DR Mambo Jambo
JF-Expert Member
- May 10, 2012
- 12,622
- 28,459
Najua haiwezi kuwa Rahisi Hivyo ila ili Kuboresha uchumi wa nchi, kuongeza ajira, ufanisi, na maisha ya Watanzania kunahitaji mkakati mpana unaohusisha sekta mbalimbali. Hapa kuna ushauri na mapendekezo kwa serikali Ambao kwangu Nimeona Unafaa na Nitakuwa naweza na Fedha kwa Makadirio ya Chini zitakazo okolewa..
Kwanza Kabisa Ni kupunguza matumizi Yasiyokuwa ya Lazima
Tuanze kwa Kudhibiti safari za nje za viongozi wa serikali kwa kuhakikisha zinafanyika pale tu inapohitajika sana.Kwa mfano Waziri wa Tamisemi Kwenda Kujifunza Kuhusu Local Government Nchini Urusi ,Wakati angeweza Kutumiwa Doccuments za Analytical Jinsi ya Kuongoza Local Government..Kudhibiti mikutano ya serikali isiyo na tija na kutumia njia za kisasa kama mikutano ya mtandaoni (virtual meetings) ili kupunguza gharama za usafiri na posho.
Mfano:- Katika mwaka wa fedha 2022/2023, serikali ilitenga zaidi ya TZS 500 Bilioni kwa safari za kikazi za viongozi ndani na nje ya nchi..
Basi kama Kuna Ulazima Sana angalau Tupunguze Matumizi ya Safari za Viongozi kwa kupunguza Bajeti yake kwa 50% yaani Angalau Iwe Tsh 250 Bilion..
Pili Kupunguza matumizi ya magari ya kifahari serikalini na kutumia magari yenye gharama nafuu na yanayotumia mafuta kidogo..
Tutoke kwenye Bajeti ya Bilion 180 Kwa Mwaka Ya Magari na Uendeshaji Tufike mpaka kwenye Bilion 20 Hivi au 30 au Kama Kuna Ulazima Sana Angalau Bilion 50..
KUFUTA OFISI YA MKUU WA WILAYA NA KUGAWA MAJUKUMU KWA MKURUGENZI WA HALMASHAURI
Ikiwa lengo ni kupunguza gharama za serikali, kupunguza urasimu, na kuongeza ufanisi wa utendaji, basi Ofisi ya Mkuu wa Wilaya inaweza kufutwa na majukumu yake kuhamishiwa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri, Hata Hivyo tumeshuhudia Mara nyingi sana Ofusi ya Mkuu wa Wilaya Ikiwa na Migongano ya Mara kwa mara ya Kiutendaji na Mkurugenzi kwa sababu ya Muingiliano wa Kimajukumu
Na Kuhusu Majukumu ya mkuu wa Wilaya Yanaweza kugawiwa kama Ifuatavyo..
KUPUNGUZA IDADI YA MAJIMBO YA UBUNGE NA KUTUMIA HALMASHAURI KAMA MAJIMBO
Lengo letu si Kila mtu apate Keki ila Lengo ni kubana matumizi ya serikali na kupunguza gharama za uchaguzi na uendeshaji wa Bunge, basi hatua mojawapo ni kupunguza idadi ya majimbo ya uchaguzi na kutumia Halmashauri kama majimbo ya uchaguzi, Ili pesa Itakayobaki itumioe kwenye Bajeti ya Majukumu Mengine ambayo Yanahitajika sana..
Tanzania ina majimbo ya uchaguzi 264 (kwa mujibu wa uchaguzi wa 2020). Na pia Tanzania pia ina Halmashauri 184 (manispaa, wilaya, miji).
Hii ina maana kuwa kuna zaidi ya majimbo 80 ya ziada ambayo yanaongeza gharama za uchaguzi na mishahara ya wabunge, ambao wanafanya kazi sawa kabisa..
Badala ya kuwa na majimbo 264, tungekuwa na majimbo 184 pekee (sawa na idadi ya halmashauri).
Hii itasaidia kupunguza wabunge wa majimbo kutoka 264 hadi 184, hivyo kuokoa mabilioni ya shilingi kila mwaka.Na Tutaongeza Uchumi wetu..
Pia, wabunge wa viti maalum na wale wa kuteuliwa waondolewe, ili wawepo wabunge wa kuchaguliwa na wananchi pekee, Na Wabumge wa Kuchaguliwa na Wananchi wanaweza Kuwepo Wa Viti maalumu ila wanapigiwa Kura na Wanachi kitaifa Wasizidi 20
Tutaokoa Tsh ngapi?
Ikiwa kila mbunge wa jimbo analipwa mshahara na marupurupu wastani wa TZS 18,000,000 kwa mwezi, basi:
Kwa kupunguza idadi ya wabunge wa majimbo pekee, serikali ingeokoa zaidi ya TZS 20.4 Bilioni kwa mwaka katika mishahara tu!
