Nawasalimu wote, mambo zenu, shikamoo wakubwa ila siwanyimi chochote unaruhusiwa kuomba
Nirudi kwenye mada jamani kaka zangu na rafiki zangu wa kiume kwenye swala la kumtongoza mwanamke mnaboa jamani kila ukija unaongela mambo ya mapenzi tu oooh i love you, oooh sijui unaumbo nzuri hivi jamani haya maneno yanachosha kila siku kuongelea hayo hayo.
Okey basi mwanamke najaribu kubadilisha mada hata tuongelee utamaduni wetu huna hoja unajiumauama kiuchumi ndo kabisa nakupoteza hivi niwaulize huwa mnafikiria nini kwenye akili zenu?
All over the way unafikiria kuniambia i love you mimi huwa unanichosha jamani lets talk about other issues nichekeshe, tuongeleee uchumi, okey basi be funny mtu anaishia kukwambia i love na kubusu busu mikono hivi ni nini lakini BE CREATIVE GUYS LOH TOOO MUCH
Unakuta mwanaumme unamuuliza what is your plan for future anaongelea vitu vya ajabu a wengine amna majibu yani mimi nachefuka moyo nikiona mwanume ajielewi natamani kutapika.
Basi wanaume jiongeze basi ongea love yes, hapo hapo ongelea uchumi, siasa na hata utamaduni ili nijue una upeo gani wa kufikiri loh, mpira usiongelee wala movie.
Ihope mtajiongeza kwa kweli, nawapenda wote.
Umeongea kitu cha maana saana .
Kama ungekua bunge spika angeaema Hoja yako ina mashiko.
Ila nataka nikueleweshe jambo moja.,iko hiviii ,
Mwanaume anapomwaproach mwanamke ,anavaa tabia husika ya mwanamke mwnyewe,mfano, ww Miss Chaga kakukuta unapenda siasa ,atakuja Akiongelea updates za Bunge na Mambo ya siasa.. Kama ww napenda habari za Macelebrities atakuja hivyo hivyo , yaani ni kama kinyonga ,atahakikisha anamartch na ww kwa namna unavyotaka ,ili tu akupate .
Mwanume hawezi ongelea jambo ambalo halikuvutii ,zaidi atakuboa.
Kuna wanawake hata ukiwauliza Raisi wa Tanzania ni nani ,anaweza kukuambia Ni Mkapa, mtu ka huyo ina maana siasa hazipendi,kuongea siasa na yeye ni kimchefua.
Hivyo basi ,jambo hili linaanza moja kwa moja na nyie wenyewe ,ni namna ipi mnajiweka mnapotongozwa. ??
" Miss Chaga" ww Atakayekutongoza ni lazima aje akiwa ana Msimamo wa Muundo wa Serikali unayoihitaji.
Na aweze kuutetea muundo huo.