Usalama wa Daraja la mto Wami umezingatiwa?

Usalama wa Daraja la mto Wami umezingatiwa?

and 998 others

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2012
Posts
28,227
Reaction score
39,713
Daraja la mto Wami pamoja na umuhimu wake katika sekta nzima ya usafiri hususani kuunganisha nchi ya Tanzania na mikoa ya kaskazini na nchi jirani za Kenya, Uganda, Somalia, Sudan kusini n.k. Hofu yangu kuu ni wembamba wake/daraja (inayopelekea kusubiriana). Kwa nini kusiongezwe upana na uimara kama daraja la MKAPA kuepusha majanga yanayoepukika?
**UPDATE**
Ujenzi wa njia/daraja jipya unaendelea. Tunapongeza kwa jitihada hizi
 
Niliulizia nkaambiwa lina zaidi ya miaka 50 siku chache baada ya uhuru ndio lilizinduliwa,kiukweli limepitwa na wakati na hili lipo chini ya TANROAD ni suala la kutenga budget tu kwan wote tunajua uchakavu wa daraja,utapita kote umelala ila ukifika hapo unaamka sababu tu roho zinajua ni eneo la kifo
 
Ndugu joshua Hofu yangu zaidi ni kwa malori ikitokea likakosa breki likakukuta unasubiria mwenzio apite darajani litakusukumizia mtoni ukaliwe na mamba huko

Mkuu umegusa mlemle si kuna ajali ya lori ilitokea hapo kwenye mwezi wa 12 baada ya kufel breki na kuja kuiliparamia basi palepale darajan au umesahau?
 
Pale linasubiriwa janga zaidi ya MV BUKOBA, ni hatari sana kile kidaraja aisee. Hivi pale chini kuna nguzo hata ya ku-support hicho kidaraja?
 
Dah pale kwakweli daraja linahitaji kupanuliwa.Kiusalama (safety)wewe umeona kitu kinaitwa "near miss".Umaskini wetu pale ingepigwa suspended bridge kutoka upande mmoja kwenye mwingine kuua huo mlima unaosumbua malori
 
nilishangaa walipoleta hoja eti wanataka kujenga daraja kuunganisha zazibar na bara wakati la wami limewashinda,zanzibar bara kl70,wami mita100????
 
Niliwai kusikia lengo la kujengwa vile ni mahsusi kwa gari moja tuu ili uzito usizidi na kusababisha ajali...hata hivyo ni bora walifanyie matengenezo hilohilo coz wakijenga lingine upya ndo itakua hatari zaidi maana naamini halitakuwa na ubora kabisa (mvua kidogo tu litavunjika)kwa navyoijua serikali yangu sikivu
 
kiukweli, ajali nyingi pale wami zinasabishwa na daraja. Maana dereva anawaza mteremko mkali pamoja na zamu ya upitaji darajan.
 
Back
Top Bottom