Ushauri: Mama Samia ukitoka Uganda, tunaomba tuondolee Kamanda Sirro

Volatility

JF-Expert Member
Aug 22, 2018
3,920
7,469
Najua kwa sasa machafuko ya huko Msumbiji yanakukosesha usingizi, ukizingatia ukaribu wa Taifa letu na maeneo ambayo Majeshi ya Serikali ya Msumbiji yameshindwa kudhibiti hao tunaombiwa ni magaidi.

Mimi naomba nikutie moyo, hofu yako ni sahihi, na ninakuombea kwa Mwenyezi Mungu akupe busara za kukabaliana na changamoto hizo.

Ni Mategemeo yangu kwamba washauri wako wa masuala ya ulinzi na usalama, na Majeshi yetu yako tayari kukabiliana na changamoto hizo, na mpaka sasa ninaunga mkono maamuzi ya Serikali yetu kuzuia wakimbizi wa machafuko huko Msumbiji kuweka kambi nchini mwetu, endelea na msimamo huu mpaka dakika ya mwisho.

Lakini, ukirudi, ukirudi kutoka Kampala tuondolee Sirro. Vilio, majonzi, machungu, na hasira za wananchi wa Taifa hili dhidi ya Serikali yako na Magufuli ni namna Jeshi la Polisi chini ya Sirro lilivyoshindwa kujiweka mbali na matukio ya utekaji nyara na mauaji ya Raia katika mazingira yaliyoonekana kuwa ya kisiasa.
 
Magufuli atakumbukwa Sana kwa namna alivyoweza Kudhibiti hali ya ulinzi na usalama wa nchi. Mtakumbuka, kabla yake, nchi ilikumbwa na Vitisho vya magaidi( Rejea uwepo wa Alshaba kwenye mapango ya Ambon), kuibuka kwa makundi ya Waislam wenye Itikadi Kali yaliyokua yanajihusisha na utekaji nyara, kuua watumishi wa Mungu ( Hasa upande Zanzibar) na kuchoma makanisa.

Baada ya hapo, mtakumbuka tishio la MKIRU. Uwepo wa Magaidi Kibiti waliokua wanaua Maaskari na viongozi wa serikali, lilikuwa ni tishio kubwa kwa Usalama wa nchi na Watanzania walishaingiwa na hofu kwamba Sasa Yale ya Somali yangekua yanafanyika kwenye Pwani ya Tanzania.

Kwa umahiri wa vyombo vyetu vya ulinzi na Usalama chini ya Amir Jeshi Mkuu, JPM, tishio lile lilithibitiwa kwa ustadi Mkubwa na kweli mpaka Mungu anamchukua, nchi iko salama.

Katika hili, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama nao wanahitaji help.

Mwenyezi Mungu azipokee roho za marehemu waliouawa kwa bahati mbaya kwenye operation ile, awapokee kwenye nuru ya uso wake.
 
Tunataka amani na upendo awamu ya 6 hoyee tunakunywa mbege na komoni kiroho safi na inashuka koo kelele na shobo zimeenda na mwendazake
 
Magufuli atakumbukwa Sana kwa namna alivyoweza Kudhibiti hali ya ulinzi na usalama wa nchi. Mtakumbuka, kabla yake, nchi ilikumbwa na Vitisho vya magaidi( Rejea uwepo wa Alshaba kwenye mapango ya Ambon), kuibuka kwa makundi ya Waislam wenye Itikadi Kali yaliyokua yanajihusisha na utekaji nyara, kuua watumishi wa Mungu ( Hasa upande Zanzibar) na kuchoma makanisa.
Baada ya hapo, mtakumbuka tishio la MKIRU. Uwepo wa Magaidi Kibiti waliokua wanaua Maaskari na viongozi wa serikali, lilikuwa ni tishio kubwa kwa Usalama wa nchi na Watanzania walishaingiwa na hofu kwamba Sasa Yale ya Somali yangekua yanafanyika kwenye Pwani ya Tanzania.
Kwa umahiri wa vyombo vyetu vya ulinzi na Usalama chini ya Amir Jeshi Mkuu, JPM, tishio lile lilithibitiwa kwa ustadi Mkubwa na kweli mpaka Mungu anamchukua, nchi iko salama.
Katika hili, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama nao wanahitaji help.
Mwenyezi Mungu azipokee roho za marehemu waliouawa kwa bahati mbaya kwenye operation ile, awapokee kwenye nuru ya uso wake.
Amina
 
