Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 39,924
- 61,707
Babu yangu alinishauri kwamba,mjukuu wangu ni vizuri kuzaa mapema kwa sababu matunda yake utakuja kuyaona uko mbeleni, sasa hivi kwa sababu ya ujana na 'u-much know' unaweza ukapuuzia ukaona ujinga kwa sababu ya kufuata mkumbo;hutojuta kuzaa mapema.Kwa hiyo ndugu zangu,ni vizuri kwa mwanaume aliye na miaka 35+ awe tayari ameanzisha familia au kuwa na mtoto/watoto,na kwa mwanamke ni vizuri kuwa umeolewa au kuwa na mtoto/watoto unapokuwa na umri wa miaka 30+.