Kazi nyingi ngumu ngumu za suluba za hatari ufanywa na wageni mfano mashambani, kuchunga na kulisha mifugo, kukata mbao, udereva wa masafa, kusafisha ma kreni, Kazi za kuning'ia juu, usafi, ulezi,kubeba box, derivery yaani kutumwa usambaze vitu, nk malipo ni kwa masaa unajumlishiwa unapewa kwa wiki, au kama ni deiwaka unalipwa baada ya kazi inategemea kuanzia dola 10 kwa saa. Watz wengi awafanikiwi nje hawana malengo wakifika nje wao ni kufungua zipu na chupa tu.
Kazi ya udereva ni nzuri unalipwa kwa maili plus uzoefu na masaa ukiwa skilled unauzoefu unaenda kwa wauza matruck unalipa kwa Mkopo unamiliki truck kwa mwezi unaingiza dollar elf 10.
Nje msingi wako mkuu ni uaminifu ,bidii na uvumilivu hivi vitatu ndo siri ya kutajirika nje. Kikubwa Sana cha kuweka kichwani mwako nchi usitafute shortcut au mambo ya illegal illegal tii sheria na toa ushirikiano, ukileta ubongo utapigwa patration to bongo.