Usahihi: Mazungumzo yanaendelea vizuri

Usahihi: Mazungumzo yanaendelea vizuri

Kama mkimuacha Lowasa msijidanganye na kudanganya watu! Uraisi ni ndoto kwa upinzani,wala sipotezi muda wangu kwenda kupigia kura upunzani bora nibaki home tu.

Nyie ndio masalia ya Team Lowassa mliojeruhiwa juzi Dom??? poleni sana
 
Asichofahamu Makene na anachofahamu Dr Slaa ni kwamba Mtei, Ndesamburo, Mbowe na Mbatia ni TeamLowasa hivyo mbele ya Lowasa Dr slaa si lolote. Kwahiyo yule Lizaboni yawezekana kabisa yuko sahihi.
 
Makene, CHADEMA nyie ni waongo kuanzia wewe wa kwenye nyasi hadi Mtei. Mliwahi kukanusha haya kuwa siyo ya kweli kumbe ni kweli, wizi mtupu
View attachment 267977View attachment 267977View attachment 267977

Tunajua kwamba CCM na wapambe wake mngependa sana CDM idondokee PUA kwa kumkaribisha FISADI wenu ambaye mwaka 2005 na 2010 ndiyo aliyewasaidia kuingi IKULU,leo mnamuona hana maana sababu ya hali yake TETE,kweli nimeamini MNAFIKI haachi ASILI yake.

Siasa chafu mlizomfanyia Salim Ahmed Salim mliwahi hata kumuomba radhi?Msipende kufanya siasa chafu.

Na pia mnajua fika watanzania wengi wameanza kuiamini CDM ,na mnajua wakikiuka tu yale matarajio ya wengi ya kupiga vita ubadhirifu wa mali ya umma kwa kumpokea mtu ambaye alitumia vibaya nafasi yake kama kiongozi inakuwaje?Watamwambia nini Mwanachama wa kawaida?

Tunajua huko CCM hata huyo anayemnyooshea mwenzie vidole aliingia kwa siasa chafu na pesa nyingi ilimwagwa.!!!!!!!!!Na leo tunashuhudia RUSHWA,UFISADI,UDINI,WIZI wa MALI ZA UMMA,MADAWA YA KULEVYA,UKABILA/UKANDA ukiongezeka kwa kasi kubwa kwa sababu ya udhaifu na ulegelege wa kiongozi aliyeingia madarakani kwa mshindo ule ule leo anaoupigia kelele.Hawezi kumkemea Kijana wake wala MAKADA wake kwa kueneza ukanda ,ukabila na udini! Sababu anajua ndivyo vilivyomuweka hapo.

Mara nyingi tumemsikia Nape Nnauye na Ridhiwani wakiongelea ukanda eti watu wa kaskazini hawawezi kamwe kuwa marais mpaka na kiapo eti over his dead body................

Sasa nadhani hawa wote hawajui Geography,jamani Kilimanjaro siyo kaskazini,Kilimanjaro ni Kaskaz-Mashariki,na huko kwa Magufuli ndiko hasa KASKAZINI,jamani hata jiografia ya darasa la nne pia imewashinda??

Na mwisho hakuna mtu aliyeiumba TANZANIA siyo wanachama wa CCM ,watoto wao,au binadamu yeyote na hivyo kila raia mtanzania mwenye sifa bila kujali KABILA,DINI,UKANDA atokao wanahaki ya msingi ya kugombea na kuchaguliwa kuwa viongozi wakuu wa TANZANIA yetu.

Tanzania yetu sote siyo ya wanaccm tu,na uzuri rais wenu kasem....'Hata huko kwa wapinzani wako watu wazuri zaidi kuliko CCM wenye uwezo na sifa za kuongoza TAIFA letu"

Tuwe fair kwa kila kitu tukifanyacho,for once tuache siasa za chuki,siasa chafu, siasa za visasi hazitatupeleka kokote.Tuwaache watanzania wachague kiongozi/viongozi wanaoona watatupeleka kule tukutakako.
 
Asichofahamu Makene na anachofahamu Dr Slaa ni kwamba Mtei, Ndesamburo, Mbowe na Mbatia ni TeamLowasa hivyo mbele ya Lowasa Dr slaa si lolote. Kwahiyo yule Lizaboni yawezekana kabisa yuko sahihi.

Sema usichfahamu wewe kuwa CDM siyo chama cha kifamilia kama CCM.NA hilo ni kutokana na statement ya Mwenyekiti wenu ...'URAIS wake ni wa kwake na familia yake"

CDM ni independent entity,hatuhitaji MAFISADI tunataka Tanzania huru .Na Tanzania bila CCM/LOWASSA inawezekana.

Acheni siasa chafu.............Tuacheni watanzania tuchague kwa uhuru.Hata huyo Magufuli ni mwizi kama hao wengine.CCM wote ni kambare waishio kwenye tope tu.Msiwapake matope wengine.Bakini huko huko.
 
Nyie ndio masalia ya Team Lowassa mliojeruhiwa juzi Dom??? poleni sana
Vyovyote usemavyo ukweli unabaki palepale Slaa hana uwezo wa kuishinda Ccm. Kama unabisha subiri uone atakavyoangukia pua. Hanajipya la kuwaambia wa TZ. Uzee nao umemmaliza kabisaa.
 
Haya ni mashairi ya alinacha. Ufundi wa lugha wa makene anayetegemea kula kwa kupindisha ukweli wa mambo
Nyie si mmeshampata mgombea wenu na mnasema anakubalika kama maji ya uhai, na leo mnamtambulisha kwa wakazi wa Dar es Salaa!? Sasa mnafuata nini huku badala ya kumtambulisha mtu wenu!?
 
Nawaombea Mungu viongozi wenu wa UKAWA waongonzwe na roho wa bwana waje na kauli moja...wapenda mabadiriko wotee tutawaunga mkono...
ccm ni sawa na gari bovu kumbadirisha dereva sio kigezo cha gari kuendelea na safari....so tunahitaji kubadirisha gari kununua mpya na kutoa gari bovu(mfumo fisadiii hata naye mapombe makufuli atakuwa fisadii tuuu)
 
Asichofahamu Makene na anachofahamu Dr Slaa ni kwamba Mtei, Ndesamburo, Mbowe na Mbatia ni TeamLowasa hivyo mbele ya Lowasa Dr slaa si lolote. Kwahiyo yule Lizaboni yawezekana kabisa yuko sahihi.

Hii comment inachekesha kweli. Uhuru wa maoni wakati mwingine hugeuka kuwa very funny thing.

Hivi bado huwa mnayo hiyo kete kudhani mnaweza kuyumbisha CHADEMA kwa kutunga maneno ya mgawanyiko kati ya Viongozi wakuu?

Hiyo ni hadhi ya CCM ambako Kinana alihutubia mkutano wa hadhara Mwanza akatoa maagizo ambayo si tu Mkiti wake alifanya tofauti bali hata wabunge hawakutii. Wakapitisha mswada wa kifisadi Bungeni.

Kama una hamu na mgawanyiko wa ndani ya Chama waulize CCM wanaopumulia mitambo kwa sasa.
 
Vyovyote usemavyo ukweli unabaki palepale Slaa hana uwezo wa kuishinda Ccm. Kama unabisha subiri uone atakavyoangukia pua. Hanajipya la kuwaambia wa TZ. Uzee nao umemmaliza kabisaa.

Unatumbusha namna ambavyo NEC walilazimika kufuta website yao kwa sababu walijua matokeo yalikuwa too questionable kumtangaza mgombea wa CCM.
 
Back
Top Bottom