Ushauri kwa shule za Dsm na wizara ya Elimu

Ushauri kwa shule za Dsm na wizara ya Elimu

stabilityman

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2024
Posts
812
Reaction score
1,753
Mimi binafsi sifurahishwi kabisa na tabia inayojitokeza katika baadhi ya shule za msingi ambapo mtoto anatakiwa kwenda kila siku na shilingi 1000 kwa ajili ya chakula, na endapo akikosa hela hiyo anapewa adhabu ya fimbo au kubezwa.

Ninapenda kutoa maoni yangu kwa heshima, lakini pia kwa uwazi:

1. Si kila mzazi ana uwezo wa kutoa pesa kila siku, hasa katika mazingira ambayo mambo ya kiuchumi ni magumu.

2. Kama mzazi nina uwezo wa kumpikia mtoto chakula nyumbani na kuweka kwenye chombo chake, si sahihi kwa shule kukataa mtoto kutumia chakula alichopewa nyumbani.

3. Shule kutaka pesa pekee kama njia ya kupata chakula, bila kuzingatia hali tofauti za familia, kinaweka mzigo usio wa lazima kwa wazazi.

4. Mtoto kupigwa fimbo kwa sababu ya kukosa fedha ni jambo linaloumiza sana—kisaikolojia na kimwili—na halipaswi kuwa adhabu ya kosa kama hilo.

5. Elimu ya msingi hapa nchini inapaswa kuwa bila vikwazo, na mzazi kumwandalia mtoto chakula si kosa, wala haitakiwi kuwa chanzo cha adhabu.

6. Tunapaswa kufundisha watoto utu, heshima, usawa na upendo—sio kuwaogopesha au kuwaumiza kutokana na changamoto za nyumbani ambazo hawana uwezo wa kuamua.

7. Wizara ya Elimu na mamlaka husika zingeangalia suala hili kwa makini, kwani linaathiri motisha ya watoto kusoma na linaweza kuchochea unyanyasaji wa kimyakimya shuleni.

8. Naamini kuna njia bora zaidi za kusimamia chakula cha wanafunzi, kama maelewano na wazazi, si adhabu.

Kwa kifupi: Mimi binafsi sina furaha na mwenendo huu, na ninaamini kuna haja ya mabadiliko ili kulinda usalama, utu na haki ya mtoto kupata elimu bila hofu au shuruti zisizo na msingi.
Habari huu ujumbe nimekutana nao Facebook amepost mdau

#followerseveryone
#wizarayaelimu
#WatotoKwanza
#trackandfield
 
Inasikitisha sana nasio dar es salaam tu hata huku mkoani Kuna baadhi ya shule wanatoza fedha kwaajili ya chakula.
 
Inasemekana kwa mikoa ya kaskazini moja ya sababu inayochangia wanafunzi kufanya vizuri ni uwepo wa chakula shuleni, wewe mtaalamu unatuambia wazazi wanabebeshwa mzigo mzito wanapotakiwa kuwapa watoto wao buku buku za maosi shuleni, kwa hiyo unamaanisha hakuna haja ya mwanao kupata chakula awapo masomoni?
 
Inasikitisha sana nasio dar es salaam tu hata huku mkoani Kuna baadhi ya shule wanatoza fedha kwaajili ya chakula.
Wanakwambia watoto wanafeli kwa sababu ya njaa ni fact ndio lakini sio hiyo peke yake hata ufundishaji walimu weupe sana kichwani wanatafsiri notes tu, japo wapo wachache wao hasa hao wapo shule kubwa kubwa lakini hawa wengine ni wapo shallow sana! hata wakikasirika
 
Ametoa hoja ya maana kabisa.
Bahati mbaya hio huduma ya chakula shuleni si huduma tena ni biashara.

Mfano shule anasoma mtoto wangu kuna mzabuni anatoa inayo itwa huduma ya chakula, sasa waalimu ndio wamepewa kandarasi ya kukusanya fefha , tena kwetu si 1000 bali ni 1500.

Sasa ole mwanafunzi asie lipa!

Si kilamzazi ana aweza kulipa hio 1500, wengini wana watoto 3, mzazi ana lipa 4,500 kila siku ya masimo.

Tufanye siku za masomo ni 200 kwa mwaka, hapo mzazi awe na zaidi ya milion 2, hapo bado usafiri , bado hela za mitihani kila mwezi 6,000 kwa kila mwanafunzi, michango mingine nk.

Na hio ni shule ya serikali inayo simamiwa na halmashauri!

Lakini tuna ambiwa elimu ni bure!

Hivi wangewapa uji ambao labda iwe 300 hadi 500 ingeshindikana kwa mzazi kweli?
 