MAREKEBISHO YA BAADHI YA WIZARA IKIWEMO KUPUNGUZA WIZARA,KUUNGANISHA WIZARA ILI KUONGEZA UFANISI
Kwa sasa Nchi yetu Ina wizara 24, kati ya Hizo wizara kuna Wizara zaidi ya Kumi ambazo zinashabiiana Context na Wizara zingine na Wakati mwingine Zina Overlap kwemye Utendaji kwanini Wizara zimazotegemeana Zisiwekwe Pamoja na Kuwa Wizara Moja ilu Kuongeza Ufanisi na Kupunguza Matumizi ya Vikao Nje ya Wizara, na Kuna Wizara nyingine Inafanya majukumu ya Wizara Zingine zinapaswa Kupunguza Au Kuondolewa kabisa..
Kwa mfano kwa Sasa Tuna makadirio ya:
Vipi kama Tukipunguza Wizara zikafanya kazi zile zile na Tukapata
ningependekeza Pia kufutwa kwa Wizara ya TAMISEMI na majukumu Yake Yarudishwe kwenye Wizara zinazosimamia baadhi ya mambo hayo..
TAMISEMI inaweza kufutwa na majukumu yake kuhamishiwa kwenye wizara nyingine. Kwa mfano:
Tunaweza Kupunguza Gharama Nyingi sana Kwa Kufanya Hivi wewe Unahisi Ni Kipi Kipunguzwe au Kiongezwe Kusaidia Hili Janga
Kwanza Kabisa Ni kupunguza matumizi Yasiyokuwa ya Lazima
Tuanze kwa Kudhibiti safari za nje za viongozi wa serikali kwa kuhakikisha zinafanyika pale tu inapohitajika sana.Kwa mfano Waziri wa Tamisemi Kwenda Kujifunza Kuhusu Local Government Nchini Urusi ,Wakati angeweza Kutumiwa Doccuments za Analytical Jinsi ya Kuongoza Local Government..Kudhibiti mikutano ya serikali isiyo na tija na kutumia njia za kisasa kama mikutano ya mtandaoni (virtual meetings) ili kupunguza gharama za usafiri na posho.
Mfano:- Katika mwaka wa fedha 2022/2023, serikali ilitenga zaidi ya TZS 500 Bilioni kwa safari za kikazi za viongozi ndani na nje ya nchi..
Basi kama Kuna Ulazima Sana angalau Tupunguze Matumizi ya Safari za Viongozi kwa kupunguza Bajeti yake kwa 50% yaani Angalau Iwe Tsh 250 Bilion..
Pili Kupunguza matumizi ya magari ya kifahari serikalini na kutumia magari yenye gharama nafuu na yanayotumia mafuta kidogo..
Tutoke kwenye Bajeti ya Bilion 180 Kwa Mwaka Ya Magari na Uendeshaji Tufike mpaka kwenye Bilion 20 Hivi au 30 au Kama Kuna Ulazima Sana Angalau Bilion 50..
KUFUTA OFISI YA MKUU WA WILAYA NA KUGAWA MAJUKUMU KWA MKURUGENZI WA HALMASHAURI
Ikiwa lengo ni kupunguza gharama za serikali, kupunguza urasimu, na kuongeza ufanisi wa utendaji, basi Ofisi ya Mkuu wa Wilaya inaweza kufutwa na majukumu yake kuhamishiwa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri, Hata Hivyo tumeshuhudia Mara nyingi sana Ofusi ya Mkuu wa Wilaya Ikiwa na Migongano ya Mara kwa mara ya Kiutendaji na Mkurugenzi kwa sababu ya Muingiliano wa Kimajukumu
Na Kuhusu Majukumu ya mkuu wa Wilaya Yanaweza kugawiwa kama Ifuatavyo..
- Majukumu ya Utawala na Usimamizi wa Halmashauri Yahamie kwa Mkurugenzi wa Halmashauri, kwa sababu Mkurugenzi wa Halmashauri tayari ana jukumu la kusimamia maendeleo na huduma za jamii. Anaweza kupewa mamlaka ya kusimamia usalama na utawala wa wilaya bila kuhitaji Mkuu wa Wilaya.
- Masuala ya Ulinzi na Usalama yanaweza kusimamiwa na Kamati ya Ulinzi ya Wilaya (RPC, OCD, na Wenyeviti wa Halmashauri) na Kingine Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD) anaweza kuchukua jukumu la kuratibu usalama moja kwa moja bila Mkuu wa Wilaya.
- Kuhusu Kuriport kwa mkuu wa wilaya Kamati ya Ulinzi ya Wilaya inaweza kuripoti moja kwa moja kwa Mkuu wa Mkoa.
- Kuripoti kwa Serikali Kuu Majukumu ya Mkuu wa Wilaya Kuriport kwa Serkali kuu yaani Kwa Rais kuhusu Hali ya Usalama majukumu hayo Yahamie kwa Mkuu wa Mkoa..
KUPUNGUZA IDADI YA MAJIMBO YA UBUNGE NA KUTUMIA HALMASHAURI KAMA MAJIMBO
Lengo letu si Kila mtu apate Keki ila Lengo ni kubana matumizi ya serikali na kupunguza gharama za uchaguzi na uendeshaji wa Bunge, basi hatua mojawapo ni kupunguza idadi ya majimbo ya uchaguzi na kutumia Halmashauri kama majimbo ya uchaguzi, Ili pesa Itakayobaki itumioe kwenye Bajeti ya Majukumu Mengine ambayo Yanahitajika sana..