Magufuli atakumbukwa Sana kwa namna alivyoweza Kudhibiti hali ya ulinzi na usalama wa nchi. Mtakumbuka, kabla yake, nchi ilikumbwa na Vitisho vya magaidi( Rejea uwepo wa Alshaba kwenye mapango ya Ambon), kuibuka kwa makundi ya Waislam wenye Itikadi Kali yaliyokua yanajihusisha na utekaji nyara, kuua watumishi wa Mungu ( Hasa upande Zanzibar) na kuchoma makanisa.
Baada ya hapo, mtakumbuka tishio la MKIRU. Uwepo wa Magaidi Kibiti waliokua wanaua Maaskari na viongozi wa serikali, lilikuwa ni tishio kubwa kwa Usalama wa nchi na Watanzania walishaingiwa na hofu kwamba Sasa Yale ya Somali yangekua yanafanyika kwenye Pwani ya Tanzania.
Kwa umahiri wa vyombo vyetu vya ulinzi na Usalama chini ya Amir Jeshi Mkuu, JPM, tishio lile lilithibitiwa kwa ustadi Mkubwa na kweli mpaka Mungu anamchukua, nchi iko salama.
Katika hili, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama nao wanahitaji help.
Mwenyezi Mungu azipokee roho za marehemu waliouawa kwa bahati mbaya kwenye operation ile, awapokee kwenye nuru ya uso wake.
Lakini vitisho, mateso na mauaji dhidi ya wanasiasa vilipitiliza.
 
Tumbuke muundo wa kisiasa nchini mwetu kwa mujibu wa katiba yetu ni sehemu kubwa sana ya maisha yetu ya kila siku. Magufuri alishindwa kuelezea msimamo wake wa kisiasa kwa hoja, akatumia mabavu na nguvu za kijesho kutimiza mawazo yake ya kisiasa huku akiacha mamilioni ya watanzania wakiwa hawaelewi mstakali waTaifa kisiasa ni upi.
 
Magufuli atakumbukwa Sana kwa namna alivyoweza Kudhibiti hali ya ulinzi na usalama wa nchi. Mtakumbuka, kabla yake, nchi ilikumbwa na Vitisho vya magaidi( Rejea uwepo wa Alshaba kwenye mapango ya Ambon), kuibuka kwa makundi ya Waislam wenye Itikadi Kali yaliyokua yanajihusisha na utekaji nyara, kuua watumishi wa Mungu ( Hasa upande Zanzibar) na kuchoma makanisa.
Baada ya hapo, mtakumbuka tishio la MKIRU. Uwepo wa Magaidi Kibiti waliokua wanaua Maaskari na viongozi wa serikali, lilikuwa ni tishio kubwa kwa Usalama wa nchi na Watanzania walishaingiwa na hofu kwamba Sasa Yale ya Somali yangekua yanafanyika kwenye Pwani ya Tanzania.
Kwa umahiri wa vyombo vyetu vya ulinzi na Usalama chini ya Amir Jeshi Mkuu, JPM, tishio lile lilithibitiwa kwa ustadi Mkubwa na kweli mpaka Mungu anamchukua, nchi iko salama.
Katika hili, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama nao wanahitaji help.
Mwenyezi Mungu azipokee roho za marehemu waliouawa kwa bahati mbaya kwenye operation ile, awapokee kwenye nuru ya uso wake.
Magu aliondoa hivyo vitisho na kuwa yeye gaidi namba moja wa ndani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tungejua kesho itakuwaje tungejipendekeza kwa mama alipokua VP. Wengine walimdharau hata akitua uwanja wa ndege kutoka katika safari za kumeakilisha Rais hawakwenda kumpokea.
 
Akitoka UG adeal kwanza na Voda.. hawa jamaa wamegoma kushusha bei za bundle
 
... lilidhibitiwa... siyo lilithibitiwa! Kuna utofauti wa "dhibiti" na "thibiti". Ila nakupongeza sana kwa kutoa ushauri mzuri
Magufuli atakumbukwa Sana kwa namna alivyoweza Kudhibiti hali ya ulinzi na usalama wa nchi. Mtakumbuka, kabla yake, nchi ilikumbwa na Vitisho vya magaidi( Rejea uwepo wa Alshaba kwenye mapango ya Ambon), kuibuka kwa makundi ya Waislam wenye Itikadi Kali yaliyokua yanajihusisha na utekaji nyara, kuua watumishi wa Mungu ( Hasa upande Zanzibar) na kuchoma makanisa.
Baada ya hapo, mtakumbuka tishio la MKIRU. Uwepo wa Magaidi Kibiti waliokua wanaua Maaskari na viongozi wa serikali, lilikuwa ni tishio kubwa kwa Usalama wa nchi na Watanzania walishaingiwa na hofu kwamba Sasa Yale ya Somali yangekua yanafanyika kwenye Pwani ya Tanzania.
Kwa umahiri wa vyombo vyetu vya ulinzi na Usalama chini ya Amir Jeshi Mkuu, JPM, tishio lile lilithibitiwa kwa ustadi Mkubwa na kweli mpaka Mungu anamchukua, nchi iko salama.
Katika hili, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama nao wanahitaji help.
Mwenyezi Mungu azipokee roho za marehemu waliouawa kwa bahati mbaya kwenye operation ile, awapokee kwenye nuru ya uso wake.
 
Back
Top Bottom