Ushauri wangu kwa CHADEMA, CUF, NLD NCCR-Mageuzi (UKAWA)

Ushauri wangu kwa CHADEMA, CUF, NLD NCCR-Mageuzi (UKAWA)

DALA

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2009
Posts
2,259
Reaction score
4,691
Heshima mbele wanajukwaa!

Sina sababu ya kutoa usuli mreefu kwenye hili maana kila mwenye macho anashuhudia kinachoendelea kwenye ulingo wa siasa. Natakiwa ku decleare interest though. Mimi ninaungamkono mabadiliko hivyo andiko langu linaegemea upande huo.

Tumeshuhudia matokeo ya tafiti za kura za maoni zikitolewa huku zikiashiria CCM kuongoza katika kinyang'anyiro hiki cha uraisi. Ukweli ni kwamba unaweza ukawa ni sahihi au usiwe sahihi inategemea nani amefanya utafiti na anamrengo gani hivyo ni swala la kujadiliwa kwa hoja.

Upande wa pili wa hili ni kuhoji utayari wa upinzani hususani UKAWA kujiwekea mikakati ya ku counter attack objectively na practically predictions. Ninavyoelewa ni kwamba umma unaandaliwa kisaikolojia ukiunganisha matukio mfano yule mzee aliyesema hawakotayari kuachia ikulu na haya matokeo. Mazingira yanaandaliwa ili bao la mkono litakapodumbukizwa watu warejelee matokeo haya ya tafiti hizi.

Ili kuwa realistic, nashauri UKAWA wasiangaike na kura za maoni ila waendeleze kampeni ya kiwango ambacho hakijawahi kutokea hapa nchini hilo la kwanza. La pili, nashauri UKAwA waandae timu ya mawakala/Walinzi wa kura kila kituo, Kata na Wilaya maana hapo ndo pana goli kwa wakati huu. Hawa mawakala wasiwe tu mawakala ikiwezekana watumie wanafunzi wa vyuo vikuu na wenye kujielewa, watu wenye hasira na umasikini, wenye uchu wa maendeleo ambao hawatanunuliwa vituoni.

Kusiwepo na wakala mmoja eti ndo analinda kura za UKAWA kila kituo kisa vyma vingine havijasimamisha mgombea kwa kuzingatia umoja wao.

Kwa njia hii tutashuhudia mtokeo ya utafiti halisi yakitolewa baada ya 25/10/2015 kwa upole ambao haujawahi kutokea.

Haya ni maoni yangu na siyo sheria.
Aluta continua
 
Tunatumai/tunayaona mazigazi tukiyakuta hatukuti maji
 
Kumbe mbinu chafu zinaandaliwa na magamba kuwahonga mawakala wa vyama ili waweze kupiga bao la mkono. Kwa hiyo UKAWA mnatakiwa kuwateua watu wasio na uroho wa pesa kuwa wakala. La sivyo watahongwa na kuruhusu goli la mkono
 
Wanawandaa watu kisaikolojia ili wakubali kushindwa au wanataka ku create kitu kinaitwa apathy - yaani watu wasiende kupiga kura.

Pollster jana alionekana akiwa na Mwigulu na Kigwangala kabla hajaingia chumba cha kutolea matokeo. Definitely matokeo yao ni questionable and lacks credibility.
 
Hujamalizia kwamba hayo matokeo yenu baada ya uchaguzi muyachukue na muyakubali mambo ya nchi kutokutawalika hayana nafasi wakati huu. Dr. Slaa kaleta usumbufu mkubwa na katia damage baada ya uchaguzi 2010 this time mjiandae kuchukua matokeo yenu hakutakuwa na nafasi ya kuwabembeleza wala mambo ya serikali ya kitaifa, Hapa kazi tu.

Mambo ya waziri Babu Duni aliyofanya katika baraza kugoma angali yeye ni waziri hatutaki yatokee tena.

Heshima mbele wanajukwaa!

