Ushauri: Mwanaume hapendi kunisaidia

Ushauri: Mwanaume hapendi kunisaidia

shushushu_mchokozi

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2016
Posts
405
Reaction score
265
Bahari za leo ndugu zangu,

Naombeni ushauri ndugu zangu,

Naona hili jambo kama linaniweka njia panda vile. Nina mwanaume mmoja ni rafiki yangu kimapenzi, ila tatizo lake kubwa ni kwamba hajui kusaidia na ikitokea nikawa na shida nikamuomba jambo kapesa kidogo yeye hanipi ila anasema tu mimi ukizaa na mimi ndio nitakupa hela.

Ndugu zangu huyu naona hanifai hata kidogo.

USHAURI WENU WAPENDWA
 
Umeisha khitimisha kuwa hakufai sasa hapo ushauri gani unautaka? nadhani umejipima na kuona hakuna future na huyo bwana kwa mujibu wa maelezo yako endelea mbele.
 
Na kweli hakufai jata kidogo, hata ukizaa naye jataweza kutoa msaada, atakuambia mapaka umzalie watoto watano. Piga chini huyo.
 
Mantiki ya neno ukizaa na yeye ni kipimo tu cha kutaka kujua mustakabali wa penzi lenu je upo tayari kuwa na yeye. Sio awe anakugharamikia kwa kila kitu halafu kumbe wewe una malengo yako binafsi baadae ukamuacha njia panda na kumkimbia.

Jamaa anaonekana historia yake ameshaumizwa sana mpaka hana imani na wewe mpaka umkubalie kumzalia ili hata ukimuacha ataendelea kuwa na mwanae. Hakuna haja ya yeye kupoteza pesa zaidi kama wewe huna muelekeo kuna baadhi ya ishara ameziona kutoka kwako na hakuelewi elewi msimamo wako ndo maana hataki kuingia kichwa kichwa
 
Mantiki ya neno ukizaa na yeye ni kipimo tu cha kutaka kujua mustakabali wa penzi lenu je upo tayari kuwa na yeye. Sio awe anakugharamikia kwa kila kitu halafu kumbe wewe una malengo yako binafsi baadae ukamuacha njia panda na kumkimbia.

Jamaa anaonekana historia yake ameshaumizwa sana mpaka hana imani na wewe mpaka umkubalie kumzalia ili hata ukimuacha ataendelea kuwa na mwanae. Hakuna haja ya yeye kupoteza pesa zaidi kama wewe huna muelekeo kuna baadhi ya ishara ameziona kutoka kwako na hakuelewi elewi msimamo wako ndo maana hataki kuingia kichwa kichwa

Hapa kuna ukweli kabisa

Maana na mimi nilishanitokeaga hivyo unampenda mtu kwa kila hali unamsaidia kwenye mambo yake mengi tu alafu mwisho wa siku unaitwa kaka wa msaada umegharamika weee mwisho wa siku anakuacha kama mzoga

nakubaliana na wewe kabisa
 
wewe huwa unamsaidia? pia ushasema hakufai unajuaje kama na yeye aishaona wewe haufai? yaani wewe nae humfai
 
Mmmh ila wanaume mmezidi jaman yaan mpka MTU umpe mimba ndio uwe na uhakika nae jaman jaman,je Dada zenu wakifanyiwa hivyo mtafurahi?
 
Hapo ukishabeba mimba story yako inaishia hapo, huna mimba hawez kukusaidia, ukishabeba ndio atakujali huyo anakutumia kwa starehe tu na Hana mapenz ya kwel mana mapenz ya kwel nikusaidiana katika shida na raha, nafikir ushasema hakufai hop Hilo ni wazo la moyo wako mana unambiwa sikiliza mashaur yote ila mwisho sikiliza moyo wako unasemaje kuhusiana na Hilo mana moyo hua haudanganyi
 
Hivi tunaingia kwenye mapenzi ili tuwe tunasaidia/kusaidiwa?
 
Kwenye blue ulimaanisha hivo? Any way, bila msaada wake kwako hamuwezi kuishi? Humpendi wewe na huo ndio mtego wake kwako


Bahari za leo ndugu zangu,

Naombeni ushauri ndugu zangu,

Naona hili jambo kama linaniweka njia panda vile. Nina mwanaume mmoja ni rafiki yangu kimapenzi, ila tatizo lake kubwa ni kwamba hajui kusaidia na ikitokea nikawa na shida nikamuomba jambo kapesa kidogo yeye hanipi ila anasema tu mimi ukizaa na mimi ndio nitakupa hela.

Ndugu zangu huyu naona hanifai hata kidogo.

USHAURI WENU WAPENDWA
 
Back
Top Bottom