Urais CCM: Hofu ya uasi yatanda

Urais CCM: Hofu ya uasi yatanda

Habari za uzushi kwa vile hii habari inaihusu CCM au habari za uzushi kwa vile sio CDM iliyoshambuliwa?
Pengine uelewi profile yangu. Mimi siyo mtu wa chadema au ccm. Sijafungwa na mahaba ya kivyama kutokuona habari za uzushi na nyekundi kuiita nyeupe na nyeupe kuiita nyekundu!
 
?Hizi habar zinaandikwa kwenye magazeti na watanzania wanazisoma ila mwisho wa siku wanawachagua hao jamaa,,,,,,mtu anatumia mamilioni ya pesa kuwapa watu wakahonge ili achaguliwe,sasa hayo mambo ya ufisadi tutaacha kuyaskia kweli/
 
wasiwasi wangu katika hili ni kuwa kama watu wanatumia nguvu ya pesa katika kutafuta kura nini maana yake atakapopata nafasi hiyo. mwalimu aliwahi kusema ya kuwa ikuli ni mahali patakatifu ni sehemu ambayo inahitaji kuheshimiwa sasa kama leo watu wanaanza kufanya kinyume nas kile ambacho mwalimu alikuwa anakataa maana yake ni kuwa watu wanaangalia maisha yao peke yao na wala siyo maisha ya watanzania

Nilitaka kujibu kitu lakini nikaacha nisijepigwa ban bure
 
Wanaccm wenzangu mwaka huu kula ni ccm lakini kura ni UKAWA tusiliangamize taifa kwa ajili ya chama. Hata Mwl.Nyerere alisema "ccm sio mama yangu" pia alisema "watz wanahitaji mabadiliko wasipopata mabadiliko ndani ya ccm watayatafuta nje ya ccm"
Swali je tunategemea mabadiliko yoyote kutoka ccm? Jibu ni Hapana.
Kwaiyo inabidi yapatikane nje ya ccm.
 
Mwaka huu Mzee wa Monduli atawatoa kamasi. Mlimtengenezea zengwe la Richmond likabuma. Leo hii mnakuja na propaganda nyepesi. Hatudanganyiki ngoo!
 
Watanzania tulio wengi tunajiuliza ni lipi lengo la huyu Lowassa kutaka kwa nguvu zote kuingia Ikulu, ni kuwatumikia wananchi? Kukitumikia chama chake? Au ni kwa ajili ya maslahi yake binafsi??? Lowassa ana lipi jipya na unique la kuifanyia nchi hii???

Iko wazi, Lowassa ni mwizi na fisadi aliekubuhu...Watanzania tunapaswa kumuogopa mtu huyu???

Lowassa anataka tu kuweka historia kuwa aliwahi kuwa rais.
 
Mzee wa Monduli inaelekea hana mpango wa kujitoa. CCM wana kazi mwaka huu!!
 
Watanzania tulio wengi tunajiuliza ni lipi lengo la huyu Lowassa kutaka kwa nguvu zote kuingia Ikulu, ni kuwatumikia wananchi? Kukitumikia chama chake? Au ni kwa ajili ya maslahi yake binafsi??? Lowassa ana lipi jipya na unique la kuifanyia nchi hii???

Iko wazi, Lowassa ni mwizi na fisadi aliekubuhu...Watanzania tunapaswa kumuogopa mtu huyu???
kwanza una hakika aneyeongelewa ni EL?
Pili,kuna ushahidi wa hayo mambo yanayoongelewa kwenye hilo gazeti na mitandaoni?
Tatu,kwa nini iwe ni ngumu kupata ushahidi hata mmoja tu wa tuhuma hizi za rushwa kwa wanaoutaka uraisi kwa tiketi ya CCM wakati iliwezekana kupata ushahidi wa rushwa kubwa kadhaa kama ESCROW?
Mwisho,kwa nini hata wale "key players" wa watia nia hawatoi ushahidi wa "foul plays" zinazofanywa na pande pinzani ilhali wao wanajitanabahisha kuwa na "ushirikiano" mkubwa na watu wa vyombo vya usalama?
Kama kweli kabisa hakuna kambi ambayo inaweza kupata ushahidi japo kidogo usio na shaka,je kweli hao watu watu wanauwezo wa kutuongoza kweli au wote wanaogopa ya "mwaga mboga nimwage ugali" kwa kuwa wote ni "foul players"?
 
huyu anatakiwa avuliwe uanachama ili chama kiweze kuendeshwa bila mihemuko

Jifunzeni kwa CHADEMA. waliovowafanya na wakala wenu ZITO KABWE, hawakuogopa kwamba ata influence negatively. Walichukua hatua sahihi na bila kumpa nafasi ya kufanya uharibifu zaidi. Chama si mtu. Leo Zito hayupo, CHADEMA kimekuwa na kuimarika wa kiwango na kulia fedha, ana mikataba. Kama ninyi mtamwogopa, mwacheni kwenye chama lakini kwenye uraisi asahau. Na ccm chatu haipewi uraisi Tanzania!.[/QUOTE]
Well presented. Big up.
 
Maccm yanaangaika sana kubaki ikulu lakini ukweli unabaki palepale kuwa mwaka huu ndo mwisho wao. Acha walane wao kwa wao, ukawa waingie ikulu.
 
Ccm inahitaji kukaa kando ili ijitathmini na kujiweka upande wa taifa badala ya kukimbilia ikulu wakati imebeba silaha za kulimaliza taifa.

Mtu yeyote anayekula njama, na kupanga hila za kuhujumu haki na kweli kwenye chama chake, na kutumia njiia haramu za kushinikiza yeye ndiye awe the best candidate huku akijua siyo, anatakiwa kwanza chama kimfikishe kwenye idara za nidhamu ya chama ili ajitetee na kuonywa ikiwa itabainika amekosea bahati mbaya.

Lakini pale inapokuwa bayana kwamba ni mafia, anatumia kila njia halal na haramu ikiwemo rushwa, vurugu na kushawishi uasi ulio kinyume cha sheria, lengo lake likiwa ni kutafuta uongozi, huyu anatakiwa avuliwe uanachama ili chama kiweze kuendeshwa bila mihemuko ya ugaidi na uhaini wa ndani.


Huyo mtu anayetumia hila, uwongo, rushwa, fitina, udanganyifu na vitisho kwenye chama chake, chama chake kikimwogopa, ni dhahiri chama hicho ni dhaifu na moja kwa moja kinajiondolea sifa ya kukabiliana na changamoto kubwa zilizopo na zinazoweza kujitokeza. Kwa mtaji huo, Watanzania hawanasababu ya kuchagua chama chenye woga wa kipum.bavu wakati ambao wimbo wetu ni kupata uongozi imara.

Kama lowasa atawatisha kwa fedha zake na za kutoka nje, huku akijua na dunia ikijua hana sifa ya kuwa raisi, lakini kwa woga wa ccm wakamwogopa na kumptisha, hiyo ccm itaongozaje nchi wakati taifa linatishiwa na changamoto ambazo hazijawahi kuwepo kutoka ndani na nje ya nchi? Kwa hiyo kila atakaye black mail, ama kujitunishia misuli, ccm hiyo kwa woga itaridhia matakwa yake hata kama yako kinyume na kweli. Huyo Lowasa, atakapokuwa raisi kwa nguvu ya rushwa, ama kwa woga wa ccm, nani atahakikisha anasimamia maslahi ya taifa, wakati atakuwa tayari keshatangaza ubabe na chama chake hakina uwezo wa kumsimamia wala kumdhibiti?


Ninasema tena, Tanzania inahitaji uongozi imara na safi. Ccm ina makandokando mengi na kamwe kwa sababu yoyote, msije mkafanya kosa la kusimamisha fisadi linalokataliwa na kila mtu, kwa kuwa limetumia rushwa na ushawishi haramu, nanyi mkaliogopa mkasuribi hadi liwamalize, na kuwaondoa kwenye utaratibu, mbaki mnapiga miayo.

Jifunzeni kwa CHADEMA. waliovowafanya na wakala wenu ZITO KABWE, hawakuogopa kwamba ata influence negatively. Walichukua hatua sahihi na bila kumpa nafasi ya kufanya uharibifu zaidi. Chama si mtu. Leo Zito hayupo, CHADEMA kimekuwa na kuimarika wa kiwango na kasi haijawahi kuwepo.

Ccm mwondoeni huyo fisadi na mfitini miongoni mwenu. Hana nguvu wala sera yoyote zaidi ya tamaa na ubinafsi. Inawezekana pia anapigana kwenda ikulu kwa sababu huko anakochukulia fedha, ana mikataba. Kama ninyi mtamwogopa, mwacheni kwenye chama lakini kwenye uraisi asahau. Na ccm chatu haipewi uraisi Tanzania!.
mkuu kwa mbaaali nakuona kama bado unakaimani kama zimwi ccm kuendelea kutawala Tanzania .binafsi sioni Rais ccm si Makongoro si Lowasa.ndege wanaofanana huruka pamoja mkuu(hao tofauti Yao ni majina tu ila hulka zao ni sawa)
 
Watanzania tulio wengi tunajiuliza ni lipi lengo la huyu Lowassa kutaka kwa nguvu zote kuingia Ikulu, ni kuwatumikia wananchi? Kukitumikia chama chake? Au ni kwa ajili ya maslahi yake binafsi??? Lowassa ana lipi jipya na unique la kuifanyia nchi hii???

Iko wazi, Lowassa ni mwizi na fisadi aliekubuhu...Watanzania tunapaswa kumuogopa mtu huyu???

Mtu anayeenda ikulu kwa kutoa fedha aogopwe kama ukoma.
 
Watanzania tulio wengi tunajiuliza ni lipi lengo la huyu Lowassa kutaka kwa nguvu zote kuingia Ikulu, ni kuwatumikia wananchi? Kukitumikia chama chake? Au ni kwa ajili ya maslahi yake binafsi??? Lowassa ana lipi jipya na unique la kuifanyia nchi hii???

Iko wazi, Lowassa ni mwizi na fisadi aliekubuhu...Watanzania tunapaswa kumuogopa mtu huyu???
jk aliutafuta urais kwa style hiii hii,mpaka wazee wetu wengine wakaitwa Hezbollah,matokeo yake si unayaona?Tanzania ni kama paradiso sasa chezea committed people wewe
 
Hakuna wa kuitoa ccm makini ikulu acheni ndoto za mchana labda kama mnajifariji tu
sisiem makini kwa lipi!? Nisaidie ndugu yangu! Huo umakini uko wapi!!! Acha kutuchora au nawe ni mmoja wao?
 
Back
Top Bottom