Sina sababu ya kutoa usuli mreefu kwenye hili maana kila mwenye macho anashuhudia kinachoendelea kwenye ulingo wa siasa. Natakiwa ku decleare interest though. Mimi ninaungamkono mabadiliko hivyo andiko langu linaegemea upande huo.

Tumeshuhudia matokeo ya tafiti za kura za maoni zikitolewa huku zikiashiria CCM kuongoza katika kinyang'anyiro hiki cha uraisi. Ukweli ni kwamba unaweza ukawa ni sahihi au usiwe sahihi inategemea nani amefanya utafiti na anamrengo gani hivyo ni swala la kujadiliwa kwa hoja.

Upande wa pili wa hili ni kuhoji utayari wa upinzani hususani UKAWA kujiwekea mikakati ya ku counter attack objectively na practically predictions. Ninavyoelewa ni kwamba umma unaandaliwa kisaikolojia ukiunganisha matukio mfano yule mzee aliyesema hawakotayari kuachia ikulu na haya matokeo. Mazingira yanaandaliwa ili bao la mkono litakapodumbukizwa watu warejelee matokeo haya ya tafiti hizi.

Ili kuwa realistic, nashauri UKAWA wasiangaike na kura za maoni ila waendeleze kampeni ya kiwango ambacho hakijawahi kutokea hapa nchini hilo la kwanza. La pili, nashauri UKAwA waandae timu ya mawakala/Walinzi wa kura kila kituo, Kata na Wilaya maana hapo ndo pana goli kwa wakati huu. Hawa mawakala wasiwe tu mawakala ikiwezekana watumie wanafunzi wa vyuo vikuu na wenye kujielewa, watu wenye hasira na umasikini, wenye uchu wa maendeleo ambao hawatanunuliwa vituoni.

Kusiwepo na wakala mmoja eti ndo analinda kura za UKAWA kila kituo kisa vyma vingine havijasimamisha mgombea kwa kuzingatia umoja wao.

Kwa njia hii tutashuhudia mtokeo ya utafiti halisi yakitolewa baada ya 25/10/2015 kwa upole ambao haujawahi kutokea.

Haya ni maoni yangu na siyo sheria.
Aluta continua
 
Ndio habari ambazo nyumbu wa ukawa wanapenda kuziskia hzi.
 
Pia moja ya mkakati viongozi wangu wa juu tumieni redio za mikoani kulitangaza jina la LOWASSA na kuchapisha mabango mengi yasukumwe kwenda vijijini na hata mjini hayatoshi ukilinganisha na ya wapinzani wetu CCM.
 
Hujamalizia kwamba hayo matokeo yenu baada ya uchaguzi muyachukue na muyakubali mambo ya nchi kutokutawalika hayana nafasi wakati huu. Dr. Slaa kaleta usumbufu mkubwa na katia damage baada ya uchaguzi 2010 this time mjiandae kuchukua matokeo yenu hakutakuwa na nafasi ya kuwabembeleza wala mambo ya serikali ya kitaifa, Hapa kazi tu.

Mambo ya waziri Babu Duni aliyofanya katika baraza kugoma angali yeye ni waziri hatutaki yatokee tena.


Unachochoandika hapa kwa kulia lia ni nini kama mtashinda halali na kwa gap la 65% hao UKAWA nguvu ya kupinga wataitoa wapi? Maana yake CCM si ndio watakuwa wengi. Hivi watu wachache wanaweza kuwazidi wengi? Hii ni dalili tosha kwamba mnakwenda kuanguka Uchaguzi huu na mnajitahidi kuwaaminisha uma kwamba mtashinda.

CUF kuwa kwenye serikali ya Umoja wa Kitaifa ndio mmeifanya tiketi ya kuendelea kuwadhulumu na kuwakandamiza wananchi, mkifikiri CUF watabweteka kwa mishahara, malupulpu na vyeo. CUF wataendelea kusimamia misingi ya uwajibikaji, haki, uzalendo, uadilifu, uwazi na utawala bora. Tukutane Octoba 25
 
Ushauri ni mzuri tatizo ni kununuliwatu, Rais ni magufuli
 
Back
Top Bottom