Ushauri: Roho inaniuma, nimezaa na mwanamke nisiyempenda. Bado anataka kuishi na mimi

Legendary!

Mwanaume "ubarikiwe" kupata mke anayekutii. Utajisikia kama Amiri Jeshi unayeamrisha Jeshi kubwa lenye nguvu kushinda kila vita. Kinyume chache jiandae kushindwa na mapambano ya Maisha. Bila mke anayekupenda na kukutii ujue kabisa hutoboiiii.
Pointi mkuuu mwambie uyo ,wanawake wa sasa sanaa tupu
 
Yatakurudia mateso anayopitia mwenzii sa iv mrudie na umlee mtoto wenu ao ndio ndugu zako wa ukweli...mwanamke aliekaa na ww kwny dhiki zako zte na akakuvumilia cha zaidi akakuzalia uyo ndo mkeo ...usifanye uharibifu kwny maisha ya uyo dada mpende na umpendezeshe uone utampenda ka ao wa nje
 
Yatakurudia mateso anayopitia mwenzii sa iv mrudie na umlee mtoto wenu ao ndio ndugu zako wa ukweli...mwanamke aliekaa na ww kwny dhiki zako zte na akakuvumilia cha zaidi akakuzalia uyo ndo mkeo ...usifanye uharibifu kwny maisha ya uyo dada mpende na umpendezeshe uone utampenda ka ao wa nje
Hata sasa napata mateso makubwa, sasa ni mateso gani zaidi ya haya ambayo naweza kuyapata?
 
Habari wadau! Katika mihangaiko ya hapa na pale kuna binti nilimkuta mahali, kifupi nikamtamani na nikataka nipite tu.

Baada ya mbinu za hapa na pale, alinipa namba na tukajikuta penzini, baada ya mawasiliano ya kama wiki, nilimwambia aje home.. nilitaka kula mzigo akabana na mimi kulazimisha huwa siwezi na ukizingatia sikumuelewa kabisa ikabidi nimpotezee mazima.

Suala la kutompenda halina shida ila sio poa kumtukana kimaumbile etu ‘’ Kifupi’’
 
Nakushauri yafuatayo.
1.Mtunze mtoto wako na hakikisha anakaa vizuri, mpatie mahitaji na mkatie bima ya afya ili usisumbuliwa kila wakati anapoumwa.

2. Tumia akili unapotafuta mke, usitumie hisia na moyo. Ukitumia hisia ukaoa baadaye ukiwa naye ukiona upungufu ndipo akili yako itafanya kazi utajua kuwa ulikosea. Na hilo ndilo lililokutokea ukampa mtoto wa watu mimba maana ulimtamani na ukafanya nae ngono zembe ili hali akili yako ilimkataa.

3. Acha tamaa ya kutaka penzi la haraka itakuharibia maisha yako inaelekea unapenda sana mashepu mkuu,, hahaha nakutania mkuu.
 
Roho mbaya, kutokujali hisia za mwenzio na ubinafsi vimekujaa mkuu. Unaweza vipi kumuita mtu usiempenda muishi pamoja kwa manufaa yako kibiashara.

Hukufanya vyema mkuu ungemkataa toka mwanzo tu, ushampa usingle maza na si ajabu wewe ni mmoja kati ya wanaopa kwa miungu wote kua hawawezi kuoa single maza.
 
Ila wanaume kama humpendi mtu kwanini umtongoze kwanini uamshe hisia za mapenzi kwenye moyo wake then baadae unamuacha ateseke it's very sad acheni kuplay na hisia za watu jamani
 
Habari wadau! Katika mihangaiko ya hapa na pale kuna binti nilimkuta mahali, kifupi nikamtamani na nikataka nipite tu.

Baada ya mbinu za hapa na pale, alinipa namba na tukajikuta penzini, baada ya mawasiliano ya kama wiki, nilimwambia aje home.. nilitaka kula mzigo akabana na mimi kulazimisha huwa siwezi na ukizingatia sikumuelewa kabisa ikabidi nimpotezee mazima.

Yule binti baada ya hapo hakukata tamaa aliendelea kunitafuta mara kwa mara, kila mara alikuwa akianza yeye, pamoja na kumchunia kote hakukata tamaa na kipindi hicho alikuwa hayupo tena mkoa niliokuwepo.

Muda ulienda ikapita kama miaka miwili, mimi juhudi zangu za kupata mwenzi zikawa zinagonga mwamba, kuna wakati uchumi wangu uliyumba sana na kwa vyovyote nilikuwa nahitaji mtu wa kusimamia shughuli zangu ili mimi nipambane kivingine.

