Urais 2015: Khamis Mgeja atema cheche

Urais 2015: Khamis Mgeja atema cheche

Mkuu hakuna kuhariri hapo. Nimecheka sana kuona kinaitwa chama chetu cha ccm, badala ya chama cha mapinduzi.

Kwani yeye sii ni mwana ccm or.... Issue kubwa hapo ni ujumbe kwa hao wahuni na wakora ndani ya chama
 
Tokea lini kawa mtumishi wa Lowassa, acha kuongea kama mwanamke mpumbavu (mke wa Ayubu)...... Nape hana cha kupoteza ndani ya ccm kwa sababu ana chama alichokianzisha ccj.....

Nyie wagonjwa wa Lowassamania mkiambiwa ukweli mnabwabaja matusi. Haiwasaidii na wala haimsaidii Lowassa wenu. Dada wa NSSF unapakatwa nini? Hakuna asiyejua kuwa Khamis Mgeja yuko kwenye payroll ya Lowassa kumfanyia kampeni urais kwa miaka mingi sasa.
 
Swala siyo yuko kundi gani, issue kubwa ni uhai wa chama..... Au wewe ni chadema nini, unataka ccm ife babu Slaa achukue nchi.....

Kwani CCM ni Mama yangu? (....by JKN)

Unadhani ni dhambi ya mauti endapo Mtanzania mwingine yeyote kutoka nje ya chama chenu akichukua usukani wa kutuongoza na kutuvusha?
 
Kuwadi mkubwa na mpiga vuvuzela namba moja,umejaza unaa na fitina zisizosemeka, ww mgeja Unamwambia nani hayo maneno ya kutungiwa? Hv kuna shda gani nape kusema ccm haitomsimamisha mtu mchafu? Huyo anayekutekenya kama ni usafi unajichekesha nn??!? Toeni laana na MUNGU anamfaham next ceo wa tz toka mihemko hapa,
 
Kazi iko, mwenyekiti wa mkoa comrade Mgeja anajitaji kujifunza "Technical writing" kujua ni wapi utumie koma, kituo, au herufi kubwa.
 
Una uwakika na hilo mkuu....

Nape Nnauye ni janga ndani ya CCM. Madudu yako yangu akiwa chuo wanafahamika na siku moja tutayaanika humu jamii forum. Haya yanahusu yangu aanze elimu ya huu mpaka masters. Tuomba tena like kipindi cha "this week in perspective" wapambanishwe na John Mnyika ndiyo mjue huyu bwana alivyomwepesi Kwa Mnyika.
 
CCM bana

Yeye anayetuhumu wengine kwa kutoa matamko bila vikao, yeye ametumia kikao gani kutoa tamko lake?.

Chama kimemshinda kukiongoza mkoani Shinyanga halafu anataka kufundisha wengine jinsi ya kukiongoza.

Viongozi wote mkoani Shinyanga wanapiga majungu badala ya kufanya kazi kwa mujibu wa taratibu, kanuni na katiba ya chama chao.

CHADEMA wakisimamisha wagombea wazuri katika mkoa wa Shinyanga, ninaamini wanaweza kuchukua kata na majimbo yote ya uchaguzi.

Kwa mkoa wa Shinyanga, CCM is slowly dying
 
Kwa mara nyingine wajumbe mbali mbali wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi wamezidi kukemea uhuni unaofanywa na baadhi ya makada wa chama hicho hasa Nape, kwa kutoa kauli za uchonganishi na bila kufata utaratibu na kanuni za chama.

Naomba nisiongee sana, pitia attachement hapo chini.

Asanteni
Ocampo four

Msemakweli ni mpenzi wa Mungu. Muacheni Nape afanye kazi. Shida yako(na vijana wenzio wa E.L) mnaumia sana mtu anaposema issue ya Ufisadi na Uchafu.

Anatatizo gani Nape kusema kuwa "CCM haitachagua mtu mchafu??). Na nikwanini #team_lowasa pekee ndo mje kutoa povu na kulialia ovyo namna hii?

Nawaambia mme'wrong number huko. Nawasihi mtengeneze mipango mizuri faster wakati huu mchache uliobaki mzirambe kwelikweli kwani baada ya "uteuzi" ndo itakuwa ZE END ya team yenu.

Lowasa is totally rotten in this country.
 
Huyu Mzee alikuwa anajaribu kusema nini?so vague.Why coming out with such ambiguous statement?ni kujipendekeza kwa Boss wake Lowassa tu ndo kumemsukuma kutoa statement hii ama nini?
 
Hii ndiyo Bongo Darisalam...lol!

Ni kuganga njaa kwa kwenda mbele. Kwa haraka ya mshiko hata hakuwa na muda wa kuhariri taarifa yake!

Ni kweli kabisa mapesa ya Lowassa huyu yanamsumbua kaona Jk muda wake karibu unaisha soko limeanza kurudi kwa Lowassa nae kaanza kujipendekeza
 
Tokea lini kawa mtumishi wa Lowassa, acha kuongea kama mwanamke mpumbavu (mke wa Ayubu)...... Nape hana cha kupoteza ndani ya ccm kwa sababu ana chama alichokianzisha ccj.....

Uko sahihi kabisa huyu Mzee katumwa na Jizi Lowassa
 
Hii ni vita baina ya CCM maslahi na CCM imani, inaniwia vigumu kujua kundi maslahi ni lipi kati ya team Membe na team Lowassa, kwa sababu kati ya wote sioni CCM imani hapo.
 
mwaka huu kazi kweli kweli! mimi kama mwanachama wa ccm naweza nayaona yafuatayo;
1. Hakuna kiongozi hata mmoja ndani ya chama chetu ambae hayuko kwenye kundi la mgombea fulani kuelekea uchaguzi mkuu ujao.
2.kuna viongozi ambao dhahili wanachukizwa na hali ya mambo iliyopo ndani ya ccm kuelekea uchaguzi mkuu na kura za maoni na kuna wengine ni wanafiki tu wanatengeneza mapito ya wanaopenda wapitishwe na chama.
3. kuna wanachama wenzetu ambao wao wanajiona ni wanachama wa daraja la juu kuliko wanachama wengine na wanaweza kumkaripia mwanachama mwenzao,kumtishia chochote na hata kumtengenezea scandle.
4.kuna wanachama wenzetu wachumia tumbo wanao taka fulani apitishwe ili walipwe fadhila wapewe vyeo ama vya kisiasa au kiutendaji kama si wao moja kwa moja basi ndugu zao na hali hii ni hatari sana kwa mstakabali wa nchi yetu maana taifa litakuwa na viongozi wajinga na wenye upeo mdogo wa uelewa wa mambo.
6.kuna kundi linalo penda kazi ya nape na kuna kundi linalo lia na nape usiku kucha kuwa hafai toka kapewa nafasi ya uenezi na kuna kundi lonalo mbariki nape na kazi zake zote.hawa wanaamini kuwa napenanaendana na kasi ya siasa za ushindani.
6.kuna mitandao hatari imeundwa na wagombea kutengeneza mikakati isiyo shindwa kuhakikisha wagombea wao wanapitishwa kwenye kura za maoni kwa gharama yoyote ile ikiwemo kuchafuana kwenye media n.k na hawa ndiyo mgenja analia nao bila shaka.
7.viongozi wa ccm akiwemo nauye wanahubiri sana kufuata misingi na taratibu za chama kwenye nafasi ya urais tu wakati hali iliyopo kwenye majimbo ni mbaya sana watu wanatamani kutoana roho na mbaya zaidi watu wa meandaa milima ya hela kwaajili ya ubunge tu.
Kwa mantiki hiyo alichp sema mzee mgenja hata kama mfuasi wa lowasa yilo sahihi inatakiwa ccm ichukuwe tahadhali nyingi dhidi ya makundi ya wagombea tofuti na hivyo ijiandae kwa mpasuko mkubwa ambao unaweza kugharimu sana chama kwenye uchaguzi ujap
 
Katika hali inayoashiria kuwapo kwa mgawanyiko mkubwa kuelekea katika kuteua mgombea urais ndani ya CCM na pia kumjibu Katibu Mwenezi wa CCM Bw. Nape Nauye, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga Bw. Hamis Mgeja amesema hakuna aliye na hati miliki ya chama hicho kikongwe nchini!

Aidha Mgeja amewaonya viongozi wa chama hicho kuacha mara moja kuwatisha makada wake wanaotangaza nia ya kuwania nafasi ya kugombea urais kupitia CCM! Hii ni baada ya Nape kuweka vikwazo na hatua sita ambazo chama hicho kitazitumia kupata mgombea wake!

Chanzo: Magazeti asubuhi Star TV.

My take: Kuna uwezekano mkubwa tukashuhudia mtifuano ambao haujawahi kutokea tangu mwaka 1977 CCM ilipozaliwa! Tusubiri tuone sinema ya buree!!
 
Mgeja ni Lowasa!!!na shinyanga,mwanza,geita ndiyo mikoa yenye wapiga kura wengi
 
Mgeja ni Lowasa!!!na shinyanga,mwanza,geita ndiyo mikoa yenye wapiga kura wengi


Lakini ameongea vitu sahihi hakuna mwenye mamlaka ya uumbaji au hati miliki ndani ya CCM waache siasa za chuki na fitina.
 
Katika hali inayoashiria kuwapo kwa mgawanyiko mkubwa kuelekea katika kuteua mgombea urais ndani ya CCM na pia kumjibu Katibu Mwenezi wa CCM Bw. Nape Nauye, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga amesema hakuna aliye na hati miliki ya chama hicho kikongwe nchini!

Aidha Mgeja amewaonya viongozi wa chama hicho kuacha mara moja kuwatisha makada wake wanaotangaza nia ya kuwania nafasi ya kugombea urais kupitia CCM! Hii ni baada ya Nape kuweka vikwazo na hatua sita ambazo chama hicho kitazitumia kupata mgombea wake!

Chanzo: Magazeti asubuhi Star TV.

My take: Kuna uwezekano mkubwa tukashuhudia mtifuano ambao haujawahi kutokea tangu mwaka 1977 CCM ilipozaliwa! Tusubiri tuone sinema ya buree!!



Namuonea huruma Nappe na shobo zake siku atakaposalimu amri....

Namuonea huruma sababu anayemtuma kazi hana uwezo wakusimamia anachoamini mpaka mwisho...

Chuki binafsi na visasi vitamtokea puani huyu mpuuzi.
 
Back
Top Bottom