Ushauri Huu Serikali Iupokee Mikono Miwili
Nyongeza Siyo Kwa Dsm Tu Nchi Nzima Michango Imezidi Wazazi Hatupumui
*Serikali Ifute Neno Elimu Bure

Michango Na Cash Ni Nyingi Sana Kwa Wazazi
 
Pamoja na malalamiko yote hayo kiini cha tatizo ni wazazi.
Hapo wengi mko tayari kuwa na watoto lakini malezi ya watoto hamko tayari.

Wanaume wengi wa kibongo matuzimizi yao binafsi kwa siku ni zaidi ya tsh 10000,, tena hao ni wa kipato cha chini wengine matumizi Yao binafsi kwa siku ni zaidi ya 100000 tena hapo anakwambia kajibana sana.

Mtoto juu ya miaka mitano anahitaji malezi kupitia pesa yako zaidi maana hapo mtoto kaanza shule, muda na akili.
Wazazi wapeni malezi stahili watoto ikiwepo haki ya kufurahia mazingira ya shule bila kuwa na njaa na bila kutamani vya wengine.
Baadae mtoto akiwaka tamaa akaanza wizi au uhuni utamlaumu Nani!?

Pia muwe mnahudhuria vikao vya shule na kushiriki mijadala kuepusha malalamiko kama haya.
 
Inasemekana kwa mikoa ya kaskazini moja ya sababu inayochangia wanafunzi kufanya vizuri ni uwepo wa chakula shuleni, wewe mtaalamu unatuambia wazazi wanabebeshwa mzigo mzito wanapotakiwa kuwapa watoto wao buku buku za maosi shuleni, kwa hiyo unamaanisha hakuna haja ya mwanao kupata chakula awapo masomoni?
Tumia akili vizuri kumuelewa mleta uzi ..hoja yake 👉ni kipigo kwa mtoto kwa kukosa hela ambayo siyo jukumu la mtoto bali mzazi au mlezi wake
 
Hakuna elimu bure hii nchi, kuna hidden costs nyingi sana kila kona zinazolalamikiwa na wazazi ambazo zinasimamiwa na sheria za mchongo za walimu wakuu.
 
Pamoja na malalamiko yote hayo kiini cha tatizo ni wazazi.
Hapo wengi mko tayari kuwa na watoto lakini malezi ya watoto hamko tayari.

Wanaume wengi wa kibongo matuzimizi yao binafsi kwa siku ni zaidi ya tsh 10000,, tena hao ni wa kipato cha chini wengine matumizi Yao binafsi kwa siku ni zaidi ya 100000 tena hapo anakwambia kajibana sana.

Mtoto juu ya miaka mitano anahitaji malezi kupitia pesa yako zaidi maana hapo mtoto kaanza shule, muda na akili.
Wazazi wapeni malezi stahili watoto ikiwepo haki ya kufurahia mazingira ya shule bila kuwa na njaa na bila kutamani vya wengine.
Baadae mtoto akiwaka tamaa akaanza wizi au uhuni utamlaumu Nani!?

Pia muwe mnahudhuria vikao vya shule na kushiriki mijadala kuepusha malalamiko kama haya.
Una hoja usikilizwe
 
Ametoa hoja ya maana kabisa.
Bahati mbaya hio huduma ya chakula shuleni si huduma tena ni biashara.

Mfano shule anasoma mtoto wangu kuna mzabuni anatoa inayo itwa huduma ya chakula, sasa waalimu ndio wamepewa kandarasi ya kukusanya fefha , tena kwetu si 1000 bali ni 1500.

Sasa ole mwanafunzi asie lipa!

Si kilamzazi ana aweza kulipa hio 1500, wengini wana watoto 3, mzazi ana lipa 4,500 kila siku ya masimo.

Tufanye siku za masomo ni 200 kwa mwaka, hapo mzazi awe na zaidi ya milion 2, hapo bado usafiri , bado hela za mitihani kila mwezi 6,000 kwa kila mwanafunzi, michango mingine nk.

Na hio ni shule ya serikali inayo simamiwa na halmashauri!

Lakini tuna ambiwa elimu ni bure!

Hivi wangewapa uji ambao labda iwe 300 hadi 500 ingeshindikana kwa mzazi kweli?
Wazazi kutaneni na uongozi wa shule mpange utaratibu mzuri, we unywe supu na chapati mbili halafu mwanao anywe uji, hujui uji unaleta usingizi??
 
Wazazi kutaneni na uongozi wa shule mpange utaratibu mzuri, we unywe supu na chapati mbili halafu mwanao anywe uji, hujui uji unaleta usingizi??
Wazazi wengi hawaendi kwenye vikao wanaishia kulalama nje, mawazo yao wanapaswa kuyawasilisha kwenye vikao
 
Back
Top Bottom