Huyu binti nilimpanga nianze kuishi naye akakubali, hapo kiukweli moyo haukuwepo kabisa kwake, kilichonivuta kwake ni ule uvumilivu na kutoomba hela kabisa. Nikajipa moyo pengine nitampenda nikianza kuishi naye.

Baada ya kama miezi mitatu, alipata ujauzito na mimi mambo yangu angalau yakaanza kwenda mbele. Hapo kuna mwanamke wangu ambaye alikuwa bado A level nilikuwa nachatt naye bado. Kuna siku alikuta sms, akatishia kuondoka akafunga mpaka mabegi, nikaona isiwe kesi nikaomba msamaha nikaita mpaka mtu akaniombea msamaha maisha yakaendelea.

Wakuu kuishi na mtu usie na hisia naye ni kazi sana, nikawa naona yote nafanya kumfurahisha yeye tu, kweli ananipenda sawa lakini kwangu je? Nitajidanganya mpaka lini, nikawa nawaza sana hivi huyu kweli ndo wa kufa na kuzikana? Kifupi sikuwahi kuwa proud na yeye hata siku moja, mapenzi yakageuka mateso bila chuki, hakuna kitu kigumu kama unalala na kuamka na mtu ambaye humpendi na wala huna hisia naye.

Miezi ilienda mimba ikawa kubwa ikabidi arudi kwao kujifungua, hapo kwao hawanifahamu zaidi ya kuwasiliana na dada ake. Miezi ilienda akajifungua mtoto wa kike, copy yangu kabisa..furaha yake ilikuwa kubwa ila mimi kwangu ilikuwa tofauti nikawa nawaza sana hatma yetu.

Ilipita miezi kadhaa nikawafuata wakarudi nyumbani, hapo furaha sina najilazimisha tu. Mwanamke naye akaanza visirani vya hapa na pale, tatizo dogo mara atishie kurudi kwao, mara naenda lini kujitambulisha (moyoni nikawa najisemea huyu angejua).

Basi kuna siku katika pita pita huko mtaani kuna binti nikapata namba yake nikaanza kumtongoza kwa kutumia kisimu kidogo, sms inbox nikawa nafuta dah kumbe nilisahau kusett sent item zijifute, basi kwenye pekua pekua yake akakuta zile sms, akalia sana mara mimi nataka kumuua sijui mtoto mdogo n maneno mengine mengi sana.(kifupi toka nimekuwa naye sikuwahi chepuka kabisa). Basi baada ya hapo minuno ikaanza, nikijaribu kujirudi anakaza, nikasema poa isiwe shida.

Siku moja niliamka asubuh, sikumsemesha kitu akaweka maji bafuni sikuoga wala chai aliyoandaa sikunywa nikaondoka zangu, baadaye akatuma sms kwa haya maisha yamemchosha nikamwambia sawa, akataka nauli na mtaji. Nikamwambia mm nina nauli tu, akasema bila mtaji haondoki nikamwambia nauli hiyo hapo, ukiondoka sawa usipoondoka sawa ni wewe.

Kweli akakusanya mazaga yake, asubuh nikawapeleka ubt, wakaondoka. Niseme tu ukweli siku hiyo nilijihisi kutua mzigo mzito sana, nafsi ikawa nyeupe sana, japo nilijua nilimkosea na kumpotezea muda lakini ningefanyeje.

Sasa baada ya kuondoka haikupita hata wiki akaanza kuomba kurudi na kuomba msamaha sana. Kiukweli mimi sikuwa tayari, niligoma na sasa ni mwaka umepita tangu aondoke, kifupi bado sijapata mwanamke wa kueleweka atakayetuliza moyo wangu, kwenye hili wala sina haraka najipa moyo nitampata tu hata kama nitatumia miaka kumpata.

Sasa changamoto inakuja huyu mama wa mtoto wangu, bado hajakata tamaa mpka leo anaamini atarudi kwangu, kumwambia ukweli kwamba simpendi naona itamuumiza sana na hii sioni kama ni option nzuri.

Kwa wazoefu wa mambo, nitumie njia gani kumfanya huyu mwanamke aendelee na maisha yake, najua anadeserve furaha na kupendwa, but kwangu hivyo havipo na kamwe hatakuja kuvipata. Je nitumie njia gani kumuweka ajue kwamba hana nafasi kwenye maisha yangu.
Kijana kumbuka misemo ya wahenga, mpende akupendae, ipo siku utakuja kumkumbuka, wakuu humu wana msemo wao kuwa husipende kutumia kichwa cha chini kwenye maamuzi yako tumia kichwa cha juu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom