Ushauri wa wazi kwa J. J. Mnyika (Mb)

Ushauri wa wazi kwa J. J. Mnyika (Mb)

attachment.php

Makubwa haya
 
Yakipatikani maji kimara yote mpaka mbezi,mwakani agombee tofauti na hapo atafute jimbo lingine.

Miaka hamsini hata kujua kuwa ubungo lilikuwa ni jimbo tulikuwa hatujui,ukiacha mnyika ambae ndo ameleta hata goodwill ya jimbo kwa maana ya kujulikana na watu wengi,amini usiamini majimbo mengi yanayoshikwa na watawala ukiacha kukosa huduma nyingi za kijamii kwa muda mrefu hata hayajulikani manake wabunge wake ni mabubu.
 
Acheni kubeza,mnyika kafanya Mambo mengi,unataka hadi uyashike kwa mikono ndio uamini.?
Kanyaga twende J.J.Mnyika kijana shupavu na hodari katika medani za siasa Safi.
 
Hivi kwanini John Mnyika hana degree wakati amewahi kuwa mwanafunzi wa evening class udsm?
 
Mnyika wana ubungo hawakukosea kukupa ubunge kamwe! Unawatendea mema wana ubungo, unawatendea mema watanzania!

Mkuu, ni kweli kabisa, mimi tangu nipate akili na kufuatilua siasa za Dar, Ubungo haijawahi kupata Mbunge mahiri kama JJ Mnyika.

Nilikuwepo enzi za Hussein Hading'oka, akaja Ngula, akafuata Lamwai ambaye aling'olewa na Mahakama, kisha Charles Keenja.

Ktk wote hao niliowataja, hakuna aliyefikia viwango vya Mnyika.

Vv
 
Amefanya nini cha maana ktk jimbo lake tangu ameingia?

Una maana gani? Kufanya nini kama kipi?

Mnyika ni Mwakikishi bora kabisa wa wananchi ktk mkoa wote wa Dar es salaam.

Ktk Wabunge wote wa Dar, Wabunge vilaza kabisa ni wale wa CCM ukimweka kando Dk. Ndugulile wa Kigamboni, Wabunge kama Mtemvu wa Temeke, Mahanga wa Segerea, Mwaiposa wa Ukonga, Zungu wa Ilala na Idd Azan wa Kinondoni.

Vv
 
Mh. Mnyika,nilikufahamu tangu ulipogombea Ubunge wa Ubungo kwa mara ya kwanza mwaka 2005 dhidi ya Charles Keenja. Wakati huo nilikuwa mwanachuo wa mwaka wa kwanza UDSM nikichukua Sheria. Ingawa sikuwa mpigakura wako kwakuwa nilijiandikisha Kibaha,nilikuunga mkono. Ukiwa kijana na mwanafunzi mwenzetu UDSM,tulijivunia uwepo na ugombea wako.

Mh. Mnyika,mwaka 2010 nilihamisha kituo changu cha kupígia kura kwa ajili yako. Nikahamisha toka Kibaha hadi Ubungo. Nikakupigia kura Nkrumah Hall UDSM nikitambua uwezo,nia na sababu zako za kuwa Mbunge wa Ubungo. Safari hii nikiwa mwajiriwa wa UDSM. Ukamshinda Hawa Ng'umbi wa CCM na kuwa Mbunge.

Tangu kuwa Mbunge,hukuwahi kutuangusha kama vijana katika hoja na msimamo wa kitaifa. Umekuwa ukiongozwa na kauli zithibitikazo kwa nyaraka na tafiti mbalimbali. Hakika vijana wa Tanzania unatuwakilisha vyema na tunajivunia kukuchagua kuwa Mbunge wa Ubungo.

Nakushauri mambo mawili. Mosi,uanze upya au umalizie elimu ya juu yako. Tunahitaji ubongo wako ulioimarika zaidi kielimu. Elimu ya juu kwa nafasi na uwezo wako wa kiuongozi haiepukiki. Pili,endelea kuwatumikia wananchi wako wa Ubungo na Tanzania kwa ujumla kwa weledi,uwezo na bidii uliyojaaliwa. Asante


Hapo kwenye red mkuu naomba ufanunuzi wa kisomi? kwanini elimu ya juu? Kwani ubongo unaimarika na elimu ya juu pekee? Kwanini sasa? Asomee nini na kwanini? Mbona kuna watu humu avatar zao wamevaa majoho ya vyuo vikuu lakini michango yao wala haishahabiani na avatar zao? Ahsante
 
Hivi kwanini John Mnyika hana degree wakati amewahi kuwa mwanafunzi wa evening class udsm?

Watu huwa wanaongeza maarifa pale wanapoona kuwa kuna mahitaji,kuna wafanyabiashara wengi wamemaliza secondary tu wakawa succsefull kwa yale wanayofanya hivyo kuona hakuna haja ya maarifa mengine kuna nchi ambazo huwa wanakuwa awarded degrees sababu wamedemonstrate practical entrepreneurship bila shule,kwetu hapa kuna maprofesa wa dev.studies na entrepreneurship hata banda la kuku hawana,to me unamaliza undergraduate ukiona imeshindwa kukusaidia kufikia malengo yako, u opt for masters, uona bado unaendelea and so on,
 
Una maana gani? Kufanya nini kama kipi?

Mnyika ni Mwakikishi bora kabisa wa wananchi ktk mkoa wote wa Dar es salaam.

Ktk Wabunge wote wa Dar, Wabunge vilaza kabisa ni wale wa CCM ukimweka kando Dk. Ndugulile wa Kigamboni, Wabunge kama Mtemvu wa Temeke, Mahanga wa Segerea, Mwaiposa wa Ukonga, Zungu wa Ilala na Idd Azan wa Kinondoni.

Vv

Amelifanyia nini jimbo lake?
 
Watu huwa wanaongeza maarifa pale wanapoona kuwa kuna mahitaji,kuna wafanyabiashara wengi wamemaliza secondary tu wakawa succsefull kwa yale wanayofanya hivyo kuona hakuna haja ya maarifa mengine kuna nchi ambazo huwa wanakuwa awarded degrees sababu wamedemonstrate practical entrepreneurship bila shule,kwetu hapa kuna maprofesa wa dev.studies na entrepreneurship hata banda la kuku hawana,to me unamaliza undergraduate ukiona imeshindwa kukusaidia kufikia malengo yako, u opt for masters, uona bado unaendelea and so on,

Kwahiyo aliacha kusoma baada ya kuona degree haitamsaidia kitu... au baada ya kuona kwamba haitaji degree ili kufanya shughuli zake? Don't get me wrong, mimi binafsi namkubali sana John Mnyika kwa utendaji wake. Tena yeye ni mfano mkubwa sana wa kuigwa na kuonyesha kwamba mtu haitaji kuwa na degree ili kuwa mwanasiasa mzuri. Swali langu tuu nilitaka kujua kama aliacha kusoma, alifukuzwa, au alikuwa "discontinued".
 
Pendekezo la kusoma degree ni zuri lakini si mhimu. Ufanisi wa mtu hasa katika siasa haitokani na idadi ya degrees. Wewe uliyeko University unafundisha ndiyo unatakiwa usome degrees zote maana usipofanya hivyo hutakuwa na kibarua. Laprofeseri Mhongo na Tibaijuka wamelisaidia nini taifa pamoja na kuwa na degrees zote? Is no sense. Watu wengi waliofanikiwa hawana hata hizo degrees unazozisema. Tuachane na huo utumwa wa kimtazamo. Tuwachague wagombea kwa uwezo wao kuchapa kazi na siyo idadi ya degrees.
 
Amelifanyia nini jimbo lake?

Kwa tunaoishi kimara tunajua angalau mabomba ya wachina cku iz yana mgao kidogo wa maji. Lakn ukiacha hilo kama govt hitoi hela ya maendeleo unataka atoe hela yake mfukoni we ----? ubungo upinzan hata waweke jiwe litachaguliwa jiwe habar ndo hiyo,utaki kula wembe ufe.
 
Kwa tunaoishi kimara tunajua angalau mabomba ya wachina cku iz yana mgao kidogo wa maji. Lakn ukiacha hilo kama govt hitoi hela ya maendeleo unataka atoe hela yake mfukoni we ----? ubungo upinzan hata waweke jiwe litachaguliwa jiwe habar ndo hiyo,utaki kula wembe ufe.

Acha kujidanganya kikao cha juzi kimara mwisho amezomewa na kina mama baada ya kumuuliza maji uliyotuahidi yako wapi? Maji hakuna jimbo lake? Atoe hela yake? Inamaana Halima Mdee anatoa hela yake mfukoni kutengeneza barabara na makaravati? Maji? Mfuko wa kuendeleza jimbo wanaopewa bungeni anapeleka wapi? Subiri 2015 akipita nigeuke jiwe.
 
namkubali mnyika,lkn kuongoza ubungo ni kama kuongoza nchi.

kaka umejisahau sana.

umewaaahau kina keenja eee
 
Uyu nabii naye katokea wapi kila mda untaka kukutana na Rais ivi umekosa watu wa kukutana nao?
mfate ata kakobe basi akushauri una njaa mpk mungu anakushangaa
 
Kwahiyo aliacha kusoma baada ya kuona degree haitamsaidia kitu... au baada ya kuona kwamba haitaji degree ili kufanya shughuli zake? Don't get me wrong, mimi binafsi namkubali sana John Mnyika kwa utendaji wake. Tena yeye ni mfano mkubwa sana wa kuigwa na kuonyesha kwamba mtu haitaji kuwa na degree ili kuwa mwanasiasa mzuri. Swali langu tuu nilitaka kujua kama aliacha kusoma, alifukuzwa, au alikuwa "discontinued".


As long as ana deliver sifahamu wala siitaji kufahamu personal issues za mtu. Mnyika peke yake ni sawa na basi la marcopolo lililojaa wabunge wenu wale wa "wanafiki waseme ndio" wanajibu "ndiooooo" ukimtoa filikunjombe.
 
Back
Top Bottom