Siku zote nimepuuza kujiunga humu. Msimamo wangu umesababishwa, si tu ya maudhui murua ya mtandao huu, bali shida ya kujibizana na "mizimu". Kwa msaada, leo nimejitahidi kuingia, tena kwa jina langu halisi bila kujificha. Naishi Kwembe-Kati, na kwa kweli mimi ni mmoja wa wazee-ndiyo maana naitwa Mzee wa Kwembe-Kati. Nasema wazi, kila utakaposoma Mzee wa Kwembe-Kati, ujue ni mimi Manyerere Jackton. Simu yangu ni 0759 488 955. e-mail yangu ni
manyererej@hotmail.com.
Nimesoma matusi mengi yanayonilenga. Lakini nashindwa kujibu kwa sababu sijui namjibu nani? Hii ndiyo faida na hasara ya kujibizana na "mizimu". Kudhalilishana, au kushushiana hadhi kwa sababu tu ya Jamhuri imeandika nini, nadhani si sahihi. Lazima tuwe na ustaarabu. Wanaoliandamana Gazeti Jamhuri, hasa la leo, wajaribu kuingia ndani, wasome yaliyomo, na waone msimamo wa Gazeti. Nawakaribisha tubishane hoja za msingi. Matusi, kejeli ay husda haviwezi kuisaidia jamii yetu. Wanaonifahamu vema wanajua sijawahi kuwa mnafiki wala mchumia tumbo. Kwangu mimi, Tanzania na Watanzania ni zaidi ya kila kitu.
Manyerere Jackton
Kwembe-Kati
Dar es Salaam