Ushauri unahitajika....

Ushauri unahitajika....

mzee wa nguna

Senior Member
Joined
Dec 5, 2012
Posts
138
Reaction score
139
Kuna dada mmoja ambaye anafuatiliwa kwa saana na kaka mmoja. Mwanzoni huyo dada alianza kuufungua moyo wake kama amkubalie,lakini kadiri walivyoanza kuzoeana huyo dada amegundua kwamba mwenzie hakidhi kabisa vigezo vya kuwa mpenzi wake. Sasa kila akijaribu kumpotezea yule kaka anapagawa balaa,anabembeleza na kushawishi kwamba atamvumilia tu hivyo hivyo hata kama ham-feel eti atamsaidia kadiri safari ya maisha inavyosonga. Wanaishi mikoa tofauti,asipojibu meseji wala kupokea simu kaka wa watu anasafiri hadi aliko huyo binti.....afanyeje naye ameshaamua kwamba huyo mwanaume hamfai? Kwanza umri mdogo halafu anaganda sana,boring!
 
amwambie wazi, kwamba hamtaki.


Asante kwa ushauri. Ameshajaribu kumweleza kwa njia ya msg kwamba hana tena nia ya kuwa mpenzi wake...ndio kwaanza anazidi kubembeleza ooh kwani umekuwaje,mara nimekuudhi nini jamani nijirekebishe? N.k n.k...nadhani unaweza pata picha mpaka kuja kuomba ushauri humu JF kijana amekuwa kero,ni kama anatafuta kisingizio cha kucommit suicide
 
kuna njia nyingi za kukata mawasiliano na mtu ikiwemo kubadili laini bila kusema chochote,,kumwambia wazazi wameshakula mahari yangu bila mimi kujua so nasubiri kuolewa nakadhalika YAANI TAFUTA NJIA ZA KUMUACHA MTU BILA KUMUUMIZA
 
Huyo ndo kapenda kweli amkubalie tuuuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom