Mimi ni mtumishi wa serikari,nina mkopo nmb ambao natarajia kuumaliza mwaka 2017,zaidi naomba kujua kama naweza kuomba mkopo benki nyingine.
Duhh,mkopo juu ya mkopo?
We umekopa na deni linaisha 2017 which means umekopa juzi tu hapa,then unakopa tena.
Mkuu madeni kwa bank kwa mfumo huo ni kujitia umaskini.
Wazungu wanasema jikune pale mkono unapofikia,usipofikia basi tafuta ukutwa ujikune kama mbuzi.
Uwezekano wa kukopa unategemea na mambo yafuatayo.
1. Kama benki mpya inaweza kununua deni lako NMB. Kaongee nao uwaeleze kuhusu mkopo wa sasa.
2. Kama unaweza kufuta mkopo wa sasa kwa kurudisha benki hela wanazokudai
3. Endapo una salio la kutosha kwenye mshahara wako, hujafikia 1/3 ya mshahara.
4. Unaweza pia kuongea na NMB wakupe top up.
Msaada namba 2, hapo utarudisha hela kama zinavyosoma kwenye deni husika au kutakuwa na punguzo kwa kulipa kwa mkupuo?
Unaporudisha balance kama inavyosomeka kwa wakati huo interest inakufa. Mabenki yetu huwa yanatengeneza schedule inayoonesha malipo ya kila mwezi na interest yake. Kwa hiyo ukifuta deni na interest iliyobaki inafutwa. Hii strategy huwa inasaidia sana kupunguza cummulative interest ambayo mabenki yetu yanatoza.
Mkuu hili ni kwa benki zote hapa nchini au?
Mkuu umenikumbusha mwalimu wang wa economics sio kuwa namaanisha na wewe una lengo hilo hapa bali alisema benk zina shida sana ilkuwa kweny ishu za credit creation bank moja inatoa mkopo alaf mkopaji anakula pesa zote then anaenda kukopa kwingne kiasi cha juu kidogo af anakuja kulpa tena na mchezo unakua huohuo life linaenda