Ushauri: Dada yangu ananiomba sana Pesa

Ushauri: Dada yangu ananiomba sana Pesa

Cash Generating Unit

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2019
Posts
13,284
Reaction score
39,491
Wakuu habari. Dada angu tunashare mama amekua ananiomba sana pesa sio kwamba sipendi but imekua too much sana. Akiwa hana pesa ya vikoba sijui michezo yao wanajua wenyewe lazima anichek nitampa anaweza sema nimkope but huwa simdai imeisha hyo.

Ameolewa na ana wtt wa2 Ila cha kushangaza shemej yangu yupo vizuri anafanyia kazi Taasisi kubwa tu huko chugga. Yeye kama yeye ana biashara zake za saloon zinamwingizia pesa.

Nawaza mimuulize pesa anazopata kwenye busn anafanya nn au shem hatoi matunzo? Naona kama haitakuwa sawa, honestly yeye ndo anatakiwa kunisave dg lake yeye kama yeye maisha katoboa tyr.

Nipeni ushauri hapa bandugu.
 
Inawezekana akawa anakuamini sana, na amekuona katika ndugu zake wewe unafaa kumpa msaada. Jaribu kumsaidia maana siku utapata tatizo na unaweza ukakosa mtu wa kukusaidia lakini yeye ndiye atakayekuja kukuinua.
Kwa kawaida mtu unayemsaidia, ni vigumu kumuonea aibu pindi unapohitaji msaada.
 
Saidia pale unapokuwa na uwezo wa kusaidia wala usiwaze. Ni kama uwekezaji na huyo ndugu yako jua kuwa anakukubali sana na atakuja kukulipa makubwa. Ukiwa una mwambie sina ukiwa nacho msaidie
 
Sidhani kama mtu anaweza kuanzisha mchezo bila chanzo cha mapato ila tunakuwa tumekwama tu kupata
Hahahah ukiwa na mradi wa kukuingizia pesa huwezi kwama shida yenu mnategemea huruma zetu ME!

Unakwamaje, unakuta mtu anacheza mchezo wa 30k kila siku ila anategemea aombe ombe kwa watu hio biashara inaniboaga sana. Na unajua kabisa mtu kazi hana ila shobo zake tu kwani lazima ucheze?
 
Saidia pale unapokuwa na uwezo wa kusaidia wala usiwaze. Ni kama uwekezaji na huyo ndugu yako jua kuwa anakukubali sana na atakuja kukulipa makubwa. Ukiwa una mwambie sina ukiwa nacho msaidie
Usijidanganye ndugu kama hawa wakisikia unashida huwa wanafurahi sana hizi pesa anazompa unaweza kukuta anampa mwanamme mwingine jaribu kuchunguz kama unafanya matumizi sahihi kwanini Kila usiku akwame
 
Next time akija kukuomba pesa muambie Kuna issue unaifanya na hii pesa umeitenga kwa issue hiyo lakini unaweza kumkopesha.

Akirudi tena muambie dada hujarudisha ile pesa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom