Ushauri Ndugu Zangu!

Juuchini

JF-Expert Member
Dec 10, 2018
1,300
1,659
Mimi ni Daktari kitaaluma na ni mwenye kuzingatia maadili ya kazi yangu.
Tangu mwaka jana mwezi wa kumi na mbili nilipelekwa idara ya watu wenye maambukizi ya virusi vya UKIMWI.
Pamoja na huduma za kliniki pia idara hii pia inahusika na upimaji wa VVU kwa wale wateja wanaofika hospitalini hapa kwa ajili ya matibabu lakini hali za maambukizi hazijulikani (unknown HIV status).
Katika harakati za upimaji nikakutana na binti mmoja ambaye umri wa ni miaka kama ishirini na miwili.
Huyu tulipompima tukakuta ana maambukizi ya virusi vya UKIMWI.
Tukamfanyia ushauri nasaha na kumwanzisha tukiamini ametuelewa kumbe akachukua dawa halafu akaenda kuhifadhi ndani kwake. Ikapita tarehe ya kurudi, ikapita mwezi.
Siku mmoja nikiwa nakagua mafaili nikakuta namba zake nikampigia simu.
Nilipojitambulisha akakataa simu akatumia sms kuwa nimwache afe.
Baadae nikaendelea kutumiana nae meseji za kumshawishi atumie dawa lakini ananizungusha sana.
Jana aliniomba nimtembelee lakini
Nikashindwa kutokana na majukumu yangu
Leo pia akaniomba nimtembelee na bado nikakwama kutokana na kubanwa na majukumu.
Kilichonifanya niandike huu uzi ni kwamba amekuwa akilalamika sana kama vile tuko kwenye mahusiano.
Na anahisi mimi ninamnyanyapaa
Kisa ana maambukizi ya virusi vya UKIMWI.
Mimi ni mhubiri wa yale maneno kwamba "ukitumia dawa za ARV huwezi kuambukiza wengine" .
Lakini binafsi siamini kitu kama hicho.
Sasa wadau nifanye nini maana niko kwenye Ethical dillema.
Ushauri wenu jamani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumbe ndio huwa mnasema hivyo kuwa ukitumia ARV huambukizi wengine??

Hapo unataka ushauri kuhusu nini?anavyokulalamikia kama mpenzi wako?
Ama namna ya kumshawishi ameze dawa?
Akikujibu nitag

"Enough of No Love"
 
Braza tukushauri kwenge ipi ya kukutana nae au... Mshawishi akafanye viral load kwanza na kama kukutana nae ni kitu cha kawaida sana mnaweza mkakutana nae kabisa na yakubidi ukubali kuwa hawezi kukuambukiza kama ashaanza kutumia ARV japo hauamini ila ni hivo.


Sony mobile phone
 
Kumbe ndio huwa mnasema hivyo kuwa ukitumia ARV huambukizi wengine??

Hapo unataka ushauri kuhusu nini?anavyokulalamikia kama mpenzi wako?
Ama namna ya kumshawishi ameze dawa?
Boss tafiti zinaonyesha hivyo sio tu kusema ni kitu ambacho kimefanyiwa tafiti.
Sema tu ule uoga wa kibinadamu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Braza tukushauri kwenge ipi ya kukutana nae au... Mshawishi akafanye viral load kwanza na kama kukutana nae ni kitu cha kawaida sana mnaweza mkakutana nae kabisa na yakubidi ukubali kuwa hawezi kukuambukiza kama ashaanza kutumia ARV japo hauamini ila ni hivo.


Sony mobile phone
Hajawahi kutumia hata ile baseline CD4 count hafanya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aisee, ko unacho ogopa ni kukutana nae? na bahati mbaya huna uhakika kama alishaanza tumia dawa

Sony mobile phone
 
Mimi ni Daktari kitaaluma na ni mwenye kuzingatia maadili ya kazi yangu.
Tangu mwaka jana mwezi wa kumi na mbili nilipelekwa idara ya watu wenye maambukizi ya virusi vya UKIMWI.
Pamoja na huduma za kliniki pia idara hii pia inahusika na upimaji wa VVU kwa wale wateja wanaofika hospitalini hapa kwa ajili ya matibabu lakini hali za maambukizi hazijulikani (unknown HIV status).
Katika harakati za upimaji nikakutana na binti mmoja ambaye umri wa ni miaka kama ishirini na miwili.
Huyu tulipompima tukakuta ana maambukizi ya virusi vya UKIMWI.
Tukamfanyia ushauri nasaha na kumwanzisha tukiamini ametuelewa kumbe akachukua dawa halafu akaenda kuhifadhi ndani kwake. Ikapita tarehe ya kurudi, ikapita mwezi.
Siku mmoja nikiwa nakagua mafaili nikakuta namba zake nikampigia simu.
Nilipojitambulisha akakataa simu akatumia sms kuwa nimwache afe.
Baadae nikaendelea kutumiana nae meseji za kumshawishi atumie dawa lakini ananizungusha sana.
Jana aliniomba nimtembelee lakini
Nikashindwa kutokana na majukumu yangu
Leo pia akaniomba nimtembelee na bado nikakwama kutokana na kubanwa na majukumu.
Kilichonifanya niandike huu uzi ni kwamba amekuwa akilalamika sana kama vile tuko kwenye mahusiano.
Na anahisi mimi ninamnyanyapaa
Kisa ana maambukizi ya virusi vya UKIMWI.
Mimi ni mhubiri wa yale maneno kwamba "ukitumia dawa za ARV huwezi kuambukiza wengine" .
Lakini binafsi siamini kitu kama hicho.
Sasa wadau nifanye nini maana niko kwenye Ethical dillema.
Ushauri wenu jamani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Da mbona unatuabisha ww, daktar gan sasa. Huamn kwamba matumiz ya ARV yanapunguza mambukizi?. Inamana huwamin pia WHO, statistic ya mambukiz sasa na zaman unaona sawa na kama yamepungua reason n nini?
Daktar kama husomi ni kazi bure.
Ningekuwa na mda ningekuwekea hata References.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Da mbona unatuabisha ww, daktar gan sasa. Huamn kwamba matumiz ya ARV yanapunguza mambukizi?. Inamana huwamin pia WHO, statistic ya mambukiz sasa na zaman unaona sawa na kama yamepungua reason n nini?
Daktar kama husomi ni kazi bure.
Ningekuwa na mda ningekuwekea hata References.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ninao couple kadhaa ambao wako na discordant results ila huwezi kukosa uoga wa kibinadamu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom