Ccm inahitaji kukaa kando ili ijitathmini na kujiweka upande wa taifa badala ya kukimbilia ikulu wakati imebeba silaha za kulimaliza taifa.
Mtu yeyote anayekula njama, na kupanga hila za kuhujumu haki na kweli kwenye chama chake, na kutumia njiia haramu za kushinikiza yeye ndiye awe the best candidate huku akijua siyo, anatakiwa kwanza chama kimfikishe kwenye idara za nidhamu ya chama ili ajitetee na kuonywa ikiwa itabainika amekosea bahati mbaya.
Lakini pale inapokuwa bayana kwamba ni mafia, anatumia kila njia halal na haramu ikiwemo rushwa, vurugu na kushawishi uasi ulio kinyume cha sheria, lengo lake likiwa ni kutafuta uongozi, huyu anatakiwa avuliwe uanachama ili chama kiweze kuendeshwa bila mihemuko ya ugaidi na uhaini wa ndani.
Huyo mtu anayetumia hila, uwongo, rushwa, fitina, udanganyifu na vitisho kwenye chama chake, chama chake kikimwogopa, ni dhahiri chama hicho ni dhaifu na moja kwa moja kinajiondolea sifa ya kukabiliana na changamoto kubwa zilizopo na zinazoweza kujitokeza. Kwa mtaji huo, Watanzania hawanasababu ya kuchagua chama chenye woga wa kipum.bavu wakati ambao wimbo wetu ni kupata uongozi imara.
Kama lowasa atawatisha kwa fedha zake na za kutoka nje, huku akijua na dunia ikijua hana sifa ya kuwa raisi, lakini kwa woga wa ccm wakamwogopa na kumptisha, hiyo ccm itaongozaje nchi wakati taifa linatishiwa na changamoto ambazo hazijawahi kuwepo kutoka ndani na nje ya nchi? Kwa hiyo kila atakaye black mail, ama kujitunishia misuli, ccm hiyo kwa woga itaridhia matakwa yake hata kama yako kinyume na kweli. Huyo Lowasa, atakapokuwa raisi kwa nguvu ya rushwa, ama kwa woga wa ccm, nani atahakikisha anasimamia maslahi ya taifa, wakati atakuwa tayari keshatangaza ubabe na chama chake hakina uwezo wa kumsimamia wala kumdhibiti?
Ninasema tena, Tanzania inahitaji uongozi imara na safi. Ccm ina makandokando mengi na kamwe kwa sababu yoyote, msije mkafanya kosa la kusimamisha fisadi linalokataliwa na kila mtu, kwa kuwa limetumia rushwa na ushawishi haramu, nanyi mkaliogopa mkasuribi hadi liwamalize, na kuwaondoa kwenye utaratibu, mbaki mnapiga miayo.
Jifunzeni kwa CHADEMA. waliovowafanya na wakala wenu ZITO KABWE, hawakuogopa kwamba ata influence negatively. Walichukua hatua sahihi na bila kumpa nafasi ya kufanya uharibifu zaidi. Chama si mtu. Leo Zito hayupo, CHADEMA kimekuwa na kuimarika wa kiwango na kasi haijawahi kuwepo.
Ccm mwondoeni huyo fisadi na mfitini miongoni mwenu. Hana nguvu wala sera yoyote zaidi ya tamaa na ubinafsi. Inawezekana pia anapigana kwenda ikulu kwa sababu huko anakochukulia fedha, ana mikataba. Kama ninyi mtamwogopa, mwacheni kwenye chama lakini kwenye uraisi asahau. Na ccm chatu haipewi uraisi Tanzania!.