RockSpider
JF-Expert Member
- Feb 16, 2014
- 6,859
- 2,758
Nape Mnauye aka Mnauye Jr ni member humu ndani, badala ya kuwatumia akina Msalani pale Lumumba aje humu apate elimu ya Bure...
Kwa mara nyingine wajumbe mbali mbali wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi wamezidi kukemea uhuni unaofanywa na baadhi ya makada wa chama hicho hasa Nape, kwa kutoa kauli za uchonganishi na bila kufata utaratibu na kanuni za chama.
Naomba nisiongee sana, pitia attachement hapo chini.
Asanteni
Ocampo four
Mkuu uwe unaunganisha dots, Khamis Mngeja ni mfuasi wa Lowasa everybody knows it, nafikiri Khamisi alikerwa na matamshi ya Nape ambayo yapo humu pia, ingawa sisi wengine haya tuhusu but pitia hapa ujikumbushe.https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...aihitaji-mgombea-wa-kusafisha-kwa-dodoki.htmlSijaona alipomtaja Nape au macho yangu hayaoni vizuri? Hhahhaa!
Sasa yeye katumia vikao gani?
Ni TAMKO,jambo la msingi kwamba mfikishie ujumbe rafiki yako Membe kuwa aache siasa za kitoto.
mwaka huu kazi kweli kweli! mimi kama mwanachama wa ccm naweza nayaona yafuatayo;
1. Hakuna kiongozi hata mmoja ndani ya chama chetu ambae hayuko kwenye kundi la mgombea fulani kuelekea uchaguzi mkuu ujao.
2.kuna viongozi ambao dhahili wanachukizwa na hali ya mambo iliyopo ndani ya ccm kuelekea uchaguzi mkuu na kura za maoni na kuna wengine ni wanafiki tu wanatengeneza mapito ya wanaopenda wapitishwe na chama.
3. kuna wanachama wenzetu ambao wao wanajiona ni wanachama wa daraja la juu kuliko wanachama wengine na wanaweza kumkaripia mwanachama mwenzao,kumtishia chochote na hata kumtengenezea scandle.
4.kuna wanachama wenzetu wachumia tumbo wanao taka fulani apitishwe ili walipwe fadhila wapewe vyeo ama vya kisiasa au kiutendaji kama si wao moja kwa moja basi ndugu zao na hali hii ni hatari sana kwa mstakabali wa nchi yetu maana taifa litakuwa na viongozi wajinga na wenye upeo mdogo wa uelewa wa mambo.
6.kuna kundi linalo penda kazi ya nape na kuna kundi linalo lia na nape usiku kucha kuwa hafai toka kapewa nafasi ya uenezi na kuna kundi lonalo mbariki nape na kazi zake zote.hawa wanaamini kuwa napenanaendana na kasi ya siasa za ushindani.
6.kuna mitandao hatari imeundwa na wagombea kutengeneza mikakati isiyo shindwa kuhakikisha wagombea wao wanapitishwa kwenye kura za maoni kwa gharama yoyote ile ikiwemo kuchafuana kwenye media n.k na hawa ndiyo mgenja analia nao bila shaka.
7.viongozi wa ccm akiwemo nauye wanahubiri sana kufuata misingi na taratibu za chama kwenye nafasi ya urais tu wakati hali iliyopo kwenye majimbo ni mbaya sana watu wanatamani kutoana roho na mbaya zaidi watu wa meandaa milima ya hela kwaajili ya ubunge tu.
Kwa mantiki hiyo alichp sema mzee mgenja hata kama mfuasi wa lowasa yilo sahihi inatakiwa ccm ichukuwe tahadhali nyingi dhidi ya makundi ya wagombea tofuti na hivyo ijiandae kwa mpasuko mkubwa ambao unaweza kugharimu sana chama kwenye uchaguzi ujap