Ushauri wa wazi kwa J. J. Mnyika (Mb)

Ushauri wa wazi kwa J. J. Mnyika (Mb)

Pia barabara ya Suka - Golani kuwa kiwango cha lami hajatimiza
 
Atenge muda kutembelea wapiga kura kuliko kushinda mtaani UFIPA
 
Pamoja na ushauri mzuri.Ila sikubaliani na kwenye nyekundu. Maisha ni malengo na nini kiwecha kipaumbele-ni kweli kati harakati hii ya ukombozi wa Pili wa Nchi yetu hakuna ubishi Mh.JJ Mnyika hakosi kuwa kati ya Tatu Bora ya Vijana.

Na hilo la Elimu ya juu kuwa jambo la lazima kwa suala la kiuongozi kwangu ni jambo la kupuuzwa na si kuhusudu sana maana historia imeliproof wrong.
Jiridhishe na hawa hapa chini kabla hujawaaminisha wengi.



Nje ya Africa;


Kila kitabu na zama zake. Nakubaliana na wewe kuwa kuna watu wamefanya makuu bila elimu kubwa, lakini hizi si zama za kuenzi hilo suala kwani hakuna vikwazo vya kielimu kama zamani. Kwa umri wa Mnyika bado anayo nafasi ya kujiendeleza zaidi kielimu ili kuendeleza kipaji chake. Asiridhike na mawazo kuwa elimu sio lazima.No Mnyika Please! elimu ni muhimu sana kwa kizazi cha sasa usije kubweteka itakukosti baadae.


Naoungana na Petro, Mnyika sasa hivi nafasi za kujiendeleza kielimu ni nyingi mno. hata kama UDSM walikubania bado unayo nafasi kubwa kwenye vyuo nvingine ndani na nje ya nchi. Changamkia fursa uliyopata before it is too late!
 
Mh. Mnyika,nilikufahamu tangu ulipogombea Ubunge wa Ubungo kwa mara ya kwanza mwaka 2005 dhidi ya Charles Keenja. Wakati huo nilikuwa mwanachuo wa mwaka wa kwanza UDSM nikichukua Sheria. Ingawa sikuwa mpigakura wako kwakuwa nilijiandikisha Kibaha,nilikuunga mkono. Ukiwa kijana na mwanafunzi mwenzetu UDSM,tulijivunia uwepo na ugombea wako.

Mh. Mnyika,mwaka 2010 nilihamisha kituo changu cha kupígia kura kwa ajili yako. Nikahamisha toka Kibaha hadi Ubungo. Nikakupigia kura Nkrumah Hall UDSM nikitambua uwezo,nia na sababu zako za kuwa Mbunge wa Ubungo. Safari hii nikiwa mwajiriwa wa UDSM. Ukamshinda Hawa Ng'umbi wa CCM na kuwa Mbunge.

Tangu kuwa Mbunge,hukuwahi kutuangusha kama vijana katika hoja na msimamo wa kitaifa. Umekuwa ukiongozwa na kauli zithibitikazo kwa nyaraka na tafiti mbalimbali. Hakika vijana wa Tanzania unatuwakilisha vyema na tunajivunia kukuchagua kuwa Mbunge wa Ubungo.

Nakushauri mambo mawili. Mosi,uanze upya au umalizie elimu ya juu yako. Tunahitaji ubongo wako ulioimarika zaidi kielimu. Elimu ya juu kwa nafasi na uwezo wako wa kiuongozi haiepukiki. Pili,endelea kuwatumikia wananchi wako wa Ubungo na Tanzania kwa ujumla kwa weledi,uwezo na bidii uliyojaaliwa. Asante
Hapo penye red toa ufafanuzi juu ya kiwango cha elimu Mh. Mnyika alichofikia!!!!
 
Lema ,sugu na mbowe mbona hujawakumbusha kurudi shule pia wanaongoza akili kubwa kina zito kabwe.
 
