Ushauri: Nimelogwa au ni upendo?

Ushauri: Nimelogwa au ni upendo?

wenzako huwa wanabalance mioyo yao
50% - kupenda
50% - kutopenda
 
unahitaji ubongo mpya huo umeshaharibika kwa kansa ya ubongo
 
The same age dah! Pole kichwa cha chini kisikutese, kama wako atarudi.

Ila pesa nayo tafuta kuna kitu hakijakaa sawa mdogo wangu.
Dah! nilikumiss aisee mamy bora umerudi nahisi leo nitalala vizuri
 
Jamani wana JF,

Naomba mnisaidie hata ushauri tu, sijui nimelogwa au ni upendo tu maana hii experience sijawahi kabisa kuwa nayo tangu nizaliwe.

Mimi ni kijana mwenye miaka 25 nilikua na mpenzi wangu (25 yrs) tuliekuwa tunapendana sana tena sana na tumeishi kwa mwaka mmoja sasa kwa malengo ya kumuoa, japo aliolewa na akakaa kwenye ndoa kwa miaka minne kabla ya kuwa na mimi na akaachika na ameshazaa mtoto mmoja mwenye miaka minne.

Shida imekuja nilipotoka na kuhamia sehemu nyingine kikazi nae akaenda kwao, ghafla mawasiliano yalipungua ikawa ugomvi hauishi na ni kwasababu amebadilika sio kama zamani.

Nimevumilia yote hayo lakini mwisho wa siku akanidhihirishia wazi kuwa anamtu baada ya kumuweka profile picture WhatsApp na kunitamkia kabisa kuwa huyo ndo mpenzi wake wa sasa na ndio aliemnunulia smartphone na nisimsumbue hawezi kurudiana na mimi.

Sikumuacha ila tulikosana kwa wiki moja tu ndo tukkaliana kimya baada ya kumpigia simu usiku simu ikawa busy akaniambia namsumbua anataka kulala na kunikatia simu siku hiyo, najitahidi kuizoea hali lakini nashindwa kabisa.

Mpaka nimemwambia kama alipitiwa akafanya hivyo basi haina shida tuanze upya lakini kasema mwili wake hawezi kuwapa watu wawili na ameshafanya nae mapenzi zaidi ya mara mbili na kasema nifute malengo yote kichwani mwangu na hana mpango wa kuolewa wala kutolewa posa kwa sasa (ilhali nilipanga kwenda kwao kujitambulisha mwezi wa 11).

Nilimzoea sana na sababu ya kuniacha hata haieleweki, wengine anawaambia simjali kifedha, wengine anawaambia mimi sijatulia, mimi ananikumbushia SMS za zamani na ugomvi wa zamani ambao tulishausolve eti ndo umesababisha.

Nifanye nini wanaJF maana hafutiki kichwani kabisa.
Hakikisha kabla hujaingia kwenye mahusiano yoyote yale unatoa kwanza PHOTOCOPY ya moyo wako kisha ORIGINAL copy unaiacha nyumban.,Just in case
 
Ukiachwa achika, Japo ni ngumu ila jaribu kuangalia zaidi malengo yako ni nini? Jiulize kabla ya hapo uliishije? Jiweke busy kufanya mambo unayoyapenda sana
 
Jamani wana JF,

Naomba mnisaidie hata ushauri tu, sijui nimelogwa au ni upendo tu maana hii experience sijawahi kabisa kuwa nayo tangu nizaliwe.

Mimi ni kijana mwenye miaka 25 nilikua na mpenzi wangu (25 yrs) tuliekuwa tunapendana sana tena sana na tumeishi kwa mwaka mmoja sasa kwa malengo ya kumuoa, japo aliolewa na akakaa kwenye ndoa kwa miaka minne kabla ya kuwa na mimi na akaachika na ameshazaa mtoto mmoja mwenye miaka minne.

Shida imekuja nilipotoka na kuhamia sehemu nyingine kikazi nae akaenda kwao, ghafla mawasiliano yalipungua ikawa ugomvi hauishi na ni kwasababu amebadilika sio kama zamani.

Nimevumilia yote hayo lakini mwisho wa siku akanidhihirishia wazi kuwa anamtu baada ya kumuweka profile picture WhatsApp na kunitamkia kabisa kuwa huyo ndo mpenzi wake wa sasa na ndio aliemnunulia smartphone na nisimsumbue hawezi kurudiana na mimi.

Sikumuacha ila tulikosana kwa wiki moja tu ndo tukkaliana kimya baada ya kumpigia simu usiku simu ikawa busy akaniambia namsumbua anataka kulala na kunikatia simu siku hiyo, najitahidi kuizoea hali lakini nashindwa kabisa.

Mpaka nimemwambia kama alipitiwa akafanya hivyo basi haina shida tuanze upya lakini kasema mwili wake hawezi kuwapa watu wawili na ameshafanya nae mapenzi zaidi ya mara mbili na kasema nifute malengo yote kichwani mwangu na hana mpango wa kuolewa wala kutolewa posa kwa sasa (ilhali nilipanga kwenda kwao kujitambulisha mwezi wa 11).

