Jamani wana JF,
Naomba mnisaidie hata ushauri tu, sijui nimelogwa au ni upendo tu maana hii experience sijawahi kabisa kuwa nayo tangu nizaliwe.
Mimi ni kijana mwenye miaka 25 nilikua na mpenzi wangu (25 yrs) tuliekuwa tunapendana sana tena sana na tumeishi kwa mwaka mmoja sasa kwa malengo ya kumuoa, japo aliolewa na akakaa kwenye ndoa kwa miaka minne kabla ya kuwa na mimi na akaachika na ameshazaa mtoto mmoja mwenye miaka minne.
Shida imekuja nilipotoka na kuhamia sehemu nyingine kikazi nae akaenda kwao, ghafla mawasiliano yalipungua ikawa ugomvi hauishi na ni kwasababu amebadilika sio kama zamani.
Nimevumilia yote hayo lakini mwisho wa siku akanidhihirishia wazi kuwa anamtu baada ya kumuweka profile picture WhatsApp na kunitamkia kabisa kuwa huyo ndo mpenzi wake wa sasa na ndio aliemnunulia smartphone na nisimsumbue hawezi kurudiana na mimi.
Sikumuacha ila tulikosana kwa wiki moja tu ndo tukkaliana kimya baada ya kumpigia simu usiku simu ikawa busy akaniambia namsumbua anataka kulala na kunikatia simu siku hiyo, najitahidi kuizoea hali lakini nashindwa kabisa.
Mpaka nimemwambia kama alipitiwa akafanya hivyo basi haina shida tuanze upya lakini kasema mwili wake hawezi kuwapa watu wawili na ameshafanya nae mapenzi zaidi ya mara mbili na kasema nifute malengo yote kichwani mwangu na hana mpango wa kuolewa wala kutolewa posa kwa sasa (ilhali nilipanga kwenda kwao kujitambulisha mwezi wa 11).
Nilimzoea sana na sababu ya kuniacha hata haieleweki, wengine anawaambia simjali kifedha, wengine anawaambia mimi sijatulia, mimi ananikumbushia SMS za zamani na ugomvi wa zamani ambao tulishausolve eti ndo umesababisha.
Nifanye nini wanaJF maana hafutiki kichwani kabisa.
Naomba mnisaidie hata ushauri tu, sijui nimelogwa au ni upendo tu maana hii experience sijawahi kabisa kuwa nayo tangu nizaliwe.
Mimi ni kijana mwenye miaka 25 nilikua na mpenzi wangu (25 yrs) tuliekuwa tunapendana sana tena sana na tumeishi kwa mwaka mmoja sasa kwa malengo ya kumuoa, japo aliolewa na akakaa kwenye ndoa kwa miaka minne kabla ya kuwa na mimi na akaachika na ameshazaa mtoto mmoja mwenye miaka minne.
Shida imekuja nilipotoka na kuhamia sehemu nyingine kikazi nae akaenda kwao, ghafla mawasiliano yalipungua ikawa ugomvi hauishi na ni kwasababu amebadilika sio kama zamani.
Nimevumilia yote hayo lakini mwisho wa siku akanidhihirishia wazi kuwa anamtu baada ya kumuweka profile picture WhatsApp na kunitamkia kabisa kuwa huyo ndo mpenzi wake wa sasa na ndio aliemnunulia smartphone na nisimsumbue hawezi kurudiana na mimi.
Sikumuacha ila tulikosana kwa wiki moja tu ndo tukkaliana kimya baada ya kumpigia simu usiku simu ikawa busy akaniambia namsumbua anataka kulala na kunikatia simu siku hiyo, najitahidi kuizoea hali lakini nashindwa kabisa.
Mpaka nimemwambia kama alipitiwa akafanya hivyo basi haina shida tuanze upya lakini kasema mwili wake hawezi kuwapa watu wawili na ameshafanya nae mapenzi zaidi ya mara mbili na kasema nifute malengo yote kichwani mwangu na hana mpango wa kuolewa wala kutolewa posa kwa sasa (ilhali nilipanga kwenda kwao kujitambulisha mwezi wa 11).
Nilimzoea sana na sababu ya kuniacha hata haieleweki, wengine anawaambia simjali kifedha, wengine anawaambia mimi sijatulia, mimi ananikumbushia SMS za zamani na ugomvi wa zamani ambao tulishausolve eti ndo umesababisha.
Nifanye nini wanaJF maana hafutiki kichwani kabisa.