USHAURI PLEASE:NINUSURU UHAI AU NIMWACHE ATOE MIMBa

USHAURI PLEASE:NINUSURU UHAI AU NIMWACHE ATOE MIMBa

Ukweli siku zote ni uhuru au umuweka mtu huru...

Kuukubali huo ujauzito hakutabadili ukweli kuwa huyu bi mkubwa kabeba kiumbe cha mtu mwingine...

Mara nyingi mimba zisizotarajiwa huwa
zinabebwa hatiani, yaani tamaa ya pombe
na kujirusha ndio iliyopelekea haya yote...

Kwa lugha nyepesi ni kuwa tamaa zake za pombe na kujirusha ndio chanzo cha haya yote na zaidi ya yote pengine hata umedanganywa namna nzima ya mazingira yaliyopelekea ujauzito...

Mimi nakushauri jambo moja usibebe mizigo isiyokuhusu, kama ni nafasi yako kama rafiki umeshaifanya kwa kumuhusia asitoe ujauzito...
 
Kila siku natamani nikae na wasichana nizungumze nao waache hii tabia..wanashindwa kujiamini,aisee basi tu.
maswala ya dini hayahusiani na malezi ya mtoto.wanaweza hata kufunga ndoa ya bomani/serikali na kila mtu akaendelea na dini yake.mtu hamtaki alafu vinywaji vyake anakunywa.kwastahili hiyo atakuletea watoto wengi akitaka uwebaba yao kisa aliwatafuta akiwa amelewa.au atatoa mimba nyingi sana.na inaonyesha ni mzoefu sana wa hilo.mda mwengine na waza wanawake wanaotoa mimba nawao wafe hapohapo(mungu anisamehe kwa mawazo yangu mabaya) wanashidwa kujiuliza wao wangetolewa na mama zao wangekuwepo??dahhhh kuna watu wanahangaika usiku na mchana kutafuta watoto alafu wao bila aibu wanataka kutoa...na akiitoa hiyo mimba asizae teeeenaaaaaa..alaaaaa
 
Duh!pagumu hapo.mwambie huyo dada alee mimba asitoe,so lazma aish na huyo kaka bt wanaweza kusaidiana kumlea mtoto.ameshapata dhambi ya kuzini,kuua tena aue!asifanye hvyo.akumbuke kuwa si kila mtoto kalelewa na wazaz wote hata yy anaweza peke yake
 
Kubali tu kunusuru uhai wa hicho kiumbe kisicho na hatia....mungu atakulipa kwa wema wako....

Kuzaa si kupata kupata majaaliwa....anaweza akakufaa huyo mtoto kuliko mtoto wako mwenyewe...
 
A cha ufala, kama mimba haikuhusu utakubali vipi kwamba mimba ni yako. Au huna uzazi mkuu anataka ufichiepo mi aibu yako
 
Yaani Pure Mathematics unashindwa kukokotoa hiyo? Kwani wewe uko tayari kuoa sasa hivi? na uko tayari kumuoa huyo msichana? Kama majibu ya hayo maswali ni ndio basi jambo la kwanza inabidi iwe ni mipango ya kutambulishana kwa wazazi na kufunga ndoa na sio suala la kwenda kutambulishwa kwamba ni mtu aliyempa binti yao ujauzito.

Baada ya hapo mambo ya baba halisi wa mtoto mtajua wenyewe baada ya kufunga ndoa kwa kuwa tayari utakua unaishi na mkeo na hakuna cha binti kuogopa aibu ya ndugu zake.

Swali ni kwamba, uko tayari kuchukua jukumu na kuwa baba wa hiari kwa mtoto ambae unajua fika kwamba si wako?
 
Last edited by a moderator:
Kwa lugha nyepesi ni kuwa tamaa zake za pombe na kujirusha ndio chanzo cha haya yote na zaidi ya yote pengine hata umedanywa namna nzima ya mazingira yaliyopelekea ujauzito...

...

Huyo huyo binti wa aina hiyo anaogopa kuiaibisha familia kwa huo ujauzito!
 
pole brother kwa yote na hongera kwa kujaribu kutetea uhai wa kijacho. nimejifunza mambo 2
1. binti anakupenda (anakukubali) ww kuliko jamaa mhusika wa mimba, kosa lake ni kuendelea kuwa na ukaribu na mtu ambaye anajua kabisa hampendi.
2. hana hofu ya MUNGU kabisa, muombee na usikubali ubebe mzigo usiokuhusu kwan utakutesa na kuharibu future yako, kama kwel unataka kuokoa maisha ya mtoto bas muombee na weka wazi mipango yake kwa ndugu zake wa karibu hasa wazazi na mlolongo mzima wa tukio ulivyokua watamuelewa tu.
"usishiriki dhambi ya uongo itakugharimu"
 
Mkuu pole sana kuukubali ujauzito ni jambo gumu. Endelea kumsihi huyo binti asiabort kwani aweza asipate mtoto maisha yake yote. Hebu jiulize huyo dada anaona aibu ipi je kwenda klabu au kulewa au kupata ujauzito. Hapo kosa ni kwenda klabu na mtu usiyempenda sasa alitegemea nini. Hata hivyo yaliyopita si ndwele mshauri alee ujauzito na atafute namna ya kuwaeleza wazazi wake asikutishie habari ya aibu. Uamuzi ni wake ili mradi utakua umemshauri vema si lazima afuate ushauri wako.
 
