Ushauri kuhusu huyu mdogo wangu mkopo wa milion 100

Ushauri kuhusu huyu mdogo wangu mkopo wa milion 100

co fm

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2016
Posts
1,569
Reaction score
2,584
Hello wadau, poleni sana na majukumu ya kulijenga taifa.

Ipo hivi mimi nina mdogo wangu mwaka jana alipata mchongo kwenye taasisi moja hivi na wanamlipa vizuri sana like 4m kwa mwezi na tena bado ni mdogo sana ni miaka 26 tu.

Juzi kaja home nikawa namuulizia habari za kazi akawa anipa stories zake kuhusiana na kazi yake ndo kaniambia anauwezo wa kukopa hadi milion 100 kwa udhamini wa ofisi yao.

Je, ni mshauri tu akope au aiache maana anaweza kukopa kwa kufanya vitu vya msingi mwisho wa siku ikawa majanga
 
Anataka kukopa sababu anakopesheka? Au ana mipango anataka kufanya? ni mipango ipi?
Akikopa ni sawa, asipokopa ni sawa, inategemea anataka kufanyia nini hiyo pesa. Ila kwa kujaribu kudadisi unachotaka kujua, Anaweza kukopa akafanyia maendeleo kama vile kujenga nyumba, ikiwa hana makazi, kununua gari kama ana changamoto za usafiri. Pia anaweza kuanzisha miradi ya maendeleo kama nyumba za kupangisha, biashara au uwekezaji katika kilimo na ufugaji.
 
Kabla ya kukopa je hiyo 4m ina matumizi na anaweza kusave?

Kuingia kwenye mkopo bila kujua utafanyia nini hiyo hela ni janga kubwa. Mwache aendelee kupata mshahara wakati anatafakari cha kufanya. Kukopa bila sababu ni kujitia umasikini.

1. Usikope kuanzisha biashara kopa kuendeleza biashara iliyosimama.
2. Usikope kununua gari la kifahari. Nunua gari la kawaida less than 20m.
3. Asikope kununua kiwanja kwa kuwa hiyo 4m akisave kiasi kwa mwaka ananunua kiwanja.
4. Asikope kujenga nyumba ya kuishi atajitia kwenye madeni na fustration kwenye umri mdogo.

Wewe ndio unataka akope mtumbue hizo hela....
 
Nimejaribu kuweka repayment plan kwa kufuata sheria inayotaka muajiriwa abakie na si chini ya 45% ya mshahara wake. So atalipa mkopo kwa miaka 6 (interest ya 18% reducing) , makato yake 2.2M. Mpaka mkopo unaisha atakuwa amelipa riba ya 64M.
So apime uwiano wa faida na hasara (gharama) za mkopo then afanye maamuzi.
 

Attachments

  • Screenshot_20260108-225822_1.jpg
    Screenshot_20260108-225822_1.jpg
    441.2 KB · Views: 6
Huo n ujinga wa hali ya juu, atalipa huo mkopo sio chini ya miaka mitano tena kwa ongezeko la zaidi ya 50M yani atalipa jumla 150+

Sasa Huu ni upumbavu, wakati ndani ya miaka minne akiweka 2M kila mwezi ana uhakika wa kupata hy 100M.

Nna uhakika anaweza kuweka 2M kwa mwezi kwa sababu hakuna familia yoyote ya kitanzania inayoweza kumaliza 2M kwa mwezi, tuache kudanganyana na kujipandisha.
 
Hello wadau, poleni sana na majukumu ya kulijenga taifa.

Ipo hivi mimi nina mdogo wangu mwaka jana alipata mchongo kwenye taasisi moja hivi na wanamlipa vizuri sana like 4m kwa mwezi na tena bado ni mdogo sana ni miaka 26 tu.

Juzi kaja home nikawa namuulizia habari za kazi akawa anipa stories zake kuhusiana na kazi yake ndo kaniambia anauwezo wa kukopa hadi milion 100 kwa udhamini wa ofisi yao.

Je, ni mshauri tu akope au aiache maana anaweza kukopa kwa kufanya vitu vya msingi mwisho wa siku ikawa majanga
Kijana ana bahati kubwa sana kupata mshahara wa 4m akiwa na miaka 26, hilo ni baraka. Ila mkopo wa ofisini wa 100m unahitaji tahadhari kubwa. Kazi si ya milele lakini deni hubaki. Kabla hajakopa ajihakikishie ana akiba ya kutosha, ana mpango wa uwekezaji unaolipa mkopo wenyewe (sio kutegemea mshahara), na aanze na mkopo mdogo kama majaribio. Bila mpango ulioandikwa na kipato mbadala, ni bora aiache kuliko kuingia majanga baadaye. Mkopo mzuri ni ule unaolipa wenyewe, si ule wa kuonyesha uwezo.
 
Kijana ana bahati kubwa sana kupata mshahara wa 4m akiwa na miaka 26, hilo ni baraka. Ila mkopo wa ofisini wa 100m unahitaji tahadhari kubwa. Kazi si ya milele lakini deni hubaki. Kabla hajakopa ajihakikishie ana akiba ya kutosha, ana mpango wa uwekezaji unaolipa mkopo wenyewe (sio kutegemea mshahara), na aanze na mkopo mdogo kama majaribio. Bila mpango ulioandikwa na kipato mbadala, ni bora aiache kuliko kuingia majanga baadaye. Mkopo mzuri ni ule unaolipa wenyewe, si ule wa kuonyesha uwezo.
Logic
 
Back
Top Bottom