Ukatibu mkuu wa chama ni nafasi nyeti na ya juu sana katika uongozi wa chama, kwa nafasi hiyo, katibu mkuu huzifahamu siri nyingi na nyeti za chama, mwenyekiti pamoja na viongozi wengine.
Kuenguliwa kwenye uongozi katika chama katika umri ambao bado una nguvu, nia na uwezo wa kuendelea kukitumikia chama na Taifa, sio salama.
Kwa siasa zetu zenye figisu na hila nyingi, Mh. Mnyika na Mbowe hawawezi kuwa huru na Amani ikiwa msiri wao (Mashinji) bado yupo hai na hajarizishwa na mambo kadhaa ktk chama.
Sio rahisi chadema iruhusu Mashinji apate ubunge au nafasi nyingine ya uongozi kwa kuhofia kwamba anayajua mengi kuhusu chama, uongozi na viongozi wake.
Kwa mantiki hii, Namshauri DKT Mashinji ahamie CCM ili kujikinga dhidi ya maadui ambao walikuwa marafiki.
DKT Mashinji asisubirie kuhujumiwa na Chadema ndipo ahame, atumie fursa hii. Waswahili wanasema 'Udongo uwahi, ungali maji'. Karibu C.C.M DKT MASHINJI.
Kuenguliwa kwenye uongozi katika chama katika umri ambao bado una nguvu, nia na uwezo wa kuendelea kukitumikia chama na Taifa, sio salama.
Kwa siasa zetu zenye figisu na hila nyingi, Mh. Mnyika na Mbowe hawawezi kuwa huru na Amani ikiwa msiri wao (Mashinji) bado yupo hai na hajarizishwa na mambo kadhaa ktk chama.
Sio rahisi chadema iruhusu Mashinji apate ubunge au nafasi nyingine ya uongozi kwa kuhofia kwamba anayajua mengi kuhusu chama, uongozi na viongozi wake.
Kwa mantiki hii, Namshauri DKT Mashinji ahamie CCM ili kujikinga dhidi ya maadui ambao walikuwa marafiki.
DKT Mashinji asisubirie kuhujumiwa na Chadema ndipo ahame, atumie fursa hii. Waswahili wanasema 'Udongo uwahi, ungali maji'. Karibu C.C.M DKT MASHINJI.