasikazini...
 
Maelezo yako safi sana, ingawa si kwa wanamuziki wote wa Congo
Mkuu kwanza ungeenda sikiza LOSAMBO ya EXTRA MUSICA kisha ungerekebisha kauri yako
si sahihi kusema wanaimba mapenzi hawaiimbii nchi yao
zipo nyimbo nyingi sana tangu miaka ya kina LUAMBO MIKIADI hadi enzi za kina KABASELE YAMPANYA
Nimekutajia LOSAMBO sababu ni maarufu
Ila wewe uliipenda sebene na midundo ya musica yake ukasahau ujumbe mzito uliopo humo ndani ya mashahiri ya hiyo nyimbo
ambapo humo utazisikia sauti zenye huzuni Mwingi na zenye UCHUNGU mkubwa na nchi yao za kina IBAMBI OKOMBI ROGATIEN na kundi nzima la EXTRA MUSICA wakiimbia nchi yao jinsi maswaibu inayoyapata kiasi wanamuomba MUNGU mpk wanamtaja kwa jina la ALLAH
awaunganishe wacongo
awape NGUVU wapambane kuikomboa nchi yao
Hiyo ni moja kati ya nyimbo nyingi tu mkuu hvyo swala la kuimba washaimba sanaaa

Hvyo nyimbo pekee hazitoshi
CONGO inahitajika apatikane KIONGOZI mzarendo asiyesimikwa na mabeberu mwenye uchungu na nchi yake wanacongo wenzake
Akawaunganisha wakawa wamoja wakaijenga nchi yao

Asikwambie mtu
WACONGO wanapata TABU
Wanateseka mno ndani ya nchi yao
Tangu enzi za KING LEOPORD mpk kesho wacongo wanaishi kwa mateso mno katika ARDHI yao ambayo imebarikiwa kila aina ya neema si madini mito misitu na ARDHI yenye rutuba na eneo pana

TATA NZAMBE YOKA LOSAMBO YA BANA YA LE CONGO
PESA NGUYA PAPA
PO TULUKA LA VIE
 
Rais Felix Antoine Tshisekedi Tshilombo wa DRC amepata uenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), wakati nchini kwake bado kunawaka moto na ebola imerudi. Je, atayamudu matatizo ya Afrika nzima ikiwa kwake bado kugumu!? Wakongo msaidieni Rais Tshisekedi...
Kuna Watu Vichwani mwenu mmejaza Usaha tu. Hivi Nchi kuwa na Machafuko ndiyo Kigezo cha Kutengwa?

Israel inasifika kwa Mapigano huko Mashariki ya Kati ila mbona bado huwa inapewa Uenyekiti wa mambo kadhaa ya Kimaendeleo na Kijeshi?

Yaani mpaka leo hujui kuwa Utamaduni wa Wakongo ni Muziki na Wakongo wengi umewatoa zaidi Kimaisha pengine hata kuliko Mimi na Wewe?

Na kwa Kukusaidia tu tokea enzi za Marehemu Luanzo Makiadi ( Franco ) a.k.a Le Grand Mitre hadi hawa wa sasa wamekuwa wakiutumia huo Muziki katika Kuleta Amani na Umoja huko Congo DR na kwa kiasi fulani umesaidia.

Changamoto ya Amani isiyopatikana Congo DR hailetwi na Wakongo bali ni Mataifa makubwa ya Magharibi ( Ulaya na Marekani ) ambao Wanapiganisha Vita huko ili wao waendelee Kubeba Rasilimali Dhababu, Almasi na Uranium.

Na usisahau kuwa Wahenga waliposema kuwa Mchawi mkabidhi ( mpe ) Mwanao hawakukosea kwani Kitendo cha Rais wa Congo DR kupewa huo Uenyekiti unaweza ukawa ni mwanzo mzuri wa kupatikana kwa Suluhu ya Kudumu ya Machafuko yaliyozoeleka huko.
 
Back
Top Bottom