Ushauri wangu kwa yanayoendelea Nchini Tanzania

Ushauri wangu kwa yanayoendelea Nchini Tanzania

The Dojin

Member
Joined
Jun 29, 2026
Posts
52
Reaction score
90
Amani iwe nanyi wakuu:

Kama Mtanzania na mwanachama wa CCM, naomba kushauri kwa yanayoendelea nchini kwetu hasa suala la utekaji, ufisadi, na ukandamizaji wa haki za binadamu,

Ushauri kwa Vyombo vya ulinzi na usalama:

Ninyi mmeapa kuilinda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dhidi ya maadui wa nje na ndani wa JMT ikiwemo na kuishauri serikali dhidi ya mambo mbalimbali ya kiusalama, swali la kujiuliza mikataba mibovu wanayoingia viongozi, rushwa na tuhuma zingine zingi ikiwemo na utekaji na mauaji yanaendelea sio tishio la amani na usalama wa taifa letu?.

Ikumbukwe kwamba ustawi wa jamii ndio msingi wa taifa lolote jamii yenye maalamiko na migogoro jamii hiyo haina ustawi na usalama, kila lenye mwanzo halikosi mwisho leo hii wewe kama mtu uliyeapa kuilinda jamhuri kuna siku utastaafu na kuwaachia wengine swali la wewe kujiuliza unatenda haki kwenye jamii? Na je siku ukitoka madarakani utapenda utendewe haya mnayoyatenda sasa hivi mfano mzuri: Suala la Humphrey Polepole wakati ameshika madaraka alijitahidi sana kutetea, kama angejua baadhi ya sheria na ukandamizaji aliokuwa anautetea ungemtokea puani angeshauri serikali ya wakati ule vizuri, ishini vizuri na wananchi. Haipo sababu ya kulinda masilahi ya mtu badala ya Taifa kwa sasa ninyi mmegeuka kuwa wapambe wa viongozi mafisadi. Kumbukeni serikali inakuja na kuondoka ninyi mtakuwepo fanyeni yale yaliyochini ya viapo vyenu.

Kumbukeni hawa wananchi mnaowaona si lolote kuna siku wataunda jeshi lao watakaloliamini lendeni masilahi ya wananchi na sio viongozi wasio waadilifu.

Kwasasa mtumbwi unaenda mlama kama Taifa lazima atafutwe yona aliweze kutoswa baharini


Ushauri kwa viongozi wa serikali:

Mawazo mbadala hayapigwi rungu na siku zote huwezi kushindana na wakati hakuna aliyewahi kushindana na wakati akafaulu, wasikilizeni wananchi wanataka nini kaeni nchi jitafakalini na kama CCM tujitafakali kwa yanayoendelea kama ni suala la katiba wapeni wananchi katiba, tume huru tendeni haki fanyani kazi kwa masilahi ya wananchi sio ya kwenu. Tukubali tukatae nchi yetu sio ile tuliyoizoea kabla ya oct 2025.

Propaganda na kutumia machawa haitasaidia kamwe, tambue kwa sasa nchi yetu inawananchi wanaojielewa sana propaganda kama za Mwigulu, Kenani, Ali hapi, na viongozi wengine haitabadili chochote. Wananchi pamoja na wanaCCM hatufurahi yanayoendelea na namna viongozi mnayoyafanya. Kuteka na kuua watu wenye mawazo mbadala na ya kwetu haitasaidia.

Mwisho

Tanzania ni ya kwetu sote awe mpinzani, asiye na dini mwenye dini,mchungaji na shekhe wote ni Watanzania haina sababu ya kutekana na kuuana kwa sababu tu mtu kaongea ukweli au katoa maoni tofauti na kile unachotaka kusikia.

Kama serikali kwa nguvu inayotumia kuzuia maandamano, kutafuta wanaoikosoa na kuwachukulia hatua, nguvu hii ingeelekezwa kwenye kutatua migogoro ya wananchi na shida za wananchi taifa lingekuwa mbali badala yake tumeharibu reputation yetu kidunia kwa sababu ya kulinda masilahi ya watu wachache wenye uchu wa madaraka.

