commited
JF-Expert Member
- Feb 27, 2012
- 1,626
- 870
​Habari za usiku ndugu zangu! Natumaini kwa uweza wa Muumba wote mko salama, ninaushauri wa baadhi ya mambo kwa Chama kikuu cha UPINZANI(CHADEMA) Hasa kwa kile kinachoendelea bungeni. Najua viongozi, kama Mbowe, Zito, Mnyika, Lissu, Dkt K. Mkumbo mtapita huku na wengineo wengine zingatieni haya ili wananchi waweze kuwatofautisha nyinyi na Wakina Lusinde (CCM)
1. Nimesikitishwa sana, tangu bunge hili limeanza wabunge wa CDM, wameshindwa kuelewa mikakati ambayo CCM, wameiweka. CCM wamejipanga kuhakikisha CDM haijadili tena kwa kina na kwa busara mada mbalimbali zinazo wagusa moja kwa moja wananchi.
Na hilo CCM wanalifanya mahususi ili wananchi wapoteze imani na CCM waone mbona nao wako sawa tu kimawazo, na kimatendo tu kama CCM, Kwa sababu woote hawawatetei wananchi.. bali ni vijembe na vituko ndivyo wanavyoweza. CCM kupitia Spika pamoja na makada wake kama wakina Stella Manyanya, Chemba, Wasira,Lukuvi na hata baadhi ya Wabunge wa vyama vya CUF, NCCR au UDP, wamekuwa wakiwashambulia CDM waziwazi tena kwa shutuma zisizo na tija.
Badala ya kueleza mikakati na hatua za kutatua matatizo ya wananchi kama vile kuhakikisha serikali inaboresha huduma za jamii, inatatua kero zamuda mrefu zinazo wakabiri wananchi, kupanda kwa mfumuko wa bei, kutekeleza kwa vitendo upunguzaji wa matumizi ya serikali, ili fedha zitakazopatikana zisaidie kuboresha miundombinu, pamoja na huduma za kijamii na nk, CCM imejipanga kuwatoa katika mstari CHADEMA, ili nao waingie katika malumbano tu.
CCM na hao niliowataja wanafanya makusudi kukishambulia CDM, kwani wanajua wazi kwa sasa CDM, ndiye Mpinzani wake na wanamikakati mingi ya kukiangamiza kabla ya 2015(Ntaieleza siku nyingine). Wanachokifanya CCD na et al.. Ni kuwatupia CDM vijembe, na kebehi, ili CDM( WABUNGE) WAKASIRIKE, na hivyo kuhamaki na kutoka katika kujadili hoja na hivyo kuishia kuendeshwa na spika kwa kuomba miongozo, na utaratibu.
Ninachowashauri jikiteni kujenga HOJA, hasa zile zenye maslahi kwa wananchi ili wananchi waweze kuwatofautisha nyinyi na Vyama vingine hasa CCM, Onyesheni Busara na hekima wakati mwingine kaeni kimya tu, angalieni mbele daima, acheni wakina Lusinde na wengineo waendeleze yao, ila nyinyi fanyeni muwezalo kuhakikisha mnazidi kujenga imani kwa wananchi kwa kuwasemea matatizo yao kila hoja inapokuja mezani. Msishindane na Tuhuma shindaneni kwa hoja, wananchi watawaamini sana, kwamba hata siku mkipewa nchi hamtaiuza au kufanya mambo kwa jazba kama serikali iliyopo inavyofanya. Muheshiwa Mbowe waeleze wabunge wako haya....
2. CHADEMA, jihadharini sana na lugha kali, na za kuudhi muwapo majukwaani au mahali popote pale kwani zaweza kuwapelekea, kuonekana kama ni watu mnaotumia mabavu zaidi badala ya hoja na elimu. JITAHIDINI SANA wananchi wanataka kusikia sera zenu ni zipi, mtawasaidiaje ili rasilimali zilizopo ziwasaidie kutatua changamoto za maisha pamoja na kuwasaidia wao kumudu gharama za maisha zinazopanda kila wakati ambazo tayari JK zimeshamshinda na hana uwezo tena wa kukabiliana nazo tena
3. Top layer ya Chadema na Wanachama woote naomba Msali sana KUMUOMBA MUNGU KWA DHATI awaepushe na kila aina ya hila zinazopangwa kwa ustadi mkubwa na maadui zenu, kupitia miongoni mwenu. Ili Mwisho wa siku msiweze tena kuzungumza lugha moja, hii miaka mitatu ijayo inaweza kuwa ndio mwisho wenu wa kuvuma, na kukubalika kwa chama katika jamii.
Kumbukeni maadui wenu wa kisiasa na serikali yao yenye makachero takribani 250,000, na Watumishi wake vya vyombo vya usalama na nyadhifa mbalimbali takribani ya 400,000 hawatakuwa tayari ajira zao ziingie mchanga kirahisi kama mnavyodhani. Mtangulizeni Mungu kwa kila Jambo.
Mungu ibariki Tanzania.
1. Nimesikitishwa sana, tangu bunge hili limeanza wabunge wa CDM, wameshindwa kuelewa mikakati ambayo CCM, wameiweka. CCM wamejipanga kuhakikisha CDM haijadili tena kwa kina na kwa busara mada mbalimbali zinazo wagusa moja kwa moja wananchi.
Na hilo CCM wanalifanya mahususi ili wananchi wapoteze imani na CCM waone mbona nao wako sawa tu kimawazo, na kimatendo tu kama CCM, Kwa sababu woote hawawatetei wananchi.. bali ni vijembe na vituko ndivyo wanavyoweza. CCM kupitia Spika pamoja na makada wake kama wakina Stella Manyanya, Chemba, Wasira,Lukuvi na hata baadhi ya Wabunge wa vyama vya CUF, NCCR au UDP, wamekuwa wakiwashambulia CDM waziwazi tena kwa shutuma zisizo na tija.
Badala ya kueleza mikakati na hatua za kutatua matatizo ya wananchi kama vile kuhakikisha serikali inaboresha huduma za jamii, inatatua kero zamuda mrefu zinazo wakabiri wananchi, kupanda kwa mfumuko wa bei, kutekeleza kwa vitendo upunguzaji wa matumizi ya serikali, ili fedha zitakazopatikana zisaidie kuboresha miundombinu, pamoja na huduma za kijamii na nk, CCM imejipanga kuwatoa katika mstari CHADEMA, ili nao waingie katika malumbano tu.
CCM na hao niliowataja wanafanya makusudi kukishambulia CDM, kwani wanajua wazi kwa sasa CDM, ndiye Mpinzani wake na wanamikakati mingi ya kukiangamiza kabla ya 2015(Ntaieleza siku nyingine). Wanachokifanya CCD na et al.. Ni kuwatupia CDM vijembe, na kebehi, ili CDM( WABUNGE) WAKASIRIKE, na hivyo kuhamaki na kutoka katika kujadili hoja na hivyo kuishia kuendeshwa na spika kwa kuomba miongozo, na utaratibu.
Ninachowashauri jikiteni kujenga HOJA, hasa zile zenye maslahi kwa wananchi ili wananchi waweze kuwatofautisha nyinyi na Vyama vingine hasa CCM, Onyesheni Busara na hekima wakati mwingine kaeni kimya tu, angalieni mbele daima, acheni wakina Lusinde na wengineo waendeleze yao, ila nyinyi fanyeni muwezalo kuhakikisha mnazidi kujenga imani kwa wananchi kwa kuwasemea matatizo yao kila hoja inapokuja mezani. Msishindane na Tuhuma shindaneni kwa hoja, wananchi watawaamini sana, kwamba hata siku mkipewa nchi hamtaiuza au kufanya mambo kwa jazba kama serikali iliyopo inavyofanya. Muheshiwa Mbowe waeleze wabunge wako haya....
2. CHADEMA, jihadharini sana na lugha kali, na za kuudhi muwapo majukwaani au mahali popote pale kwani zaweza kuwapelekea, kuonekana kama ni watu mnaotumia mabavu zaidi badala ya hoja na elimu. JITAHIDINI SANA wananchi wanataka kusikia sera zenu ni zipi, mtawasaidiaje ili rasilimali zilizopo ziwasaidie kutatua changamoto za maisha pamoja na kuwasaidia wao kumudu gharama za maisha zinazopanda kila wakati ambazo tayari JK zimeshamshinda na hana uwezo tena wa kukabiliana nazo tena
3. Top layer ya Chadema na Wanachama woote naomba Msali sana KUMUOMBA MUNGU KWA DHATI awaepushe na kila aina ya hila zinazopangwa kwa ustadi mkubwa na maadui zenu, kupitia miongoni mwenu. Ili Mwisho wa siku msiweze tena kuzungumza lugha moja, hii miaka mitatu ijayo inaweza kuwa ndio mwisho wenu wa kuvuma, na kukubalika kwa chama katika jamii.
Kumbukeni maadui wenu wa kisiasa na serikali yao yenye makachero takribani 250,000, na Watumishi wake vya vyombo vya usalama na nyadhifa mbalimbali takribani ya 400,000 hawatakuwa tayari ajira zao ziingie mchanga kirahisi kama mnavyodhani. Mtangulizeni Mungu kwa kila Jambo.
Mungu ibariki Tanzania.