Ushauri kwa Sam Mahela, Mtangazaji wa ITV

naunga mkono hoja huyu jamaa anajitahidi sana
 
Wale makubwa jinger na mabishoo wa clouds nao unawashaurije?????

Sam Mahela, big up.

Nakuona BBC kwa jicho la tatu.
 

Zeruzeru= albino
 
Mtu akija na details za diamond,zari,wema na wengine hamshangai lkn mambo kyanayogusa jamii mnashangaa.......!!!!!????
Mungu atusaidie watanzania


Kwa hapa tulipofikia hata mungu hawezi kutusaidia
 
kwa report za Sam sisi kama wadau tumshauri awanie tuzo nasio kumkatisha Tamara kama wanavofanya wengine
 
Mungu aendelee kumbaliki ni mtu makini sana Sam Maela
I salute you brother
 
"Marafiki zangu nimeskikitishwa sana na baadhi ya watu wachache wanaopinga jitihada zangu kama mwanahabari katika mjadala unaoendelea katika mtandao wa jamii forum kwenye hoja mchanganyiko, natamani kutoa majibu kwa baadhi ya watu ambao hata mtu akifanya vizuri katika jambo fulani kamwe hawawezi kukubali kwamba kimefanyika kizuri lakini bahati mbaya sijajisajili kwenye jamii forum,

kuna mtu anadai pengine ni mimi ndo nimeandika kwenye jamii forum ili kujipigia debe nipate tuzo, laiti angejua kuwa hata angeuliza baraza la habari Tanzania kama nimepeleka kazi yangu yeyote ili kushiriki tuzo.Ingawa wengi wamenishauri kufanya hivyo lakini sijapeleka. Mwingine akadai hizo habari zangu napangiwa na mhariri wangu, Dah kazi zangu nyingi za Itv,

asilimia kubwa ya kazi nimetafuta mwenyewe na siku zote sitegemei kutumwa na mkuu wangu wa kazi ili nipate habari bali naangaika mwenyewe kutafuta habari. Nilichogundu kuwa kuna baadhi ya watu hata kama mtu atafanya kizuri kamwe hawezi kupongeza ila akifanya baya basi hilo baya atalitangaza kila kona...

Mimi ni Sam na siku zote sifanyi kazi zangu kwa kushindana na mtu,bali nafanya kazi zangu kwa kumtegemea MUNGU.........ipo siku MUNGU wetu ataonekana juu yetu hata kama hakuna wa kuoneka juu yetu kwa sasa. MUNGU AWABARIKINI RAFIKI ZANGU WA FACEBOOK, kwa wale waliojiunga na jamii forum angalieni mtaona

maana kuna mwandishi mwenzangu kabadilisha jina katika jamii forum ananiponda kweli lakini yeye anashindwa kupambanua kuwa mimi nina miaka mingapi katika fani na hao wengine anaonilinganisha nao chipukizi katika fani kama sisi au ni wakongwe wa miaka mingi? MUNGU na atusaidie maana unaposhindwa kupongeza mtu awaye yeyote hata kama sio mimi anapofanya vizuri kwa ajili ya wivu basi hiyo ni roho na anayeweza kuiondoa ni MUNGU peke yake."---Source Sam Mahela FB Page.

 
Hivi ni kwanini huyu ndugu akiwa anamalizia simulizi zake kwenye tv pale anapotaja jina lake huwa anatingisha tingisha kichwa kama ana stroke vile?? au ndo sign off signature yake???
 
Km uliyosema ni kweli basi inabidi awe mwandishi, mfuatiliaji na mchambuzi bora duniani
 
Usihofu kaka kazi yenu ina changamoto nyingi lakn piga moyo konde utafika tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…