Nilimzoea sana na sababu ya kuniacha hata haieleweki, wengine anawaambia simjali kifedha, wengine anawaambia mimi sijatulia, mimi ananikumbushia SMS za zamani na ugomvi wa zamani ambao tulishausolve eti ndo umesababisha.

Nifanye nini wanaJF maana hafutiki kichwani kabisa.
Pole sana kwa mkasa mambo ya wanawake inabidi uingie kwa akili sana.Huyo tayari hakupendi na mshukuru mungu kakuonesha mapema la sivyo ungeoa gaka ndani.Piga chini tafuta hela saiz 25 bado mdogo kijana wangu.
 
Mapenzi hayahitaji uwe serious.
Ni kamchezo flani tu.
Ni kamchezo ka moyo kanakohitaji akili.
Mambo ya true love washa tv uangalie kwenye ST Novela.

Hivyo move on, siyo tu kwa sababu ni vyema, bali kwa kuwa ndo hivyo yaani.
Usipoanza leo utaanza ukiwa tayari.
Pole kwa hayo maumivu. Na hayataisha leo ndugu.
 
Nadhani hujamuelewa jamaa. Hakumpenda kwa sababu ya papuchi, bali ni kqa sababu ya mapenz. Hivyo ni vitu viwili tofauti.

Kama lingekuwa suala la papuchi sidhan kama angeandika huu uzi maana ni suala rahis sana. Lakin hili ni suala la emotinal connection ambayo imevunjwa ghafla. Si rahi ku recover kama unavyodhani.
Mkuu umeongea kiutu uzima make humu kuna mapoyoyo daily wanajifanya wao wanaweza kuhandle kila stuation kumbe wapi.
Thanks nahis mhusika atajitahid kurecover japo ni ngumu kdg
 
Naomba mnisaidie hata ushauri tu, sijui nimelogwa au ni upendo tu maana hii experience sijawahi kabisa kuwa nayo tangu nizaliwe.




Ni udhaifu wako tu ujarogwa wala nini
 
Umemamaliza. Also asitafute kisasi or kufanya vitu kujarib kumuonyesha ni zaidi yake. Bali atulie aweke focus yake kwenye maisha sasa, kenye kupona moyo.

Huyo ex wake asimuwaze ila ajue tu kama always win at the end. Ukweli utajulikana tu na yatamtokea yakumtokea atakuja kwa machozi.
Kabisa tena ningekula nikashiba na uzito ningeongezeka asitafte visas wala aishi maisha yake
 
Honestly hiyo Hali ya kuwafanya wanaume wateseke kwenye mapenzi mm sijakutana nayo na siombei initokee mara zote nimekua nikiumiza wanawake sio kuumizwa japo siku hizi siwaumizi tena nimeshakua ila nilichokuja kugundua kwenye ukuaji wangu wanaume ambao huwa hawajali sana ndio hupendwa sana tofauti na wanaume wanaopenda sana kama mtoa mada, ngoja nikuambie ninavyofikiri huyo mwanamke anakutafsiri nadhani anakuona bwege bwege japo kilichokuponza ni upendo wako kwake mwanaume kupendwa ndio raha sio unakuja kulia Lia umerogwa hapa hamna kitu kama hicho mchawi akili yako wazungu wanasema it costs to be stupid the stupider you are the more it costs, anza kumtharau tena mtharau kweli kweli tafuta totow moja kali kushinda yeye ila kuwa makini usimpende sana be a player hit them as much as you can na akikuzingua kidogo achana nae kanyaga mwingine you are so young (ila kuwa makini na hilo mdogo wangu pesa na maradhi,) ukifanya hayo nina uhakika utaenjoy na utapata mke wa maisha yako achana na
I beleive huu ni ushauri mbaya, una mshauri jamaa awe player, remmber ukichagua kwenda njia hiyo there is no going back. Halaf kaka unashindwa kutofautisha kati ya mwanamke na msichana..
Mwanamke ambae unampenda yeye anakuona poyoyo huyo ni msichana .. why? Sababu anapenda kuwa abused, kutukanwa, kudharauliwa.. ndio anapata ile adrenaline rush na kusikia raha. Hiyo hali ni so addictive.
real woman in other hand hawapend kuwa abused, show them love nao watakupenda kama ulivyo.

The thing is jamaa anatakiwa awe na msimamo haswa. Yani ni O au 1. Dem akianza mizinguo piga chini instantly chukua mwingine. Dont cheat maana huo ni upotev wa muda na resource.

+ kama unachange tabia yako from good person to be a player, kuwa mbabe ,kuwa na roho mbaya ili tu umridhishe mwanamke basi utakuwa hauko na mtu sahihi.. mtu anaetaka kuwa nawe atavumilia mapungufu yako lakin si kukulazimisha.
 
Back
Top Bottom