Ushauri: Vyama vya Upinzani vifutwe, kibaki CCM pekee kama chama dola

Kaka msingi wa CCM ulisimikwa na mfumo wa katiba iliyopo. ni ngumu sana kuitoa CCM madarakani kwa mfumo wa katiba iliyopo. Ndiyo maana mfumo wa rasimu ya pili ya Warioba ulikuwa ni hatari sana kwa CCM kuendelea kubaki madarakani, ndiyo maana waliikataa.

Mimi nakuunga mkono kabisa, haina maana vyama vya upinzani kupoteza rasilimali zao wakati Rais ameshawekwa kabla hata ya uchaguzi.

upinzani wetu hauna watu makini unaongozwa na wasela,upinzani umericruit vijana wahuni ambao wanaondoa mvuto wa chama.tumeona wakati wa kampeni mambo ya kihuni.tazama vijana na washabiki waccm unajua wazi ni watu wa mikakati.vilevile kudandia watu waliotupwa na vyama vyao na kuwawafanya lulu.viongozi huandaliwa sio kuokotaokota.

Watanzania wanaakili sana tizama kuna sehemu wamechagua diwani mpinzani lakini urais wamepigia ccm.

Ccm inachaguliwa kwa kuwa hadi sasa ndio chama bora kuliko vingine.mtu na akili zako huwezi sema hata likiweka jiwe utalichagua kuliko ccm.huko ni kuvia ubongo na matokeo yake tunayaona.

Kinachotakiwa ni kujenga vyama bora kuliko ccm.na kuachana na viongozi ndumila kuwili.
 
Kwa ushauri wako mwenyewe, ni bora ungesema mfumo wa vyama vya kisiasa uondolewe, kusiwe na vyama vya siasa, wanaotaka kuwakilisha - na isiwe kwenye mfumo wa Bunge la Westminster - wawe wagombea huru wasio na vyama au itikadi yoyote ile.

Tubaki na SERA zinazotekelezeka!

Tumejaribu siasa, tumeshindwa, tuachane nayo. Haina mafunaa kwetu!
 
CHADEMA walimsaliti DR SLAA aliyekijenga Chama mpaka kupata ulemavu wakiamini kwamba LOWASSA atawavusha! Dhambi hii lazima iwatafune na mimi nasema lazima iwatafune maana walijitakia wenyewe kwa tama zao!
 
Uloi nga mâché68;14475138 said:
Vyama vya upinzani vinajiandalia vyenyewe mazingira ya kushindwa kwa kukosa mikakati thabiti ya ushindi na usaliti wao! Mfumo ungekuwa mbaya wasingeshinda majimbo mengi ya UBUNGE na UDIWANI!


kwa tabu mpaka wananchi wakomae maeneo mengi ambapo vyama vya upinzani vimeshinda matokeo hucheleweshwa kupita kiasi.
 
Nikupe history kidogo mfumo wa vyama vingi hatukuupenda kabisa lakni wazungu wakatwambia kama hamtakuwa na vyama vingi hatuwapi misaada so that tukaogopa kukosa misaada ndo kisa cha kuwa na mfumo wa vyama vingi
 
Kaka msingi wa CCM ulisimikwa na mfumo wa katiba iliyopo. ni ngumu sana kuitoa CCM madarakani kwa mfumo wa katiba iliyopo. Ndiyo maana mfumo wa rasimu ya pili ya Warioba ulikuwa ni hatari sana kwa CCM kuendelea kubaki madarakani, ndiyo maana waliikataa.

Mimi nakuunga mkono kabisa, haina maana vyama vya upinzani kupoteza rasilimali zao wakati Rais ameshawekwa kabla hata ya uchaguzi.
Kwa mwingine hatakuelewa kwa hili lakini hicho ndicho chanzo cha kuumiza upinzani, tazama Kenya walianza na katiba ndio maana wakafanikiw! Alaaniwe sana Samweli Sitta huu ya hilo. Hatuwezi kuendelea na katiba ya tangu enzi za Chama kimoja inayoependelea upande mmoja tu.
 
Acheni kuisingizia CCM ilhali Opposition wenyewe hawajui hata wanachokisimamia ni kipi.Ifike mahali haya magenge ya mchwa wala ruzuku yasiendelee kupewa kodi zetu, they've to find their own sources.
 
CCM kingesimama kama chama cha kiasa ungekuta kimekufa muda mrefu ila ccm kimesimama kama serikali, polisi, jeshi, usalama wa taifa n.k. Sasa nguvu zoote hivi huwez kushindana nazo

kweli kwa stahili hii hata tukishinda tukikesha huku tumefunga tukiomba hatuwezi, bado matokeo yatakuwa the same
 
CHADEMA wajilaumu wenyewe kwa usaliti wao kwa DR SLAA aliyekijenga Chama wakamsaliti kwa tama zao! Na mimi nasema dhambi hiyo lazima iwatafune kwa tamaa zao mpaka sasa wamekosa mwelekeo!
 
upinzani wetu hauna watu makini unaongozwa na wasela,upinzani umericruit vijana wahuni ambao wanaondoa mvuto wa chama.tumeona wakati wa kampeni mambo ya kihuni.tazama vijana na washabiki waccm unajua wazi ni watu wa mikakati.vilevile kudandia watu waliotupwa na vyama vyao na kuwawafanya lulu.viongozi huandaliwa sio kuokotaokota.

