Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,707
- 218,255
Wakuu natanguliza Salamu , na baada ya salamu hii naingia moja kwa moja kwenye hoja.
Turudi nyuma kidogo ili tufahamu msingi mkuu wa kuanzishwa kwa hiki kinachoitwa maridhiano kati ya CCM na CHADEMA.
Maridhiano kati ya vyama hivi viwili , kimoja cha dola na kingine cha Wananchi, yalianzishwa kwa ghilba na ccm ili kuudanganya umma kwamba aliyekuwa anafanya unyama kwenye utawala wa awamu ya 5, yaani kuteka, kuua , kubambika kesi na kunyanyasa watu ni Dr Magufuli peke yake, na sasa kwa vile hayupo basi sisi tuliobaki turidhiane, kwamba wale waliokamatwa, waliofungwa, walioonewa, waliodhulumiwa, basi waachiwe ama mali zao zirejeshwe (NEVER AND NEVER AGAIN), na kwa kweli baadhi ya Wahanga wakaanza kuachiwa , wakiwemo viongozi wa Chadema Tunduma.
Nataka kuuthibitishia umma kwamba CHADEMA iliujua huu mpango wa ghilba na ilijua tu kwamba hautadumu, kutokana na ukweli kwamba Unyama uliotendwa haukuwa wa Magufuli peke yake, ulikuwa ni mpango wa ccm yote na vyombo vyao vya dola na watendaji wake, Isipokuwa kilichomponza Magufuli na wachache ni kuwa Front line kwenye unyama huo, huku wengine wakifanyia unyama wao nyuma ya Pazia.
Ushahidi wa karibu wa Jambo hili ni ule wa Kumbambikia Freeman Mbowe kesi ya Ugaidi, Mbowe alibambikwa kesi hii Wakati Magufuli hayupo, hii maana yake ni kwamba Katili ndani ya ccm hakuwa Magufuli peke yake, Ushahidi mwingine wa wazi kabisa ni kupandishwa vyeo watu wote kuanzia Polisi hadi wanaccm waliotumika kufanya unyama kwenye serikali ya awamu ya 5, IGP Wambura, huyu ndiye alikuwa mtengeneza kesi zote za uongo dhidi ya Wapinzani wa serikali, Kingai Byakanwa, Humphrey Polepole, Dr Mahera, Ramadhan Kailima, Kagurumujuli na wengine wengi waliotumika kwenye unyama na kuminya Demokrasia, wamepewa vyeo vya heshima na Serikali ya Samia.
Maridhiano siyo hongo ya kunyamazisha watu wasijadili uchafu wa Bandari na DP WORLD au uchafu mwingine, sasa kwa vile CCM imeamua kutumia watu wale wale waliotumika awamu ya 5 kubambikia watu kesi za Ugaidi na Uhaini ili kuiuzia DP WORLD bandari za Tanganyika, hapa maridhiano hakuna tena.
Nashauri Chadema ijiondoe kwenye Maridhiano hayo haraka, turudi kule kule tulikokuwa, turudi kwa Wananchi ambao ndio wenye nchi, hii ni kwa sababu HAKUNA KITABU CHOCHOTE CHA MUNGU AMBACHO KIMEAGIZA WANADAMU WARIDHIANE NA SHETANI.
Nakala: Freeman Mbowe, John Mnyika
Turudi nyuma kidogo ili tufahamu msingi mkuu wa kuanzishwa kwa hiki kinachoitwa maridhiano kati ya CCM na CHADEMA.
Maridhiano kati ya vyama hivi viwili , kimoja cha dola na kingine cha Wananchi, yalianzishwa kwa ghilba na ccm ili kuudanganya umma kwamba aliyekuwa anafanya unyama kwenye utawala wa awamu ya 5, yaani kuteka, kuua , kubambika kesi na kunyanyasa watu ni Dr Magufuli peke yake, na sasa kwa vile hayupo basi sisi tuliobaki turidhiane, kwamba wale waliokamatwa, waliofungwa, walioonewa, waliodhulumiwa, basi waachiwe ama mali zao zirejeshwe (NEVER AND NEVER AGAIN), na kwa kweli baadhi ya Wahanga wakaanza kuachiwa , wakiwemo viongozi wa Chadema Tunduma.
Nataka kuuthibitishia umma kwamba CHADEMA iliujua huu mpango wa ghilba na ilijua tu kwamba hautadumu, kutokana na ukweli kwamba Unyama uliotendwa haukuwa wa Magufuli peke yake, ulikuwa ni mpango wa ccm yote na vyombo vyao vya dola na watendaji wake, Isipokuwa kilichomponza Magufuli na wachache ni kuwa Front line kwenye unyama huo, huku wengine wakifanyia unyama wao nyuma ya Pazia.
Ushahidi wa karibu wa Jambo hili ni ule wa Kumbambikia Freeman Mbowe kesi ya Ugaidi, Mbowe alibambikwa kesi hii Wakati Magufuli hayupo, hii maana yake ni kwamba Katili ndani ya ccm hakuwa Magufuli peke yake, Ushahidi mwingine wa wazi kabisa ni kupandishwa vyeo watu wote kuanzia Polisi hadi wanaccm waliotumika kufanya unyama kwenye serikali ya awamu ya 5, IGP Wambura, huyu ndiye alikuwa mtengeneza kesi zote za uongo dhidi ya Wapinzani wa serikali, Kingai Byakanwa, Humphrey Polepole, Dr Mahera, Ramadhan Kailima, Kagurumujuli na wengine wengi waliotumika kwenye unyama na kuminya Demokrasia, wamepewa vyeo vya heshima na Serikali ya Samia.
Maridhiano siyo hongo ya kunyamazisha watu wasijadili uchafu wa Bandari na DP WORLD au uchafu mwingine, sasa kwa vile CCM imeamua kutumia watu wale wale waliotumika awamu ya 5 kubambikia watu kesi za Ugaidi na Uhaini ili kuiuzia DP WORLD bandari za Tanganyika, hapa maridhiano hakuna tena.
Nashauri Chadema ijiondoe kwenye Maridhiano hayo haraka, turudi kule kule tulikokuwa, turudi kwa Wananchi ambao ndio wenye nchi, hii ni kwa sababu HAKUNA KITABU CHOCHOTE CHA MUNGU AMBACHO KIMEAGIZA WANADAMU WARIDHIANE NA SHETANI.
Nakala: Freeman Mbowe, John Mnyika