Kwanzia mwanzo niliespect kuna sehemu una interest na haka kabinti,not bad kwa kuwa wewe ni mwanaume....
Kuna mambo mawili matatu ambayo hayaingii akilini kwa wepesi:-
-Kuoga,kujipulizia perfume,kutupia nguo za disco na vikorombwezo vyake...
-Kuungana na ''boyfriend asiyempenda'' kwenda disco...
-Kunywa alcohol ''kwa espectation za kutolewa''....
-Kupelekwa wherever,kupata mimba!
-Kuja kukaa na ''wewe rafiki usiyekuwa wa kimapenzi'' akakusimulia
-Ukamuonea huruma na unataka tukushauri hapa ...ok!

Sikia...

-Wanaume tunadhani tuna akili sana simply kwa kuwa tunavaa suruali,kuongea sauti nzito,na hutu tuhadidhi twa kichwa cha familia lakini ukweli ni kwamba mabinti wamejaaliwa akili ya pekee na ndiyo maana wao ndiyo wanaoendesha dunia (quote me)
-Sina sababu ya kuamini wala kutokuamini hii ngonjera ya huyu binti lakini nataka niku allert kwamba huenda ameshaona udhaifu wako na kwa kuwa anajua alikopatia mimba yenyewe hakueleweki ndiyo maana akakutunuku wewe!

Faida za kukubali hii zawadi ni kwamba utakuwa umeokoa kiumbe kama Mungu hatapitisha lake na hivyo ''ukarimu wako'' utakuwa umeongeza mdau mmoja wa kuvuta oxygen na kuexost Co2 ili kukuza uoto duniani!

Hasara za hii kitu ni kwamba kwa kuwa anatambua udhaifu wako basi tegemea kulea watoto wa wenzako kwa kuletea soft reason hadi uote mvi!
 
mkuu sijamshauri atoe mimba ila yeye amenipa condition nikubali akiulizwa baba wa mtoto aseme ni mimi, otherwise hayupo tayari kumtambulisha aliempa mimba, so ataitoa

Naona Kama Huyo dem anakuchezea akili yako? Yani usipo kubali ataitoa? Ukijafatwa na wazazi kutaka child support utasemaje ulikua unatania au? Usijipe majukumu hadji yalazima Kama wako kubali Huyo muachie mwenyewe ....
 
Embu tumia sifa la jina lako. Kokotoa mahesabu hayo. Ila kuna uwalakini fulani kati ya mazingira ya upatikanaji we ujauzito na ukaribu baina yenu. Haiingii akilini kwa rafiki tu aje akwambie akutambulishwe kama ndiye mwenye kiumbe ilhali hauhusiki. Yaweza ikawa umeficha kitu na unataka kuukataa ujauzito sababu hujui kama ni wako au la
 
Asilimia zaidi ya 50 ya wanawake wa miaka hii walishatoa mimba enzi za ujana wao au wakiwa ndani ya ndoa. So huyo hatakuwa wa kwanza. Na sheria za nchi hii zilishalegea kabisa kwenye adhabu za utoaji mimba.
 
Wewe huna mpenzi/ mke?
Akisikia haya itakuwaje???
Atakuelewa kuwa anataka anusuru uhai!
Na mtadanganya umma hadi lini?
Mtoto akikua mtaendelea kumdanganya?

Mwambie huyo binti haijalishi baba wa mtoto ni nani, ukweli utamweka huru

Ila kama unapigwa changa la macho vile.....
 
Mbali na moyo wako coz unaweza kukudanganya,akili yako inakuambia nini?
 
Kuna suala la ukweli na uhalisia ma sidhan kama ni rahisi kuficha ukweli na ni ngumu kutokuwepo na uhalisia. Inawezekanaje utoke out na mtu ambaye kwako hayuko moyoni? Yawezekana alikunywa pombe za ulafi mwisho wa siku akakubaliana na kila kitu then anajutia hatua zake.
Cha msingi kama ulikuwa/unahitaji kumgegeda na una mhitaji ktk maisha yako basi beba mzigo maana haiwezekani mtu alete mzigo kwako pasipo kuwepo na nia na uhalisia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom