Kama huna elimu ya computer inawezekana lakini itakuchukua muda zaidi, cha muhimu sana ni uwezo wako wa reasoning. Computer science ni broad sana, vipo ambavyo vinahitaji mtu anayejua hesabu, vipo ambavyo mtu yeyote anaweza, mfano, mtu ambaye anataka kufanya web designing ya front end, simple mobile applications, kama unajua algebra za kawaida unaweza fanya bila shida, backend pia software nyepesi nyepesi hazitokusumbua. Ila unapokuja vitu kama data mining mfano kujaribu kufanya computer mfano itambue tofauti kati ya spam mail na good emails lazima hesabu zikae kichwani, ukitaka kutengeneza drone ipae e.t.c
So cha muhimu sio kama umegusa computer before, cha muhimu jiangalie kwanza uko strong kwenye field gani, hasa za science mfano hesabu, phyics, chemistry, biology then chagua part fulani ya computer science ambayo angalau utaweza kuapply mambo unayoyafahamu, komaa hadi kieleweke.