Ushahidi kuhusu kampuni za mikopo mtandaoni

Ushahidi kuhusu kampuni za mikopo mtandaoni

Poluyakhtov

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2017
Posts
365
Reaction score
306
Habari wana JF,
Ngoja nisonge kwenye mada, kwa kipindi cha miezi ya hivi karibuni nilikumbwa na changamoto iliyohitaji fedha ya haraka. Basi katika pita pita zangu nikaangukia kwenye kampuni za mkopo mtandaoni ambazo ni PesaX pro na Zimacash. Nilikopa na kulipa kwa wakati.

Baada ya hapo nikaanza kupokea sms kutoka namba tofauti tofauti zikinisihi niombe mkopo kupitia app zao. Nilishangaa na nilipojaribu kuuliza namba yangu wameipata wapi?, jibu nililopewa ni kwamba kampuni ya mikopo ni moja isipokuwa wanatumia application tofauti.

Na nilipomwambia mtumaji wa sms kwamba ni kosa kunitumia jumbe za aina hiyo pasi na makubaliano ya kimkataba akawa anajibu kipuuzi. Niwafanyaje ili wapate somo la kutokumlazimisha mtu kukopa.Au nichukue pesa halafu nisiwalipe?
 
Huoni kama wanaingilia taarifa zako za faragha, au akili yako inawaza tu kukopa tu-jisenti tu-chache ambayo hata kununulia shart haitoshi.. 🙂 🙂 .
 
Kwa jinsi walivyo hao usipowalipa utalipiwa tu, wanamfanyia kero ndugu yako atakayeonekana anakerwa na sim zao ndo wanamn'gan'gania mpka analipa
Habari wana JF,
Ngoja nisonge kwenye mada, kwa kipindi cha miezi ya hivi karibuni nilikumbwa na changamoto iliyohitaji fedha ya haraka. Basi katika pita pita zangu nikaangukia kwenye kampuni za mkopo mtandaoni ambazo ni PesaX pro na Zimacash. Nilikopa na kulipa kwa wakati. Baada ya hapo nikaanza kupokea sms kutoka namba tofauti tofauti zikinisihi niombe mkopo kupitia app zao. Nilishangaa na nilipojaribu kuuliza namba yangu wameipata wapi?, jibu nililopewa ni kwamba kampuni ya mikopo ni moja isipokuwa wanatumia application tofauti. Na nilipomwambia mtumaji wa sms kwamba ni kosa kunitumia jumbe za aina hiyo pasi na makubaliano ya kimkataba akawa anajibu kipuuzi. Niwafanyaje ili wapate somo la kutokumlazimisha mtu kukopa.Au nichukue pesa halafu nisiwalipe?
Nilishawah kuwa na experience mbovu nao nikawakataa na sikuwah kuwasimbua kuwalipa. Wakaanza kunipigia kuniomba niwakope nikawaosha
 
FB_IMG_17399519815745160.jpg
 
Huoni kama wanaingilia taarifa zako za faragha, au akili yako inawaza tu kukopa tu-jisenti tu-chache ambayo hata kununulia shart haitoshi.. 🙂 🙂 .
Upo sahihi, na hilo swali nikishawauliza lakini majibu yao ni kama vile kuna wanachoringia.
 
Ile mikopo hapana, riba kubwa sana.
Mkopo wa 50,000 unarudisha 69,000 kwa siku 5!
 
Upo sahihi, na hilo swali nikishawauliza lakini majibu yao ni kama vile kuna wanachoringia.
Wana ringa kwa sababu tayari wamepata access ya kuingia kwenye mfumo wako wa simu, hivyo tayari wamesha kusanya taarifa zako kwa usahihi, ukizingua tu wataanza kuziweka taarifa zako wazi.. 😊😊
 
Wana ringa kwa sababu tayari wamepata access ya kuingia kwenye mfumo wako wa simu, hivyo tayari wamesha kusanya taarifa zako kwa usahihi, ukizingua tu wataanza kuziweka taarifa zako

Wana ringa kwa sababu tayari wamepata access ya kuingia kwenye mfumo wako wa simu, hivyo tayari wamesha kusanya taarifa zako kwa usahihi, ukizingua tu wataanza kuziweka taarifa zako wazi.. 😊😊
Hawanidai chochote mkuu bali wananishawishi nichukue mkopo.
 
M
Ile mikopo hapana, riba kubwa sana.
Mkopo wa 50,000 unarudisha 69,000 kwa siku 5!
Nimeingia mgodi ni zaidi ya songesha.
WamenipA 43k first time na nitarejesha 53k within a month sio mbaya , hii inaweza ikakuokoa mahala umebanwa , mara ATM haipo karibu , mara sijui ni nini kimekwama vile so inakuokoa fasta, wananiambia nilipe kabla ya muda Halafu nikope 84k , ishu ni kuwa mwaminifu , wanakuwa Kama mshkaji wako anakusaidia hela fasta unapokwama , uaminifu ni bidhaa adimu nowdays kwa binadamu,yaani ni zaidi ya gold
 
M

Nimeingia mgodi ni zaidi ya songesha.
WamenipA 43k first time na nitarejesha 53k within a month sio mbaya , hii inaweza ikakuokoa mahala umebanwa , mara ATM haipo karibu , mara sijui ni nini kimekwama vile so inakuokoa fasta, wananiambia nilipe kabla ya muda Halafu nikope 84k , ishu ni kuwa mwaminifu , wanakuwa Kama mshkaji wako anakusaidia hela fasta unapokwama , uaminifu ni bidhaa adimu nowdays kwa binadamu,yaani ni zaidi ya gold
Ni kweli huwa wanaokoa sana ukiwa na shida ya dharura.
Mfano mgodi wako poa mimi nakopa mpaka 115,000 riba yao nadhani ni zaidi ya 20% ila haivuki 27% kwa mwezi. Uzuri unapata muda wa kujipanga. Ukishindwa kuna kuomba kuongeza muda wa mwezi mmoja ila kuna gharama.

NMB wamenianzia na 39,000 nitarudisha 43,000 kwa wiki mbili ni riba himilivu.

Songesha wanasema naweza kuchukua 24,000 ila sitaki ule hauna maana.

Hao flex cash walinipigia simu kabisa kwamba naweza kuchukua mkopo wa 68,000 nilikataa.
 
Ni kweli huwa wanaokoa sana ukiwa na shida ya dharura.
Mfano mgodi wako poa mimi nakopa mpaka 115,000 riba yao nadhani ni zaidi ya 20% ila haivuki 27% kwa mwezi. Uzuri unapata muda wa kujipanga. Ukishindwa kuna kuomba kuongeza muda wa mwezi mmoja ila kuna gharama.

NMB wamenianzia na 39,000 nitarudisha 43,000 kwa wiki mbili ni riba himilivu.

Songesha wanasema naweza kuchukua 24,000 ila sitaki ule hauna maana.

Hao flex cash walinipigia simu kabisa kwamba naweza kuchukua mkopo wa 68,000 nilikataa.
Mie huu mgodi nilijaribu wakanipa sema songesha ni Kama vile ni hela zako tu unawekeza unaanza kuzikopa sema ziko kwao, wao Wana hofu mno ya ku loose so wanakopesha kidogo kidogo mno pia na riba Iko juu mno
 
Ni kweli huwa wanaokoa sana ukiwa na shida ya dharura.
Mfano mgodi wako poa mimi nakopa mpaka 115,000 riba yao nadhani ni zaidi ya 20% ila haivuki 27% kwa mwezi. Uzuri unapata muda wa kujipanga. Ukishindwa kuna kuomba kuongeza muda wa mwezi mmoja ila kuna gharama.

NMB wamenianzia na 39,000 nitarudisha 43,000 kwa wiki mbili ni riba himilivu.

Songesha wanasema naweza kuchukua 24,000 ila sitaki ule hauna maana.

Hao flex cash walinipigia simu kabisa kwamba naweza kuchukua mkopo wa 68,000 nilikataa.
Mbona unakopa vijipesa vidogo vidogo hivyo?ni njaa au ni nini?
 
Mbona unakopa vijipesa vidogo vidogo hivyo?ni njaa au ni nini?
Huamui wewe kukopa bei fulani, wao ndio wanakuanzishia kiasi fulani.
Halafu unaposema ni vipesa vidogo ni kweli tumetofautiana uchumi inawezekana ni njaa. Na ndio maana NMB walitulenga wenye njaa kuanzia TZS 1,000 hadi 1,000,000.
Sisi wengine 40,000 au hiyo 100,000 wanayotukopesha ni kubwa sana inatuwezesha kutuokoa kwenye dharura.
 
Back
Top Bottom