Mkuu mbona hii si kitu ya ajabu?Marubani "deiwaka" wapo kuanzia Dsm,Znz na nchi zote zilizoendelea.Hii kitu mbona ya kawaida sana tu.Mkuu @siambini yupo sahihi kabisaaa,vijana wengi sana wa Kizanzibar wapo nchi za Oman na UAE kama marubani baada ya huku kwetu kukosa kazi.
Kuwa rubani "deiwaka" ni kitu ya kawaida sana...Hawa huitwa "Freelencer Pilots",kwa mfano kwenye hiyo picha unayemuona ni mmoja kati ya marubani wazoefu na mahiri sana Tanzania toka enzi za Mwalimu Nyerere,anaitwa Captain Aziz,ni kaka yake na Dr Liki Abdalah yule mchambuzi wa mpira.
Huyu Captain Aziz alianzia ATC,lilipopoteza muelekeo akachukuliwa na kampuni ya Coastal Aviation inayopeleka watalii mbugani kwa wingi,pale akawa kama Chief Pilot,baadaye akastaafu.Sasa anaruka kama "deiwaka".....Freelencer Pilot!!Hapo alimpeleka Maalim Seif Znz toka Dsm,huyo nyuma yake ni mtoto wake anayetaka kumrithisha kazi ya urubani,kwa hiyo anaruka nae,baba akiwa kushoto basi dogo anakuwa kulia.Wakiwa juu basi dogo anaachiwa "usukani" anafanya yake,mpaka baba astaafu kabisa basi kazi itakuwa kwa dogo.Huyu ni freelencer pilot,au neno "deiwaka" ndio limekuchanganya!????Sasa Captain Aziz anaruka na ndege ya kampuni ya Jambo Aviation kama "Deiwaka"....Aliwahi nipa lifti toka Lindi kuja Dsm wakati wa kutafuta wadhamini wa Uchaguzi ndani ya CCM,hii ndege ilitumiwa na Membe baadhi ya sehemu kutafuta wadhamini
View attachment 378420