Mh. Mnyika,nilikufahamu tangu ulipogombea Ubunge wa Ubungo kwa mara ya kwanza mwaka 2005 dhidi ya Charles Keenja. Wakati huo nilikuwa mwanachuo wa mwaka wa kwanza UDSM nikichukua Sheria. Ingawa sikuwa mpigakura wako kwakuwa nilijiandikisha Kibaha,nilikuunga mkono. Ukiwa kijana na mwanafunzi mwenzetu UDSM,tulijivunia uwepo na ugombea wako.

Mh. Mnyika,mwaka 2010 nilihamisha kituo changu cha kupígia kura kwa ajili yako. Nikahamisha toka Kibaha hadi Ubungo. Nikakupigia kura Nkrumah Hall UDSM nikitambua uwezo,nia na sababu zako za kuwa Mbunge wa Ubungo. Safari hii nikiwa mwajiriwa wa UDSM. Ukamshinda Hawa Ng'umbi wa CCM na kuwa Mbunge.

Tangu kuwa Mbunge,hukuwahi kutuangusha kama vijana katika hoja na msimamo wa kitaifa. Umekuwa ukiongozwa na kauli zithibitikazo kwa nyaraka na tafiti mbalimbali. Hakika vijana wa Tanzania unatuwakilisha vyema na tunajivunia kukuchagua kuwa Mbunge wa Ubungo.

Nakushauri mambo mawili. Mosi,uanze upya au umalizie elimu ya juu yako. Tunahitaji ubongo wako ulioimarika zaidi kielimu. Elimu ya juu kwa nafasi na uwezo wako wa kiuongozi haiepukiki. Pili,endelea kuwatumikia wananchi wako wa Ubungo na Tanzania kwa ujumla kwa weledi,uwezo na bidii uliyojaaliwa. Asante

Petro unataka Mnyika aongeze Elimu na amalizie chuo ili apate cheti (cha kumaliza)?? Kama ni kuongeza Elimu, sawa!!! Ila kikubwa utueleze kinaga ubaga, ni kipi umeniona kimepungua kwake ili aende KUONGEZA chuoni???? Manake husishauri kitu bila kuelewa sawasawa! Je akasome SIASA ZA KUONGEA jukwaani au akamalizie Civil Engineering yake??? Je taaluma hiyo, itaongeza kipi cha ziada unachofikiri hana??Tatizo lako unafikiri zaidi KUPATA cheti kuliko KUONGEZA Elimu.You are too Academician than professional!Ushauri wako ungekuwa na maana kama ungesema umeona upungufu gani kwa J.J Mnyika.Please, think differently!!!
 
.... Mbona Akina Prof Tibaijuka, Muhogo, Kikwete, Na Wengine, Pamoja Na Elimu Yao Lakini Ni Mambumbumbu Kiuongozi. Degrii Moja Inatosha Sana.
 
... Ulitaka Tu Kutwambia Kwamba Wewe Sasa Hivi Ni Mwajiriwa Wa Udsm, Basi Tumejua Kaka, Hongera Sana...
 
.... Mbona Akina Prof Tibaijuka, Muhogo, Kikwete, Na Wengine, Pamoja Na Elimu Yao Lakini Ni Mambumbumbu Kiuongozi. Degrii Moja Inatosha Sana.

Mnyika hana hata hiyo moja! Nadhani ndiyo chimbuko la ushauri.
 
Kwani Mnyika hana digrii? Binafsi naona uelewa wake na jinsi anavyochambua masuala mbalimbali ni kama ana Masters vile. Kama kweli hana ni bora asome aipate - lakini isiwe digrii fake kama ya akina Agustine Mrema na wengineo

Malizia mkuu wengineo kina nani?wataje tafadhali
 
attachment.php
 
Amefanya nini cha maana ktk jimbo lake tangu ameingia?
 
Back
Top Bottom