URAIS 2015: Benard Membe apata pigo jingine

URAIS 2015: Benard Membe apata pigo jingine

mwenye akili timamu atajua dhumuni la hii ngonjela yako.hakuna cha zaidi ya siasa chafu na kujaribu kufanya penitration kwa jamii to potray interest binafs against membe.ijulikane tu watu hawamchagui membe kwasababu ya gotham bali kwa kumwamni membe mwenyewe nakuona anafaa.ikitokea uthibitishe juu ya madai yako kwamba membe anabebwa na nyota ya mama salma will u be in a pisition.news with no source have no power to convice and converted to just a poem.INAWEZEKANA KATIKA UCHAGUZI UJAO AKAPATIKANA RAIS KUTOKA NJE YA CHAMA CHA MAPINDUZI LAKIN RAIS BORA ATAPATIKANA KUTOKA NDANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI MWENYE WEREDI MKUBWA MWAMINIFU MUADILIFU NA AMBAYE MWENYE NIA YA DHATI KABISA KATOKA KULITUMIKIA TAIFA PASIPO KUWA NA VIGUGUMIZI KATIKA MAAMUZI.MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE

Kwa uchambuzi na maoni yako mkuu kwa sifa ulizozihainisha bila shaka atakuwa ni Mizengo Pinda ndiyo kiongozi pekee mwenye sifa hizo mwaminifu,muadilifu na huwa anafanya maamuzi sahihi na makini wakati wote huwa hakurupuki kama ambavyo wengine huwa wamekuwa wakikurupuka kwa kufanya maamuzi magumu yasiyo sahihi na kuitia serikali hasara kubwa tumeshuhudia kwa Edward Lowassa na kwa Membe pia
 
Sasa Membe atabaki na nani wakuu??

Mkuu siasa ni mchezo wa ajabu sana; nimeona hoja mbili, ya kwanza Membe hauziki kwa sababu hayuko karibu na watu.

Ya pili Membe anatumia nyota ya mama Salma kuuzika katika eneo la ukanda wa pwani, na kwamba kwa sasa mama Salma nae amemchoka sababu ni ileile, hauziki. Jambo la kujiuliza hauziki kivip?

Gotham anasemwa kuwa ameona Pinda anafaa, kivip Pinda anafaa?Kwa maoni yangu hizi ni timing zile zile za upepo wa escrow, mseme mwenzio aonekane hauziki bila sababu za msingi, wakati huo huo unasifia upande wa pili!!

Acha ibaki kuwa tetesi, ila siasa ni mchezo wa ajabu sana.
 
Wapambe wa wagombea mna tabu.mleta uzi ww ni mpambe wa lowasa sio.kazi mnayo huu mwaka
 
Sasa wandugu kwa hali ilivyo kwa sasa pinda taayari ameshanusa ikulu kila mtu sasa anakimbilia tunda zuri mtini Gotham simlaum ameona ni wapi kwenye muelekeo wa mafanikio na kwenye mikono ya hekima na busara.
 
Sasa wandugu kwa hali ilivyo kwa sasa pinda taayari ameshanusa ikulu kila mtu sasa anakimbilia tunda zuri mtini Gotham simlaum ameona ni wapi kwenye muelekeo wa mafanikio na kwenye mikono ya hekima na busara.
Mushi unachosema ni sahii pinda namkubali sana yupo makini a ajua anafanya nini na anamalengo gani anahofu namungu huyo ndio rais tunaemuitaji.
 
Ana kashfa ya kula pesa za Ghaddafi, kashfa ya vitambulisho vya taifa, kuficha hela uarabuni, kuvujisha siri za serikali

Anatembea na briefcase ya madola Huyo ya Ghadafi .....Vitambulisho lazima Mwaimu afungwe ..vitambulisho gani hata Posta tu hapo miaka imepiga watu hawajavipata...Je kule Kwetu Mtowisa vitafika lini ??. Si bora leseni Za TRA driving ....,Huyo Omar Mjenga ...Karani wake Dubai na uarabuni ...ndiye anafanya kazi ya Omba Omba wa Membe Badala ya kazi aliyotumwa na Taifa .
Damu ya Yule balozi aliyeuwawa inalia!!!!,
 
atabaki na wapiga kura mkuu.ndiye kiongozi ambaye anaonekana anauwezo asiye na skendo za wiz.

Lakini sasa sio wakati wa kuleta hizi porojo. Mtapuzwa na wengi hata kama mnaweza kuwa mlitaka wtu waujue ubaya wa mnaempigia debe. Mpaka anawatuma ina maana hajiamini??
 
Mpambe nambari moja wa waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa katika mbio za Urais nchini bwana Jack Steven Gotham anacheza miguu miwili kwenye siasa ya Urais, imebainika. Mpambe huyu ambaye ni maarufu kiasi kutokana na ukaribu wake na Membe, ndiye anayetajwa kufanya kazi ya ndani za Bernard Membe ikiwemo kufanya vikao vya kuwashawishi wajumbe wa NEC ya CCM wamuunge mkono Membe, kushika mkoba wa fedha za kuwalipa wajumbe na mikakati mingine. Jack sasa amepata jina jipya la Christian Ronaldo wa Urais.

