Sasa anataka watu waamini kuwa zanzibar haiwezi kujifanyia lolote bila ya muungano, huu ni upuuzi kabisa, kwani wazanzibar walilazimishwa kuingia katika muungano kwasababu ya umasikini? au haikuweza kujiendiesha wenyewe kiuchumi kabla ya muungano? hii ni kuficha ukweli kwa makusudi, kwasababu ni muungano unaowatia ufukara wazanzibari kwa kuwabana katika kupata fursa za kimaendeleo na kujiinua kiuchumi.
Kabla ya muungano huu wa kifisadi, uwezo wa zanzibar kiuchumi ulikuwa mkubwa kuliko wa Tanganyika na kuna kumbukumbu sahihi za kihistoria zinazoonyesha jinsi zanzibar ilivyowahi hata kutoa misaada ya kiuchumi kwa nchi kama Yemen na hata jirani zao wati huo Tanganyika.Sasa kama nchi inaweza kutoa msaada wa kiuchumi kwa nchi nyengine tena wa ghafla wakati wa maafa, ndo itakua na uchumi mdogo utakaohitaji iungane na nchi nyengine kujiendesha? Leo tujiulize uwezo ule umepotelea wapi? Malyamkono anawazuga "vichwa Panzi" kama yeye. zanzibar licha ya udogo wake na rasilimali zake kuwa chache, historia inaonyesha kuwa iliwahi kujieneza katika mtandao wa kibiashara uliounganisha nchi zote za bahari ya hindi, leo uhusiano huo mkubwa uliowahi kuiinua kibiashara na kukuza uchumi wa zanzibar inaukumbuka kupitia TAMASHA LA MAJAHAZI tu, ni ufisadi unaoitwa "Mapinduzi matukufu ya 1964" na "muungano wa 1964" umezima na kufisidi maendeleo hayo, na leo wanaibuka "vichwa Panzi" kama hawa wanaojiita Maprofesa, kutwambia eti bila ya muungano zanzibar ita suffer kiuchumi, ah! this is absurd... angenambia maneno kama haya mbele yangu ningemchapa kofi.