Ibrambeya
Member
- Jul 25, 2014
- 36
- 2
Mimi naitwa Fred ... Ni baba wa familia ya Mke na watoto wawili, naipenda familia yangu na tunaishi vizuri. Kikubwa nilipata promotion kazini Hali iliyolazimu niiache familia yangu pale tulipojenga Makazi yetu ili nikajenge Mazingira ya kuwarudia au kuachana na kazi hiyo kama ikinishinda. Kufika kazini nilikutana na binti mrembo na mzuri, sikubabaika sana nilimuona wa kawaida..... Siku zilipokwenda tukaanza kuwa na hisia za mapenzi juu yetu.... Aliniambia ana mchumba wake amemuacha Bukoba na Mimi nilimwelekeza familia yangu iko Songea.... Wakati huo tuko Arusha kikazi...... Kweli tukawa wapenzi kwa Siri na Ikifika Likizo kila mtu anaheshim mahusiano ya mwenzake.... Baada ya miez mitatu mdada alinijuza kwa busara sana anahisi ni mjamzito.... Nilivuta pumzi.... Tukakubaliana tukapime.. Kweli alikuwa ni mjamzito.... Lahaula... Ikiwa imebaki miezi sita tu ili akafunge ndoa na mchumba wake Huyo wa Bukoba..... Tukajadili tuitoe mimba hiyo ili kuzinusuru ndoa zetu, Japo tulijua ni dhambi kwa Mungu na jamii .... Japo alisisitiza yeye kabaki na mama pekee na mama alimuasa "ukipata ujauzito bila kutarajia... Chonde Chonde usitoe yatakukuta makubwa"... Kwa msaada wa mtaalam wa afya tukakubaliana tujaribu... Kwel tukafanya.... Kuja kucheki ultra sounds..... Mimba haikutoka na binti akaugua pomoni... Zaidi kumbe alikuwa na Maralia iliyojificha na pia upungufu wa damu... Hivyo vyote vikawa juu.. Damu Ilikuwa 5 ya 11 na Maralia... Takriban 11... Lahaula... Mimi ndo pekee niliyekaribu nae hapa Arusha.... Nikamuuguza hospital ya Mkoa kwa muda wa wiki na nyumbani wiki hadi akapona kabisa.. Nikiwa hoi hadi kitambi kuisha.... Yeye alinambia neno moja tu "Nimeamini unanipenda"..... Uzuri Ilikuwa kipindi cha Likizo Hivyo wote tulichelewa kwenda kwenye familia zetu.... Inshu ikawa ujauzito una miezi minne... Atamwambia nini mama yake ambae ni mjane na mboni yake ni yeye pekee... .. Koo za mchumba wake na za binti zimeshaanza kuwa Karibu kwa sababu ya vijana wao.... . Mipango ya harusi inaendelea.... Nikamsihi.. Aende Bukoba akamwambie Ukweli mpenzi wake kuwa alichepuka na ni mjamzito, pia aliugua muda mrefu, na hatua atakazo chukua basi Itakuwa imepangwa....... Kila hatua alinijuza kuwa kamweleza mchumba wake yote...... Ila mchumba wake alilia sana kwa nini alimsaliti!.... Baadae akampa sherti moja kuwa wafunge ndoa haraka sana kabla hajajifungua. Kweli ndoa iliandikishwa.... Kadi na kamati vikatengenezwa.. Mipango ya harusi ikafanyika.... Ulikuwa ni usiku wa kiza.... Totoro..... Mida ya Saa nane na robo usiku .... Binti Alinipigia simu akiwa analia..... Kuwa tumbo linamuuma.... Na anapelekwa Hospital... Kweli alipelekwa na kupewa kitanda. .. Kufika asubuhi Saa nne Alinipigia simu akinieleza.. Chupa ya uzazi imepasuka... Na kufika Saa saba na nusu mchana akajifungua kwa operation..... Saa kumi jioni alinipigia simu kwa furaha akasema amejifungua mtoto wa kiume..... Nikampa pole na Hongera..... Usiku wake alinijuza nitoe jina la mtoto nami Nilifanya Hivyo kwa kumpa jina la Baba yangu mzazi... Kumbuka Yuko hospital na zimebaki siku Tatu ifike siku ya ndoa na Ndugu wa mbali wameshaanza kusogea.... Ukoo ulipokaa wakaamua... Binti ajikaze na ndoa ifungwe maadam amejifungua tayar..... Kweli kesho yake wakaomba ruhusa na kutoka hospital.... Ndoa ikafungwa.... Nami Nilimuagiza best friend japo ni mbali Bukoba...... Hadi