Jack Gotham ni kijana wa karibu sana wa Membe ambaye amesaidiwa kupata mafanikio aliyonayo kiuchumi ikiwemo kushinda tenda ya Vitambulisho vya taifa, lakini hivi karibuni baada ya ujio wa waziri mkuu Mizengo Pinda katika mbio za Urais, Gotham ameyumba. Inasemekana kambi ya waziri mkuu ilikutana na Gotham kumuomba awe upande wao, kikao kilichofanyika nyumbani kwa kigogo mmoja eneo la Oysterbay jijini Dar es salaam. Bwana Gotham alitafakari na kuwaletea jibu baada ya siku chache kuwa anamuunga mkono Pinda kwakuwa Membe amekuwa hauziki na ni ngumu kumnadi kutokana na hulka na tabia yake ya kutokuwa karibu na watu.

Kwa kipindi chote cha katajwa kwa Pinda kwenye mbio za urais, msimamo wa Jack Gotham kwa Membe umeonekana kuyumba kwa kiasi kikubwa huku wakati mwingine aakionekana kuuma na kupuliza pande zote.

Jack Gotham anaendelea kukutana na vigogo wa juu wa team Pinda ikiwemo mke wa Pinda huku akimuhakikishia kuwa yeye Jack yako pamoja na Pinda katika mbio za Urais, na kwamba Membe ni rafiki yake, ila kwenye hili la Urais hauziki na hawezi.

Jack Gotham anaweza kumshambulia Edward Lowassa bila woga, lakini hana ubavu wa kumsema vibaya Pinda. Jack amewaelekeza baadhi ya vijana wa Membe kuwa wasimshambulie Pinda, jambo ambalo limeleta mgawanyiko makubwa.

Jack Gotham sasa ametunga udugu na Pinda, ambao anauita"ukaka". Amekaririwa akisema Pinda ni kaka yake na amemlea. Hii ni danganya toto ya kuficha usanii wake asionekane kuwa anamuunga mkono waziri mkuu Pinda. Hakuna udugu wowote baina ya wawili hawa, wala Pinda hakumlea Jack Gotham.

Jack Gotham anatoa siri za Membe kwa waziri mkuu Pinda lakini Pinda kwakuwa bado anamashaka nae amekuwa hampatii baadhi ya mipango yake ya ndani.

Jack Gotham anakutana na mzee Pinda na anavuta mzigo kama kawaida, huku pia akiendelea kukutana na waziri Membe na kuchukua dola za kimarekani.

Uamuzi huu wa Gotham katika mbio za urais unatajwa kumuweka katika wakati mgumu bwana Membe, kwakuwa kila siku ameendelea kupoteza wafuasi wake muhimu. Hata ukanda wa Pwani ambao ulikua ukiaminika kumuunga mkono, wajumbe wengi wa NEC wamemuhama Membe na kuhamia kwa mtoto wa mkulima. Mama Salma Kikwete anatajwa kuwa sasa ameanza kamchoka Membe na ameanza kujiondoa taratibu katika kumuunga mkono. Nyota ya mama Salma Kikwete ndiyo iliyokuwa inambeba Membe kisiasa na kufanya aungwe mkono ukanda wa Pwani.

Minong'ono imeanza kujitokeza kwa watu wa karibu na Membe juu ya msimamo wa meneja wao Jack Gotham. Aidha team Pinda pia imeanza kuhoji kwanini mtu huyu hachagui moja, kama anamuunga mkono Pinda au Membe. Hii inamuweka Gotham katika wakati mgumu na kumfananisha kama mtu aliyepanda farasi wawili, atapasuka msamba.
Jack Gotham ameamua kuwa Christian Ronaldo.
NIMEKUFUATILIA VIZURI SANA.

Uchambuzi wako umeenda swadakta zaid ya maelezo. Hauko "bias" kabisa.

Asante sana. Nadhani atakuwa ameoteshwa kuwa,mtoto wa mkulima ndio mwenye kifua cha kumaliza mbio hizi za #marathon .
 
unatumia nyasi aka ganja ama viroba? wakuongezeee ngapi?....
Kwa uchambuzi na maoni yako mkuu kwa sifa ulizozihainisha bila shaka atakuwa ni Mizengo Pinda ndiyo kiongozi pekee mwenye sifa hizo mwaminifu,muadilifu na huwa anafanya maamuzi sahihi na makini wakati wote huwa hakurupuki kama ambavyo wengine huwa wamekuwa wakikurupuka kwa kufanya maamuzi magumu yasiyo sahihi na kuitia serikali hasara kubwa tumeshuhudia kwa Edward Lowassa na kwa Membe pia
 
Leo vigogo wa CCM kupima nguvu zao kuipitia escrow. Ni Membe, Lowassa, Mkono kwa upande mmoja dhidi ya Pinda mtoto wa mkulima.
 
Back
Top Bottom