"Nitasema ukweli daima, uongo kwangu ni mwiko"
 
Public sympathy nimefanya nini? kiki kwa ajili ya nini? nenda facebook huku hakukufai kijana
naona porojo tu, unafiki na drama nonsense ndizo zimejaa kwenye bandiko lako,

narudia tena,
unatafuta kiki au public sympathy? gentleman, ili uelekezwa namna ya kuzipata kirahisi zaidi 🐒
 
Sawa mtekaji
Yes,
why are you hiding kindezi hivyo sasa jukwaani?

you better expose yourself kijasiri na sio kuleta unafiki useless hivyo jukwaani wakati unajijua kabisa wewe ni nani, thus very nonsense and stupid,

usiridie tena unafiki kama huo jukwaani gentleman, okay?🐒
 
Shida yako ndo hiyo tu
I think it's better someone to present the motion on the table without seeking utakatifu from a political party which they are not belong to. nadhani itapendeza zaidi.

Na bado kidogo tu aanze kuporomosha matusi, saivi yupo anafanya mazoezi ya kupandisha mori na mihemko🐒
 
I think it's better someone to present the motion on the without seeking utakatifu from a political party which they are not belong to, nadhani itapendeza.

Na bado kidogo tu aanze kuporomosha matusi, saivi yupo anafanya mazoezi ya kupandisha mori na mihemko🐒
Vingereza vingi mpaka unamaliza miti
 
Amani iwe nanyi wakuu:

Kama Mtanzania na mwanachama wa CCM, naomba kushauri kwa yanayoendelea nchini kwetu hasa suala la utekaji, ufisadi, na ukandamizaji wa haki za binadamu,

Ushauri kwa Vyombo vya ulinzi na usalama:

Ninyi mmeapa kuilinda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dhidi ya maadui wa nje na ndani wa JMT ikiwemo na kuishauri serikali dhidi ya mambo mbalimbali ya kiusalama, swali la kujiuliza mikataba mibovu wanayoingia viongozi, rushwa na tuhuma zingine zingi ikiwemo na utekaji na mauaji yanaendelea sio tishio la amani na usalama wa taifa letu?.

Ikumbukwe kwamba ustawi wa jamii ndio msingi wa taifa lolote jamii yenye maalamiko na migogoro jamii hiyo haina ustawi na usalama, kila lenye mwanzo halikosi mwisho leo hii wewe kama mtu uliyeapa kuilinda jamhuri kuna siku utastaafu na kuwaachia wengine swali la wewe kujiuliza unatenda haki kwenye jamii? Na je siku ukitoka madarakani utapenda utendewe haya mnayoyatenda sasa hivi mfano mzuri: Suala la Humphrey Polepole wakati ameshika madaraka alijitahidi sana kutetea, kama angejua baadhi ya sheria na ukandamizaji aliokuwa anautetea ungemtokea puani angeshauri serikali ya wakati ule vizuri, ishini vizuri na wananchi. Haipo sababu ya kulinda masilahi ya mtu badala ya Taifa kwa sasa ninyi mmegeuka kuwa wapambe wa viongozi mafisadi. Kumbukeni serikali inakuja na kuondoka ninyi mtakuwepo fanyeni yale yaliyochini ya viapo vyenu.

Kumbukeni hawa wananchi mnaowaona si lolote kuna siku wataunda jeshi lao watakaloliamini lendeni masilahi ya wananchi na sio viongozi wasio waadilifu.

