Habari wana mmu! nimekuwa kwenye mahusiani na binti mmoja takribani miaka 3 tulianza mahusiano kipindi tukiwa chuo kiukweli tulipendana sana na kupeana support ya kimaisha kwani familia zetu zina uwezo wa kati,baada ya kumaliza chuo mwenzangu alipata kibarua lakini pia nilikuwa namsupport kwa kuwa nilipata kazi kabla yake.Baada ya muda kidogo nilianza kuona mabadiliko kwa upande wake nikaamua kufanya uchunguzi ni kweli nikagundua anamahusiano na bossi wake ambae ni mme wa mtu,niliumia sana nikamwita akakubali nakuomba msamaha na kaniomba sana tuendelee na mahusiano yetu ya awali,kaapa kuto rudia tena na anatafuta kazi sehemu nyingine ili pale aache kwani anasema ni shetani alimpitia baada ya kushawishiwa na bosi na pia yule bosi ananijua vizuri kuwa huyu ni mchumba wangu.Kiukweli bado nampenda na tulipanga november 2016 tufunge ndoa sasa hapa nafanyaje wakuu? Naombeni ushauri wenu