badison
JF-Expert Member
- May 29, 2015
- 1,450
- 2,702
Mh. Jaji Mkuu, kumekuwa na ongezeko kubwa sana la talaka zisizo na msingi. Hii inapelekea familia nyingi kusambaratika na watoto kuteseka kuanzia ada mpaka uniform za shule. Elimu Bora inaanzia ngazi ya chini kabisa Familia.
Nina sikitishwa sana na mahakimu wengi kufanya maamuzi mabovu ya kuvunja ndoa za watu bila sababu za msingi, na hasa upendeleo huelekezwa zaidi kwa wanawake.
Yaani nimeisoma baadhi ya hukumu kila anacho zungumza mwanamke amasikilizwa na mwanaume anaonekana ndie mwenye makosa. Mahakimu wakiume wengi ni very emotional towards women, hasa wakiona machozi.
Pathetic, hakimu hatakiwi kuwa emotional hata siku moja. Kuwa hakimu sio maksi au vyeti ni integrity.
Hii pia ipo katika kugawana mali, tunataka precedent mpya ya kugawanya mali kulingana na mchango halisi wa mtu.
Haiwezekani mtu unamtunza kila kitu halafu anakusaliti, kisha mgawane 50/50. Hata kama mwanaume ndio kasaliti pia, gawiwo la 50/50 bado ni kubwa sana.
Mahakimu hawajui sheria hasa upande wa kutoka adhabu, wamefungwa na kiini macho cha jinai na madai. Kwamba, kwanini hakimu hawezi kutoka adhabu ya viboko mia moja kwa kila mwanandoa mpumbavu avunjae ndoa yake ili zao lake liteseke?! Ifike mahali adhabu ya viboko itolewe kwenye mashauri yasiyo ya msingi hasa ya ndoa na mirathi.
Hata kama kufungua kesi za talaka na mirathi ni bei rahisi hivyo, isiwe sababu ya kuleta usumbufu mahakamani na kuwasumbua mahakimu kwa kesi za talaka za kipumbavu.
Hakimu akijiridhisha hakuna sababu za msingi kuvunja ndoa atoe adhabu ya viboko 500, yaani mwaka mzima hawa wanandoa wapumbavu wanachapwa tuu na kurudi nyumbani mwaka mzima.
Mahakama ijikite kurudisha ndoa na sio kuvunja ndoa. Kila siku eti kwa sababu mtu kafungua shauri, hukumu itoke bila adhabu kali ili watu wasizoee mahakama.
Mahakama ni tunu sio sehemu ya kusikilizwa kesi za mizaha.
"There is a devil present in a court room which make a man tremble and speak the truth, the whole truth and nothing but truth" ~ Unknown
Nina sikitishwa sana na mahakimu wengi kufanya maamuzi mabovu ya kuvunja ndoa za watu bila sababu za msingi, na hasa upendeleo huelekezwa zaidi kwa wanawake.
Yaani nimeisoma baadhi ya hukumu kila anacho zungumza mwanamke amasikilizwa na mwanaume anaonekana ndie mwenye makosa. Mahakimu wakiume wengi ni very emotional towards women, hasa wakiona machozi.
Pathetic, hakimu hatakiwi kuwa emotional hata siku moja. Kuwa hakimu sio maksi au vyeti ni integrity.
Hii pia ipo katika kugawana mali, tunataka precedent mpya ya kugawanya mali kulingana na mchango halisi wa mtu.
Haiwezekani mtu unamtunza kila kitu halafu anakusaliti, kisha mgawane 50/50. Hata kama mwanaume ndio kasaliti pia, gawiwo la 50/50 bado ni kubwa sana.
Mahakimu hawajui sheria hasa upande wa kutoka adhabu, wamefungwa na kiini macho cha jinai na madai. Kwamba, kwanini hakimu hawezi kutoka adhabu ya viboko mia moja kwa kila mwanandoa mpumbavu avunjae ndoa yake ili zao lake liteseke?! Ifike mahali adhabu ya viboko itolewe kwenye mashauri yasiyo ya msingi hasa ya ndoa na mirathi.
Hata kama kufungua kesi za talaka na mirathi ni bei rahisi hivyo, isiwe sababu ya kuleta usumbufu mahakamani na kuwasumbua mahakimu kwa kesi za talaka za kipumbavu.
Hakimu akijiridhisha hakuna sababu za msingi kuvunja ndoa atoe adhabu ya viboko 500, yaani mwaka mzima hawa wanandoa wapumbavu wanachapwa tuu na kurudi nyumbani mwaka mzima.
Mahakama ijikite kurudisha ndoa na sio kuvunja ndoa. Kila siku eti kwa sababu mtu kafungua shauri, hukumu itoke bila adhabu kali ili watu wasizoee mahakama.
Mahakama ni tunu sio sehemu ya kusikilizwa kesi za mizaha.
"There is a devil present in a court room which make a man tremble and speak the truth, the whole truth and nothing but truth" ~ Unknown