Ushauri tafadhali: Nimepata dawa ya kunasiana

Ushauri tafadhali: Nimepata dawa ya kunasiana

Compact Ltd

Member
Joined
Apr 15, 2015
Posts
8
Reaction score
0
Habarini wanajamvi,

Nimeamua kuja na ID ngeni hapa, kwa unyeti wa suala lenyewe, ikizingatiwa kuwa nina miaka saba hapa JF tena ni verified user, sio kawaida hili ninalotaka kunena leo nikawa huru kwa ile ID yangu.

Habari iko hivi

Mwezi April nilikuwa nimeenda nchi jirani katika mihangaiko ya kutafuta ridhiki, nikiwa huko nikakutana na mzee mmoja wa makamo hivi maeneo ya mashambani, kiukweli mi ni mtu wa utani, tulizungumza mengi sana huku tukitaniana, na hadi narudi ndiye alikuwa rafiki yangu kwa kule.

Siku moja kabla ya kuondoka tukawa tunazungumza stori za mahusiano, hadi nikajikuta namweleza my relationship history, jinsi nilivyosalitiwa na mchumba angu katika wakati mgumu na hatua za mwisho za kufunga ndoa.Mzee akaniambia kesho yake, siku ya kuondoka atanipa "zawadi" na ana imani nitaipenda tu. Asubuhi ikafika, mzee akawa kama mtu aliyesahau vile nami muda wa kuondoka umekaribia, nikamkumbusha..

Mzee kaingia ndani katoka na "habari nyingine" na akaniambia hiyo ndio dawa ya kumfunga mwanamke akifanya mapenzi na mwanaume mwingine watanasiana, yaani uume utashindwa kutoka sehemu za siri za mwanamke hadi uwategue ndipo sehemu zao zitajiachia.

Nilifadhaika kwa kweli, kwani toka nizaliwe sijawahi kujihusisha na mambo haya ya kienyeji, pili imani yangu hainiruhusu, ila upande mwingine ukiniambia "kweli kamzizi haka kanaweza fanya mambo yote hayo?" nikajipa moyo kwani nimewahi kusikia habari hizi kwa muda, ila kwangu ilikuwa kama ngano tu.

Nikarudi Tanzania, dhamira sasa nikataka kujaribu kama kweli ile "zawadi" inafanya kazi, sijaoa, sasa nitafanyeje? Nikamwita mpenzi, nikaijaribu kwake(lakini hakujua), kwa kuwa naamini na tuna ugomvi kwa muda sasa nikimtuhumu anatoka na jamaa, na jamaa nilimuonya, nikajua kama dawa ya kweli haitachukua muda nitamnasa, kisha nikamwambia likitokea lolote anijulishe.

Haikupita hata masaa 12 nikapigiwa simu na rafiki wa mpenzi wangu akinieleza tukio lililotokea huku akinisihi niende haraka, nami nikamwomba asimweleze mtu yeyote. Nikaenda na nikawafanya waseparate, kisha nikamwambia yule jamaa kuwa lengo lilikuwa kutaka kujua ukweli, kisha nikawatakia maisha mema.

Sikutaka watu wajue tukio lile kwa hofu kuwa wanaweza kusikia wazazi wa binti ikawa tatizo kwani sina mamlaka ya kumwekea wivu mtoto wao hence sio mke wangu pia itakuwa nimemdhalilisha binti yao.

Nimeandika kutaka kuomba ushauri, kwani nafsi bado inasita sana;

1. Je ni sahihi kumfanyia mke wako dawa ya namna hii?

2. Je huu si sawa na uchawi tu?

3. Je kwa kijana kumfanyia mkeo dawa ya namna hii si kuonesha kutojiamini na wivu?


MUHIMU: Nimeandika kwa urefu ili kutoa mwanga kwa kilichotokea ili nipate michango iliyopimwa kwa mazingira husika
 
hili tangazo naomba nilidhamini

hivi El Atachukua form lini na atairudisha lini
 
Jiamini mtoto wa kiume au kama vipi kaa na mkeo na umwambie kuwa umerudi na ulimbo ili yakimkuta asishangae utakua umemsaidia kujiandaa kwa kuweka vocha kwenye simu ili akichepuka akinasiana akupigie uje kumnasua
 
i always respect you. But today, nimekuona tofauti, sio mbaya sana, ndo uelewa wako umekomea hapo?

Nafikiri shida ni id yako mpya ungekuja na.ya zamani pengine asinge kujibu hivyo
 
i always respect you. But today, nimekuona tofauti, sio mbaya sana, ndo uelewa wako umekomea hapo?

Hili ni swali au maoni

anyways kwa nini unaniheshimu???? wakati siku zote coment zangu ndo kama hizi???
anyways hivi mkuu kweli HILI ULILOLIWEKA SIO TANGAZO KAMA SIO TANGAZO HILI NI NINI

kumbuka hapo juu umesema hujaoa hapo chini ukasema hivi ni mbaya kuitumia kwa mke
UMEOA KATIKATI YA KUANDIKA UZI???

hapo juu ukasema ulikua na msichana akakuuumiza ndo ukamueleza huyo babu ndo akakupa dawa
hapo chini ukasema nikarudi na nilivyorudi nikaamua kuijaribu kwa msichana wangu YAANI MMERUDIANA KATIKATI YA UZI hilo si swali swali ni kwamba ulikua unajua ana mahusiano na jamaa INA MAANA NDO YULE YULE WA MWANAZO AU NI NANI??? KAMA SIO WA MWANZO wewe kwanini wanawake wako wako hivi Kama kweli hii sio habari ya kufikirika

by the way hapo tena ukasema ukamtanwanya huyo manzi wako baada ya kumtawanya ukamwambia lolote litakolotokea nipigie sim HIVI UNAMDANGANYA NANI????? huyo demu wako akakujibu vipi na katika hali ya kawaida lazima ashangae

eti sijakaa muda napigiwa simu na rafiki yangu kwamba huku wamenasiana Ulimpanga saa ngapi na anyways umesema hukutaka watu wajue hivyo ulienda kuwanasua fasta NANI ALIMPIGIA SIMU RAFIKI YAKO?????? ina maana watu washajua?????? na kama sio watu(kama ulivyodai ukutaka watu wajue) basi ni mmoja wa wagoni wako alimpigia simu KWANINI ASIKUPIGIE WEWE???????
endelea ku imagne things


usiniheshimu am not looking for it SILIPI NAYO KODI YOYOTE HIYO HESHIMA YA JF
 
acha kutu "kidalipo" hapa ungekuwa na hyo dawa kweli ungepata mda wa kuandika humu ungesha wafanyia michepuko yooote
 
Compact Ltd

Mijitu mingine ni ovyo sana -kama yule jamaa aliyesema hajui kwa nini watz ni fukara
 
Last edited by a moderator:
Stori za kutunga hizi hamna kitu kama hicho.
 
jiamini mtoto wa kiume au kama vipi kaa na mkeo na umwambie kuwa umerudi na ulimbo ili yakimkuta asishangae utakua umemsaidia kujiandaa kwa kuweka vocha kwenye simu ili akichepuka akinasiana akupigie uje kumnasua
umeamua kutumia jina langu a zamani??????
 
Kifupi ni kua Jamaa anajitangaza kua anazo dawa za kunasiana hivyo mkizihitaji mumuendee PM
 
Back
Top Bottom