Arusha, nae akashiriki Maelezo ya jamaa yangu ni kuwa ... Aliia sana binti.. Hasa alipokuwa akimuona yeye.... Kama mtu ambae hakufurahia ndoa hiyo... .. Zoezi likaisha... Kikubwa nilichokiona ni kuwa ndoa yake haikumbadili kitu.. Bado alipenda sana mawasiliano nami..... Nilijitahidi kumzuia.... Lakini wapi.... Kwangu niliacha kabisa kumpigia ila yeye ni lazima moja mara tatu.... Kwamba asubuhi lazima apige, mchana apige na jion hata message.... Ilibidi nimpokee kwa kuwa sasa ni mzazi mwenzangu..... Japo nilimuomba Mungu tusifanye tena mapenzi nae kwani ni mke wa Mtu sasa..... Baada ya muda wakaja na mumewe Arusha mimi nikiwa Likizo .... Kuna jiran yangu alikuwa akimtaka sana kimapenzi binti yule nami binti alinambia..... Akamkuta mumewe na kumpa A -Z juu ya mahusiano yangu na binti Huyo ... Kwani kabla tulikuwa tunafanya kazi ofisi moja na ofisi ilitupa nyumba moja...... Kwa kugawana vyumba.... Kiukweli Ilikuwa nyumba kubwa ya vyumba vinne na Sebule.... Japo iliachanishwa na kuta flani ila geti moja.. Tulikuwa tunaishi watatu.... Mimi, Binti na Mfanyakaz mwenzetu...... Hivyo kwa mgeni lazima angejua lazima ni mke wa jamaa yangu au wangu...... Tulikula na kupika pamoja....... Alipopata Habari mumewe Alianza kunitumia message za vitisho..... Nilikauka sikujibu.... Baada ya muda niliona nikikaa kimya haita nisaidia.... Siku moja nilimpigia na kumuomba tuzungumze kwa kirefu..... Na ikawa....... Kweli.. Tuliongea mengi kwa muda wa masaa matatu na yeye aliridhika ila nilimueleza mimi ni binadamu na niliteleza kuwa na mahusiano na binti Huyo kabla hajaoa... Hivyo ni Marafiki tu kwa sasa na ni mfanyakazi mwenzake.... Jamaa akadai.... Tusaidiane kumtafutia binti uhamisho Aende Bukoba..... Tukaweka mipango..... Japo nikamtahadharisha...... Kuwa aliyempa taarifa ni mtu mzuri ila nae alikuwa anamhitaji binti..... Tukapanga kukutana.. Pia akanipa condition nimjibu yule ni mtoto wangu au Vipi.... Nikamwambia mtoto mwenye Siri ni mama.. Hivyo ambane mkewe Atamwambia, japo hitimisho ikawa nimbane mkewe pia akinijibu nae nimwambie ... Wakati Nataka nianze safari.... Baba yangu mzazi akafariki ikabidi niahirishe safari ya kwenda kazini na niende msibani..... Iliniuma kwa kuwa mamangu mzazi alitangulia nikiwa primary....... Tulizika na nikaona ni mwaka wa mkosi Kwangu........ Why always me..... Kabla sijarud kazini ikatoka barua nyingine ya kwenda kuripoti katika ofisi zetu mjini Moshi...... Nikaenda kuripoti..... Na kupanga mipango ya kazi..... Nikiwa njian kufuata familia yangu ambayo mambo Haya Bado hawana taarifa nayo....... Ninavyomfahamu mke wangu akisikia naongea na simu ya Mwanamke hata Dada yangu anaumwa.... Akigundua Nina mtoto na mke wa Mtu Itakuwaje.... Najitajidi sana kumsisitiza binti ampende mumewe pia nikagundua.... Mume anaendeshwa na mke mana message za mwanzo nilimfowardia na kumueleza aache kunitafuta kila mara labda kwa shida za mtoto au kubwa.... Kumbe ikawa Kesi tena jamaa akaomba msamaha kuwa hatanipigia tena..... KIBAYA ZAIDI....... Juzi jamaa Ameanza kunitumia message za vitisho tena ..... Nataman kufanya mengi.... Ila nashindwa Nianzie wapi..... Mbele giza.... Nilipo giza..... Naithamini damu yangu... Ya jina la Baba yangu mzazi aliyetangulia mbele yake hivi punde ....... Siwez itupa kwani nikifanya Hivyo napo kwa binti ni kilio kingine.... Mana inaonesha jamaa hampendi hata kidogo mtoto Huyo .... MAWAZO YENU WADAU.......