Watanzania wanaakili sana tizama kuna sehemu wamechagua diwani mpinzani lakini urais wamepigia ccm.

Ccm inachaguliwa kwa kuwa hadi sasa ndio chama bora kuliko vingine.mtu na akili zako huwezi sema hata likiweka jiwe utalichagua kuliko ccm.huko ni kuvia ubongo na matokeo yake tunayaona.

Kinachotakiwa ni kujenga vyama bora kuliko ccm.na kuachana na viongozi ndumila kuwili.
Hao wastaarabu wanapelekwa na nani upinzani?Kwani kama wapo kwa nini wasubiri kuitwa na hao wasela?Au kwa nini wasianzishe vyama vyao kuliko kulalamikia upinzani?Na kwa kweli kwa nini wawepo wapinzani tena?


Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Pole sana ndugu. Kwani unataka vyombo vya dola viwe upande wa upinzani?

Wapinzania nao pia ni walipa kodi tena wakubwa hujui vyombo vya dola vinatumia kodi za wananchi kulipia mishahara yao na uendeshaji?
 
CCM haiwezi kuondoka madarakani kwa sababu moja kuu.

Tanzania - au nchi yoyote barani Afrika - haijawahi kuwa na mfumo wa kidemokrasia iliyo halali.

Tanzania haifuati misingi ya demokrasia kwa kuwa demokrasia ni dhana ya kigeni, sio dhana ya Kiafrika.

Demokrasia ilianzia Ugiriki, na hata huko haikuwa demokrasia iliyo ya kweli.

Waasisi wa demokrasia - mmeshuhudia jinsi ambavyo Wagiriki wanaishi maisha duni mpaka leo na uchumi wao ulivyoporomoka - wameshindwa kusimamia misingi ya demokrasia, sisi ndio tutaweza?

Tuachane na demokrasia, turudi kwenye mfumo wa uongozi wa Kiafrika wa asili, tuone kama tutashindwa.

Wakoloni walifuta mifumo ya utawala wa Kiafrika ya asili, ili watuwekee ya kwao, ambayo iliwekwa KUTUTAWALA.

Tumerithi mifumo ya kitawala ya KIKOLONI, na tunatarajia kwamba haki na amani vitadumu?

Tuache porojo, tugange ya kwetu!

HAKUNA DEMOKRASIA BARANI AFRIKA!
 
Mbowe ndo ameua upinzani baada kumpokea Lowasa. Sasa CCM inapeta tu maana mtaani kwangu sisiki kabisa kelele za PEOPLES!!!!!! kuanzia jana baada ya matokeo ya Raisi kuanza kutangazwa.
 
Miaka takriban 23 sasa tangu kuanzishwa kwa Mfumo wa vyama vingi, ni chama kimoja tu ndicho miaka yote kinatawala na kuiongoza Tanzania. Kipindi cha upinzani (uchaguzi na kampeni) chama hichi tawala (CCM) kimukua kikinadi kua ni chama cha mapinduzi na kusema wao wamepindua na hawatoa nchi.

Ni wazi tu kuwa chama hiki cha mapinduzi hawashughuliki na uchaguzi ni msemo wao tu "ushindi lazima"

Wana JF mnalionaje hili si mfumo ufutwe tu tubaki na hiki chama cha CCM.

Mnakaribishwa wadau kutoa mchago yenu.


Ahsanteni.
 
Kwa mwingine hatakuelewa kwa hili lakini hicho ndicho chanzo cha kuumiza upinzani, tazama Kenya walianza na katiba ndio maana wakafanikiw! Alaaniwe sana Samweli Sitta huu ya hilo. Hatuwezi kuendelea na katiba ya tangu enzi za Chama kimoja inayoependelea upande mmoja tu.

Pengine unapendekeza njia ipi ya kupata katiba mpya? maana hata hilo tulijaribu na majibu yake unayajua! Kuanzia viongozi wa dini hadi watu wenye ulemavu walikuwa wanatetea katiba iliyochakachuliwa,sasa unadhani ni wapi pa kutokea?

CCM itabaki pale pale, CCM ni ile ile, polisi wake, jeshi lake, usalama wataifa wake, bunge lake,mahakama zake,utatokea wapi mkuu?

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
CCM oyeeeeee. Hapa Kazi tuu. Mabadiliko Mwachieni kinyonga
 
Nyie kateni tamaa lkn mimi siwezi kurudi Misri nitapambana mpaka nifike nchi ya ahadi,siwezi kuwaacha wanangu jangwani ki-raisi namna hii. Na hata nisipofika sina shaka nitakapoishia hapatakuwa mbali na nchi ya ahadi, jambo ambalo litawafanya wasitembee mwendo mrefu. Mungu nisaidie
Sawa kabisa mkuu. Tutapambana mpaka basi. Hakuna marefu yasiyokuwa na ncha. Ccm ipo siku itakufa tena bila kutarajia. Matokeo ya mwaka huu yatawapumbaza zaidi na kusahau hatari mbele.
 
Back
Top Bottom