Ushauri na msaada

Ushauri na msaada

njumu za kosovo

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2017
Posts
4,852
Reaction score
11,723
Umuofia kwenu,

Nina kakibanda kangu huko mjini Kerege sasa wakati napiga gharama mbali mbali nikajikuta mambo yamekua mengi na mzigo (pesa inakata) na wakati huo nilikua tayari nishalipia pesa za bati kiwandani, ila gharama za mbao zikazidi.

Baada ya kushauriana na fundi na kumueleza hali halisi akasema si tatizo sana katika mbao tutaongeza na miti jamii ya mirunda ile kupaulia ili kupunguza gharama na bahati nzuri akanionyesha na nyumba alizotumia miti huwezi amini.

Lakini wakurungwa mnanishauri vipi hapo, maana nikiangalia kweli niko tight?
 
Badili mwonekano wa paa lako, au tumia mbao za iringa zina gharama ndogo, option ingine tumia mbao ndogo ama.nunua 2kwa6 zichanwe na 2kwa 4 zichanwe
 
Tafuta hela ya mbao mkuu, fundi siyo wa kumsikiliza sana yeye huwa anataka apate kazi tu ili mambo yake yaende atakulazimisha uripueripue kazi maana ukisubiria yeye atakosa hela kitakacho kuja kukukuta mbele inakua ni hasara yako
 
Umuofia kwenu,

Nina kakibanda kangu huko mjini Kerege sasa wakati napiga gharama mbali mbali nikajikuta mambo yamekua mengi na mzigo (pesa inakata) na wakati huo nilikua tayari nishalipia pesa za bati kiwandani, ila gharama za mbao zikazidi.

Baada ya kushauriana na fundi na kumueleza hali halisi akasema si tatizo sana katika mbao tutaongeza na miti jamii ya mirunda ile kupaulia ili kupunguza gharama na bahati nzuri akanionyesha na nyumba alizotumia miti huwezi amini.

Lakini wakurungwa mnanishauri vipi hapo, maana nikiangalia kweli niko tight?
Kumbe kerege sahivi ni mjini
 
Hebu naomba uzoefu wako kidogo mkuu mana nimebakiwa kama na siku mbili za kufanya maamuzi
fata ushauri comment #4 hapo,
fundi anajiangalia yeye apate kazi chap umlipe afanye issue zake
achana na ushauri wake, jichange taratib weka mbao,

nb: usisahau kupaka oil chafu kama unamjua DUMUZI
 
Back
Top Bottom