Usanifu wa Lugha umepotea

Usanifu wa Lugha umepotea

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,695
Reaction score
49,945
Wakati mwingine nikisoma maandiko mbali mbali huwa najiuliza ule usanifu wa Lugha waliokuwa nao mababu zetu na wale manju waliosifika zamani umekwenda wapi? Hata nyimbo zinazotungwa siku hizi zina ukakasi sana wa lugha kiasi kwamba inahitji uvumilivu kuzisikiliza. Tatizo letu ni nini hasa, tuna upungufu wa misamiati ya Lugha ya Kiswahili au weledi wetu katika kusanifu lugha ni mdogo?

Wakati mwingine, Ashakum si matusi, huwa najiuliza hivi hawa vijana wa siku hizi wanapotongoza huwa wanatumia maneno ya aina gani? au ndiyo mambo ya "Inakuwaje?" au "vipi baadaye una nafasi?". Ukimsikiliza bi Shakila kwenye ule wimbo wa "Kifo cha mahaba" au "Macho yanacheka, moyo unalia" unapata starehe ya fikra kiasi kwamba ni mwenza mwenye moyo mgumu tu asiyeweza kuguswa na nyimbo hizo. Zama hizi kimetokea nini?

Sasa soma vitabu, hadithi za kwenye magazeti, au uandishi wa kawaida kabisa ndiyo balaa. Kuna jama yangu ni mhadhiri kwenye chuo fulani cha umma,ameniambia ukiwapa vijana wa siku hizi Karatasi wakuandike historia za maisha yao wenyewe, kisha uwaambie zifikie kurasa tano, basi kama ni Mwalimu au Mhadhiri utanuniwa Mwezi mzima. Hata historia za maisha yao hawana maneno ya kuzielezea!?

Kwa nini uwezo wetu wa kusanifu Lugha umepotea?


Preta wewe ni wa kizazi hiki hebu tusaidie!!
 
Kama tungelikuwa tunaitunuku lugha yetu basi na tungeliifanya iwe lugha kuu katika nyanja kuu zote.

Na sehemu pekee ambayo ingefanya lugha yetu ipate chachu ya kukuwa basi ni elimu.

Niliwahi kumuuliza kijana aliyemaliza kidato cha tano anipe maana ya fanani na hadhira, majawabu na maelezo aliyonipatia, yalinifanya niondoke na fikra hasi juu ya elimu yetu
 
Mambo yamebadirika,huwezi ukataka kina Diamond waimbe kama zamani.
 
mcubic una hoja ya maana sana, lakini huu mjadala wakati fulani nilivutiwa na hoja zilizokuwa zinatolewa na Jenerali Ulimwengu kwamba kuna tofauti kubwa sana kati ya Elimu na Lugha ya kufundishia Elimu. Bahati mbaya sana sisi Lugha ya kufundishia elimu tunaona ndiyo elimu yenyewe. Mtu akijua Kiingereza basi ndiyo tunamuona ana elimu kubwa sana!

Kuna watu wanataka mpaka leo tuione lugha ya Kiingereza kama ndiyo "utaalam" wenyewe. Utawasikia "kwa lugha ya Kitaalam, inaitwa Grand canyon". Kwa mfano watu wengi hawajui kwamba teknolojia ni kutumia sayansi kutengenezea zana za kurahisishia maisha ya mwanadamu, teknolojia siyo lugha ya Kiingereza. Gari linatengenezwa na Mjapani anayejua kiingereza cha kubabia, linakuja kuendeshwa na mtanzania aliyeishia darasa la pili hajui kusoma wala kuandika hata lugha yake ya asili ya Kiswahili. Hapo lugha ya kitaalamu ipo wapi?
 
Back
Top Bottom