Tanzania ina majimbo ya uchaguzi 264 (kwa mujibu wa uchaguzi wa 2020). Na pia Tanzania pia ina Halmashauri 184 (manispaa, wilaya, miji).
Hii ina maana kuwa kuna zaidi ya majimbo 80 ya ziada ambayo yanaongeza gharama za uchaguzi na mishahara ya wabunge, ambao wanafanya kazi sawa kabisa..
Badala ya kuwa na majimbo 264, tungekuwa na majimbo 184 pekee (sawa na idadi ya halmashauri).
Hii itasaidia kupunguza wabunge wa majimbo kutoka 264 hadi 184, hivyo kuokoa mabilioni ya shilingi kila mwaka.Na Tutaongeza Uchumi wetu..
Pia, wabunge wa viti maalum na wale wa kuteuliwa waondolewe, ili wawepo wabunge wa kuchaguliwa na wananchi pekee, Na Wabumge wa Kuchaguliwa na Wananchi wanaweza Kuwepo Wa Viti maalumu ila wanapigiwa Kura na Wanachi kitaifa Wasizidi 20
Tutaokoa Tsh ngapi?
Ikiwa kila mbunge wa jimbo analipwa mshahara na marupurupu wastani wa TZS 18,000,000 kwa mwezi, basi:
Kwa kupunguza idadi ya wabunge wa majimbo pekee, serikali ingeokoa zaidi ya TZS 20.4 Bilioni kwa mwaka katika mishahara tu!
MAREKEBISHO YA BAADHI YA WIZARA IKIWEMO KUPUNGUZA WIZARA,KUUNGANISHA WIZARA ILI KUONGEZA UFANISI
Kwa sasa Nchi yetu Ina wizara 24, kati ya Hizo wizara kuna Wizara zaidi ya Kumi ambazo zinashabiiana Context na Wizara zingine na Wakati mwingine Zina Overlap kwemye Utendaji kwanini Wizara zimazotegemeana Zisiwekwe Pamoja na Kuwa Wizara Moja ilu Kuongeza Ufanisi na Kupunguza Matumizi ya Vikao Nje ya Wizara, na Kuna Wizara nyingine Inafanya majukumu ya Wizara Zingine zinapaswa Kupunguza Au Kuondolewa kabisa..
Kwa mfano kwa Sasa Tuna makadirio ya:
- Mawaziri (24)
- Naibu Waziri (26)
- Katibu Mkuu (29)
- Naibu Katibu Mkuu (45)
Vipi kama Tukipunguza Wizara zikafanya kazi zile zile na Tukapata
- Mawaziri (13)
- Manaibu Mawaziri (15)
- Makatibu Wakuu (15)
- Naibu Makatibu Wakuu (26)
- Wizara ya Fedha na Uchumi au Wizara ya Fedha na Mipango
- Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
- Wizara ya Katiba na Sheria
- Wizara ya Ulinzi na Usalama wa Taifa
- Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamil, Jinsia na Wazee
- Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Habari
- Wizara ya Nishati, Madini na Rasilimali MaJi
- Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Miundombinu
- Wizara Ya Utumishi ,Ajira na Utawala Bora
- Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Miundombinu
- Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
- Wizara ya Mazingira na Mabadiliko ya Tabia ya nchi
- Wizara ya kilimo, Mifugo,Uvuvi na Maliasili
- Ofisi ya Waziri Mkuu (Waziri Mkuu)
ningependekeza Pia kufutwa kwa Wizara ya TAMISEMI na majukumu Yake Yarudishwe kwenye Wizara zinazosimamia baadhi ya mambo hayo..
TAMISEMI inaweza kufutwa na majukumu yake kuhamishiwa kwenye wizara nyingine. Kwa mfano:
- Majukumu ya Mamlaka za Serikali za Mitaa (Halmashauri, Manispaa, na Miji) Yanaweza Kuhamia Ofisi ya Waziri Mkuu, Kwa maana Hiyo Ofisi ya Waziri Mkuu inaweza kuongoza uratibu wa serikali za mitaa bila kuwa na wizara maalum. Hii itapunguza urasimu na kuimarisha usimamizi wa rasilimali kwa ufanisi zaidi.
- Usimamizi wa Afya za Msingi yaani Zahanati, Vitio vya Afya na Hospitali za Wilaya Pia Elimu Msingi na Sekondari yanaweza Kurudi kwenye Wizara zao Yaani Wizara ya Afya na Wizara ya Elimu..
- Tukienda Maswala ya Utawala Bora Yahamie Wizara ya Katiba na Sheria za utawala wa serikali za mitaa na miongozo ya utawala bora ziwe chini ya Wizara ya Katiba na Sheria moja kwa moja.
Tunaweza Kupunguza Gharama Nyingi sana Kwa Kufanya Hivi wewe Unahisi Ni Kipi Kipunguzwe au Kiongezwe Kusaidia Hili Janga