Kwasasa mtumbwi unaenda mlama kama Taifa lazima atafutwe yona aliweze kutoswa baharini


Ushauri kwa viongozi wa serikali:

Mawazo mbadala hayapigwi rungu na siku zote huwezi kushindana na wakati hakuna aliyewahi kushindana na wakati akafaulu, wasikilizeni wananchi wanataka nini kaeni nchi jitafakalini na kama CCM tujitafakali kwa yanayoendelea kama ni suala la katiba wapeni wananchi katiba, tume huru tendeni haki fanyani kazi kwa masilahi ya wananchi sio ya kwenu. Tukubali tukatae nchi yetu sio ile tuliyoizoea kabla ya oct 2025. Propaganda na kutumia machawa haitasaidia kamwe, tambue kwa sasa nchi yetu inawananchi wanaojielewa sana propaganda kama za Mwigulu, Kenani, Ali hapi, na viongozi wengine haitabadili chochote. Wananchi pamoja na wanaCCM hatufurahi yanayoendelea na namna viongozi mnayoyafanya. Kuteka na kuua watu wenye mawazo mbadala na ya kwetu haitasaidia.

Mwisho

Tanzania ni ya kwetu sote awe mpinzani, asiye na dini mwenye dini,mchungaji na shekhe wote ni Watanzania haina sababu ya kutekana na kuuana kwa sababu tu mtu kaongea ukweli au katoa maoni tofauti na kile unachotaka kusikia
Kama serikali kwa nguvu inayotumia kuzuia maandamano, kutafuta wanaoikosoa na kuwachukulia hatua, nguvu hii ingeelekezwa kwenye kutatua migogoro ya wananchi na shida za wananchi taifa lingekuwa mbali badala yake tumeharibu reputation yetu kidunia kwa sababu ya kulinda masilahi ya watu wachache wenye uchu wa madaraka.
"Nitasema ukweli daima, uongo kwangu ni mwiko"
Mimi Kila siku nawaambia akina Tlaah Tlaah na wanaccm wengine, waache kuwafuatilia Chadema wanazidi kukipa umaarufu Kwa sababu watz wa sasa sio wajinga kama wale wa 1960s ni Bora washughulike na matatizo ya wananchi.
 
Kama kweli wewe ni mwanaccm kindakindaki basi kumeshaanza kupambazuka. Peleka haya maudhui kwa wengine ndani ya hilo kundi ovu.

Watu wa mawazo kama haya hawahitajiki huko, ndio maana mburulah Tlaatlaah ambaye ndiye mfano halisi wa mwana CCM bora anakupinga na kukushambulia.
Tatizo tunataka kupinga mawazo kwa kutumia mtutu wa bunduki kitu ambacho hatutafanikiwa, huyu Tlaatlaah ndio wanufaika wa mifumo mibovu unagemea atapenda ushauri?
 
Kama kweli wewe ni mwanaccm kindakindaki basi kumeshaanza kupambazuka. Peleka haya maudhui kwa wengine ndani ya hilo kundi ovu.

Watu wa mawazo kama haya hawahitajiki huko, ndio maana mburulah Tlaatlaah ambaye ndiye mfano halisi wa mwana CCM bora anakupinga na kukushambulia.
gentleman,
mimi simpingi yeyote yule jukwaani, ispokua naona ni unafiki mtupu mdau wa jf kutafuta utakatifu nyuma ya chama fulani cha siasa kueleza unafiki wake ambao eti yeye anaita ushauri

mie nadhani inafaa kujiepusha na hilo na itapendeza zaidi 🐒
 
Tatizo tunataka kupinga mawazo kwa kutumia mtutu wa bunduki kitu ambacho hatutafanikiwa, huyu Tlaatlaah ndio wanufaika wa mifumo mibovu unagemea atapenda ushauri?
Gentleman,
na ninakubali ushauri lakini sio unafiki kama huo ulioweka jukwaani

hakuna haja ya kuficha unafiki au kisingizio useless cha sijui cha mfumo au kunafaika kuficha unafiki wako. Ni vema kama mdau wa jf, kutoa hoja bila kujificha kinafiki kwenye mgongo wa chama fulani cha siasa kueleza porojo, upotoshaji na drama zako 🐒
 
Back
Top Bottom